Friday, January 29, 2016

HATIMAYE TIMU YA GENK YA UBELIGIJI IMEMALIZANA RASMI NA SAMATTA


Mbwana Samatta akipasha viungo vyake.
Katika dakika ya mwisho KRC Genk hatimaye imemnasa mshambuliaji iliyotumia muda na maarifa kuinasa saini yake kutoka katika klabu yake ya TP Mazembe. Samatta aliwasili jana Brussels na alisafiri moja kwa moja kuelekea Genk .

Aly Mbwana Samatta (° aliyezaliwa Dar es Salam 23 Desemba 1992 , 1.80 m na 75 kg) ni mchezaji anayeweza kutumia miguu yake yote kwa ufasaha na mshambuliaji ambaye pia anaweza kucheza kama winga wa kulia. Ametoka Kongo katika klabu ya TP Mazembe.
Samatta (kushoto), akiwania mpira.


Akiwa pamoja na klabu hii alishinda taji la klabu bingwa Afrika 2015, alikuwa mshindi mara nne mfululizo wa ubingwa wa Kongo na mshindi wa Supercup mara mbili. Samatta amefanikiwa kuchaguliwa mara ishirini kwa timu ya taifa ya nchi yake nyumbani Tanzania . Katika michezo hiyo, alifunga mabao saba.

Katika msimu wa 2015 alichaguliwa kuwa mchezaji bora kwa wale wanaocheza ligi za ndani za bara la Afrika . Amekubali kusaini mkataba hadi mwisho wa msimu 2019-2020.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...