Thursday, August 30, 2012

MISS KANDA YA MASHARIKI WATEMBELEA VYOMBO VYA HABARI MORO

Meneja Mkuu wa Abood Media, Julius Nyaisangah (Uncle J) akitoa ufafanuzi kwa warembo hao walipokuwa ndani ya Radio Abood na Abood Television.

WAREMBO 12 wanaowania taji la Redd's Miss Kanda ya Mashariki 2012 linalotarajiwa kushindaniwa Septemba 1 ndani ya Hoteli ya Nashera, jana jioni walitembelea baadhi vyombo vya habari vya mkoani Morogoro.
Warembo hao kutoka mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani na wenyeji Morogoro, walitembelea vyombo vya Abood Media vilivyo eneo la Msamvu, na kujionea jinsi vinavyoendeshwa.
Mratibu wa shindano la Redds Miss Kanda ya Mashariki 2012, kutoka Kampuni ya Nepa Production & Events, Alexandra Nikitasi akiwaongoza warembo hao katika ofisi za Abood Media.
Warembo hao wakiwa katika pozi kwenye ofisi za Abood Media.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...