Saturday, May 17, 2014

DIAMOND AFUNIKA KWENYE MBIO ZA KUELEKEA KWENYE TUZO ZA MTV BILICANAS


Diamond akizungumza jambo mbele ya watu waliokusanyika ndani ya Ukumbi wa Billicanas
Staa wa wimbo wa Number One, Nasibu Abdul 'Diamond', jana alikuwa ndani ya Ukumbi wa Billicanas kuzungumzia juu ya hatua kubwa aliyopiga hadi kuwepo katika Tuzo za MTV ambazo zinatarajiwa kufanyika hapo baadae mwaka huu.

Diamond na wasanii wengine kama Sauti Soul kutoka Kenya walikuwepo ndani ya ukumbi huo ambapo mbali na kuzungumzia furaha ya kuteuliwa, baadaye wasanii mbalimbali ambao wameteuliwa katika kinyanganyiro hicho walitumbuiza mmoja baada ya mwingine.
Waandishi wa habari na wadau mbalimbali waliokusanyika ndani ya ukumbi huo.
Muigizaji Wema Sepetu akihojiwa na mwandishi wa habari ndani ya ukumbi huo kuhusiana na uteuzi wa Diamond kuwania Tuzo za MTV.Kulia ni mwigizaji mwenzake, Aunt Ezekiel.
Wasanii kutoka Kenya, Sauti Soul wakitumbuiza ndani ya Ukumbi wa Billicanas
Diamond akiwaburudisha mashabiki waliofurika ukumbini humo.
Mashabiki wakiburudika vilivyo ndani ya Ukumbi wa Bilicanas ambapo Diamond na wasanii wengine walikuwa wakifanya yao.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...