Wednesday, December 25, 2013

AIRTEL YAWATAKIA WATANZANIA HERI SIKUKUU YA KRISMASI


-Airtel yawatakia Watanzania heri ya sikukuu
-Yazidi kutanua kifua kwamba ni Baba lao
Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel imewaasa Watanzania wote kote nchini kulinda amani na utulivu wa nchi katika kipindi hiki cha sikukuu ikiwa ni baada ya kuwatakia heri ya Christmas na mwaka mpya.

Akizungumza kwenye ofisi za makao makuu ya Airtel, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema sikukuu za Christmas na mwaka mpya ni sikukuu muhimu sana kwa wananchi wa taifa hili hivyo zinapaswa kusherehekewa kwa amani na utulivu.

“Ninawaomba wateja wa Airtel na watanzania wote kwa ujumla kutambua umuhimu wa sikukuu hizi na kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuhatarisha amani na utulivu wa taifa,” alisema Mmbando.

Aidha alisema katika msimu huu wa sikukuu bado Airtel inazidi kudhihirisha kuwa ni baba lao kwa wateja wake kwa kutoa huduma zilizo za gharama nafuu zinazowawezesha kutuma na kupokea pesa bure pia kutumia huduma mbalimbali za inataneti na kupiga kwenda mitandao yote.

“Airtel bado ni baba lao kupitia huduma zetu mbalimbali, Wateja wetu bado wanaweza kunufaika na huduma zetu ambapo kwa sasa wateja wanaweza kupata vifurushi vya inataneti kwa gharama nafuu, kupiga simu kwenda mitandao yote na pia kutuma na kupokea pesa bure,” alisema Mmbando.

Ikumbukwe kuwa vifurishi vyote vya siku vya Yatosha vinadumu kwa masaa 25 tangu mteja anapojiunga ikiwa na lengo maalumu la kumfanya mteja aweze kufurahia huduma hiyo na kuwafaidisha watanzania waendelee kuokoa pesa nyingti walizokuwa wakizitumia kwenye mawasiliano na kuanza kuzitumia katika shughuli nyingine za uchumi wa taifa na jamii kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...