Azam FC wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Jamii kwa uifunga Yanga kwa penati 4-1, leo kwenye Uwanja wa Taifa baada ya timu hizo kumaliza kwa sare ya mabao 2-2.
Yanga ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata mabaop yake kupitia kwa Donald Ngoma ambapo mpaka dakika 45 zinakamilika matokeo yalikuwa 2-0 lakini kipindi cha pili hali ilibadilika na Azam kufanikiwa kusawazisha kupitia kwa Shomari Kapombe na John Bocco.
Hivi sasa msimu wa 2016/17 umefunguliwa rasmi ambapo mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara zinatarakiwa kuanza wikiendi ijayo katika viwanja tofauti.
No comments:
Post a Comment