Musa Mateja
SHAKA! Familia ya ‘President’ wa Kruu ya Wasafi, Nasibu Abdul
‘Diamond Platnumz’ imeamua kuweka kikao kummbana staa huyo aweke wazi
kama ni kweli ana uhakika mimba aliyonayo mjasiriamali Zarinah Hassan
‘Zari’ ni ya kwake au magumashi, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na familia ya staa huyo, ndugu wa
karibu akiwemo mama, binamu yake Romy Jons, wajomba zake, mameneja na
marafiki wa karibu wa familia, waliamua kuweka kikao hicho usiku hivi
karibuni ili Diamond athibitishe kama kweli kiumbe kinachoripotiwa kuwa
ni cha kwake magazetini ni chake kweli.
“Ndugu walichachamaa, walitaka kujua kama kweli mimba inamhusu Diamond au ni magumashi ya kiki za vyombo vya habari.
“Kwenye hicho kikao walimualika na Diamond mwenyewe ili aweze
kufunguka kama ana uhakika kweli mimba ni yake,” kilisema chanzo hicho
WALITAKA ATOE MSIMAMO
“Mbali na kutaka kujua kama mimba ni yake, walitaka pia kujua ana
msimamo gani na Zari maana kila kukicha wanasikia mambo tofauti katika
mitandao na vyombo vya habari,’’ kilisema chanzo hicho.
SABABU ZAZIDI KUANIKWA
Chanzo hicho kilipobanwa na mwanahabari wetu kuhusiana na sababu
zilizowafanya ndugu wa Diamond watilie shaka mimba hiyo, kilisema ni
kauli ambazo ziliwahi kusemwa na aliyekuwa mpenzi wake Penniel Mungilwa
‘Penny’ na aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga.
“Walishitushwa na kauli ambayo aliwahi kuitoa Penny kwamba Diamond
hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba lakini kama hiyo haitoshi,
waliitafakari kauli ya mume wa Zari ambaye alidai Zari hawezi kumzalia
Diamond ndiyo maana wakataka wapate uhakika,” kilisema chanzo hicho.
MUAFAKA WA KIKAO
Chanzo hicho kikizidi kumwaga ubuyu mbele ya kinasa sauti cha Risasi
Mchanganyiko kwamba, baada ya Diamond kubanwa na nduguze, alithibitisha
kuwa Zari ndiyo kila kitu kwake kwa sasa, hivyo wasiwe na shaka yoyote
juu ya kiumbe kinachotarajiwa kuzaliwa.
“Diamond aliwahakikishia kwamba mzigo ni wake, na msimamo wake ni kufika katika hatua ya ndoa Mungu akijalia.
KUMVISHA PETE
“Kuonesha yupo serious baada ya Diamond kuwatoa hofu ndugu zake,
alisema atafanya sapraiz siku ya Mei Mosi katika shoo ya mrembo huyo,
All White Party itakayofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini
Dar,” kilisema chanzo hicho na kudokeza kuwa Diamond atamvisha pete
mrembo huyo.
DIAMOND AFUNGUKA
Ili kuweza kupata ukweli, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond ili
aweze kuweka wazi juu ya kikao hicho na kama ni kweli anatarajia
kumvisha pete Zari. Diamond alifunguka:
“Yeah ni kweli ndugu zangu walikuwa na shaka lakini nimewahakikishia
kwamba kiumbe kilichomo tumboni mwa Zari ni mali yangu, kuhusu kumvisha
pete ni mapema kidogo kulizungumzia lakini watu wahudhurie kwa wingi
katika shoo ya Zari White Party Ijumaa hii pale Mlimani City kwani
nimeandaa sapraizi nyingi sana.
“Mei Mosi itakuwa ni siku ya kihistoria sana kwake kwani kuna mambo
muhimu mengi natarajia kumfanyia mpenzi wangu Zari, watu watajua rasmi
nia yangu kwa Zari maana ni mwanamke ambaye ameamua kujitoa kwa ajili
yangu, hivyo sina budi kumuonesha upendo stahiki, nitafanya kila
linalowezekana kumuonyesha namna gani nampenda.”
SHOO YA KIHISTORIA
Kwenye shoo hiyo ya Zari, watu mbalimbali mashuhuri wanatarajiwa
kuhudhuria akiwemo dairekta mkubwa Afrika, Godfather wa Afrika Kusini na
Top Ten ya Washiriki wa Shindano la Big Brother ‘Hot Shot’ 2014.
No comments:
Post a Comment