Saturday, January 31, 2015

KOCHA FIORENTINA: CUADRADO SIO WETU TENA, ANAENDA CHELSEA

Hatua moja mbele...kiungo wa Colombia na Fiorentina Juan Cuadrado anaenda Stamford Bridge muda wowote.
Kocha wa Fiorentina, Vincenzo Montella amefunguka kuwa kiungo wa timu hiyo, Juan Cuadrado atajiunga na Chelsea na kuongeza kuwa licha ya kumhitaji lakini isingekuwa rahisi kumbakiza kutokana na ofa kubwa waliotangaziwa ambayo katu kama klabu wasingeipiga chini.
Matajiri wa London, Chelsea, wanatajwa kutenga kitita cha euro milioni 35 kwa ajili ya kuansa saini kiungo huyo raia wa Colombia pamoja na kuwaongezea Mohamed Salah kwa mkopo.
Licha ya kwamba mpaka sasa pande mbili hazigongeana mihuri ya uthibitisho wa biashara hiyo, lakini Montella amesema kuwa anamchukulia Cuadrado kama mchezaji wa zamani wa Fiorentina alipoongea kwenye mkutano wa habari jana Ijumaa jioni.
"Isingewezekana kwa kukwamisha dili lake," alisema Montella. "Kwa mtazamo wangu kama kocha inakatisha tamaa lakini klabu ilikuwa na haki ya kufanya hivyo.
"Mchezaji wa kiwango cha juu ameondoka, ingawa bado naona sifa zake kwa Salah (mbadala wake). Sidhani kumuuza ni sababu yetu kurudi nyuma. 

[Cuadrado] ni mchezaji wa kimataifa  na siku zote alipenda kuwa nasi , pia na mimi najivunia kuwa anakwenda kujiunga na timu kubwa duniani."
Cuadrado kushoto katika moja ya mechi alizoichezea Fio msimu huu, hapa akijaribu kumpita moja wa mabeki wa AS Roma

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...