Friday, December 27, 2013

WANASOKA WALIVYOJITOKEZA KUUAGA MWILI WA KOCHA WA MAKIPA SIMBA SC

 
Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Kocha wa makipa wa Simba, marehemu James Kisaka likiingizwa kwenye basi la klabu hiyo, baada ya kutolewa heshima za mwisho katika misa iliyofanyika katika Kanisa la Muhimbili, Dar es Salaam. Marehemu Kisaka atasafirishwa kwenda kwao wilayani Muheza, Tanga kwa mazishi yatakayofanyika leo.
Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo 'Julio', (kushoto) akijadiliana jambo na baadhi ya wachezaji wa soka waliokwenda kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu James Kisaka.
 
Mjane wa marehemu James Kisaka, Teddy Kisaka akifarijiana na mtoto wa pili wa marehemu Kisaka, Boniface baada ya kutoa heshima za mwisho.
Ndugu wa karibu wa marehemu Kisaka akilia alipokuwa akitoa heshima za mwisho

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...