|
Mkurugenzi wa Duka la Zizzou Fashion, Athumani
Tippo (kushoto), akimkabidhi vifaa vya michezo kocha wa timu ya Changanyikeni
Rangers, Steven Nyenge ndani ya duka hilo lililopo maeneo ya Sinza Afrikasana
jijini Dar es Salaam. |
DUKA
la vifaa vya michezo la Zizzou Fashion mapema leo lilijitolea kutoa msaada wa vifaa
vya michezo kwa timu ya soka ya Changanyikeni Rangers inayoshiriki Ligi Daraja la
Pili.
Akizungumza
katika makabidhiano hayo Mkurugenzi Zizzou Fashion, Athumani Tippo alisema
kwamba, amelazimika kutoa mchango wake kwa timu hiyo kutokana na kuonyesha juhudi,
uwezo na kujituma kwa wachezaji wa timu hiyo kwa muda mfupi tangu
ilipoanzishwa.
“Niameamua
kutoa mchango wangu wa vifaa vya michezo kwa timu hiyo kwani imenishawishi
baada ya kuifuatilia kwa muda sasa ambapo nimeziona juhudi za kocha wao, Steven
Nyenge na wachezaji wote kwa ujumla wanavyojituma kuhakikisha wanapanda
daraja,” alisema Tippo.
|
Tippo akiwa katika pozi na kocha wa timu ya
Changanyikeni Rangers (katikati), na Kocha wa timu ya watoto ya Boko Beach
Veterani, Maswanywa |
MOSHI
VETERANI YAWACHAKAZA BOKO
|
Kikosi cha timu ya Boko Beach Veterani kikiwa
katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya mchezo huo kuanza. |
TIMU
ya wakongwe ya Moshi Veterani Wikiendi iliyopita iliitembezea kichapo Boko
Beach Veterani kwa bao 1-0 kwenye mechi ya kudumisha urafiki baina ya timu hizo
iliyopigwa kwenye Uwanja wa Boko jijini Dar es Salaam.
|
Nahodha Moshi Veterani, Jafari Kiango (kushoto), akimkabidhi
mchezaji wa timu ya Boko, Godfrey Malekano ‘Messi’, zawadi ya Mchezaji Bora wa Mwezi kwa niaba ya
Zizzou Fashion, muda mfupi baada ya kumalizika kwa mchezo huo.
|
No comments:
Post a Comment