Monday, July 30, 2012

VODACOM YATOA TUZO KWA WAMILIKI WA BLOG


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twisa, akizungumza jambo muda mfupi kabla ya zoezi la utoaji tuzo kuanza.
 
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom, mapema leo imetoa tuzo kwa baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari, mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twisa, alisema tuzo hizo ni mpango wa kampuni hiyo kutambua, kuendeleza na kuongeza jitihada na maudhui katika mitandao ya kijamii na tovuti, na kuthamini mchango wa waandishi katika utoaji wa taarifa kwa jamii.
Washindi 10 katika kipengele cha mitandao ya jamii na tovuti ni wafuatao:
1: Elsie Eyakuze wa Mikocheni Report
2: Muhidini Michuzi wa Issa Michuzi Blog.
3: John Kitime wa Wanamuziki Tanzania Blog
4: Masoud Kipanya wa Kipanya .co.tz
5: Umoja wa Vijana FM
6: Millard Ayo wa Millardayo.co
7: Miriam Rose Kinunda wa Taste of Tanzania
8: Mike Mushi wa Jamii Forums
9: Rachel Hamada wa Mambo Magazine
10: Fatma Hassan wa DJ Fetty Blog.
Washindi hao wanawawakilisha wengine wengi wanaoonyesha vipaji vyao ambapo pia mchango wao unahitajika kuthaminiwa.

Mmoja wa washindi wa tuzo hizo, Masoud Kipanya (kulia), akipokea zawadi zake kutoka kwa Kelvin Twisa, huku akishuhudiwa na mmoja wa wasimamizi wa zoezi hilo kutoka Vodacom.

DJ Fetty (kulia) akipokea zawadi zake.

John Kitime (kulia) akituzwa.

Baadhi ya wadau na viongozi wa utoaji tuzo hizo wakiwa pamoja baada ya zoezi hilo.
Meneja Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (katikati), akishuhudia zoezi hilo na baadhi ya wageni wengine waliofika mahali hapo.


Baadhi ya waalikwa na wanahabari wakifutilia kwa makini zoezi la utoaji tuzo hizo.






No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...