Saturday, January 31, 2015

XAVI: BIFU LA MESSI MESSI & KOCHA KWISHINEYI!!

Moja ya mechi ambazo Messi alipigwa benchi msimu huu, jambo ambalo si rahisi kusikia kwa nyota huyo.


KIUNGO mwenye heshima ndani ya Barcelona, Xavi Hernández kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu sakata la kutoelewana kwa nyota wa klabu hiyo, Leonel Messi na kocha wake, Luis Enrique ambapo amesema kuwa wawili hao wamemaliza tofauti zao na mambo ni shwari kwa sasa.
Messi na Luis wamekuwa wakiripotiwa kutokuwa na maelewano mazuri na kwamba walikwaruzana kwenye mazoezilakini Xavi amefunguka kuwa. "Kila kitu kimeeleweka, sio ishu kubwa kwa sasa. Kuanzia kwenye makundi yao, tumelichukulia kwa ukubwa unaostahili, lilitokea lakini sasa limebaki historia.
 Akizungumzia timu yake Xavi alisema: "Kila mmoja na shauku ya ushindi. Kila mmoja anajisikia ari ya kushinda na tupo tayari katika hilo."

Amekwenda mbali na kummwagia sifa Neymar kwa kusema: "Ni mchezaji wa kipaji cha juu na tunajisikia faraja sana kuwa naye katika kikosi chetu. Ni mtu wa kipekee ana aina yake ya uchezaji, mwenye uelewa mkubwa wa soka na maisha ya yake anayoishi ni tofauti kabisa. Unatakiwa kujua jinsi gani ya kushinda, kushindwa, lakini hilo ni tofauti kwa Neymar. Ana maisha yake fulani hivi.
Xavi Hernanedz

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...