Wednesday, July 24, 2013

RAY C NA RECHO KUFANYA BONGE LA KOLABO


Mwanamuziki wa kitambo Rehema Chalamila maarufu kama Ray C ana matarajio ya kurudi katika game baada ya kuwa fiti sasa kiafya. Kupitia mtandao wa instragram Ray C amekuwa akitupia picha zinazomuonyesha akiwa na afya nzuri tena kanona si haba!

Watu wengi wamekuwa wakimuhoji kupitia mtandao huo kuhusiana na mwanamuziki Recho kutumia style inayofanana na Ray C kama anafurahia au lah huku kukiwa na nmafikirio huenda hapendezwi na kitu hicho lakini ukweli ni kuwa Ray C anamfurahia na hivi karibuni wanarajia kudondosha kolabo kwa mujibu wa alichokiandika Instagram.
Alianza kwa kupost picha ya Recho..

Kisha akaandika maelezo..


Katika interview kadhaa Recho ameshawahi kukiri kuwa alivutiwa na Ray C kuingia katika muziki na ni mmoja katika ya wanamuziki anaowazimia mpaka leo na ndio maana style zao za uimbaji na uchezaji zinafanana.Ray C pia aliwahi kuandika ujumbe wa kuwashukuru mashabiki wake kwa kumsapoti alipopata matatizo ya kiafya mpaka leo.
Najaribu kuvuta picha ya kolabo ya wawili hawa halafu siipati hiyo picha yenyewe

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...