Tuesday, February 24, 2015

KINDA LA MAN U MIAKA 18 LAPIGA BAO LA MITA 40!

 Kinda wa Manchester United, aliye kwenye kiwango kwa sasa, Oliver Rathbone amefunga bao la mwaka, baada ya usiku wa kuamkia leo kupiga bonge la bao, mita 40 na kuipa ushindi Man United ya vijana (U-18) wa mabao 2-1 dhidi ya Derby. Cha kuvutia zaidi ni kwamba bao hilo lilikuwa ni la dakika ya 90.

Kinda huyo anayemudu nafasi ya kiungo, alijiunga na United mwaka 2013, bao lake linafananishwa na lile la kptaini Wayne Rooney ‘Wazza’ alililofinga dhidi ya West Ham mwaka jana. Lakini la Wazza linatajwa kuwa la umbali wa mita 20 zaidi, lakini yanafafana katika 'action'.
Ushindi huo umeipaisha United hadi nafasi ya tatu kwenye ligi ya vijana, inayoongozwa na Middlesbrough.
 
bofya link hapa chini kuangalia 'muwa' huo uliopigwa na dogo.


https://vine.co/v/OQO7innHiT7

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...