Monday, June 2, 2014

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA NA MWENYE NDOTO ZA KUWA MWIGIZAJI WA FILAMU GRACE RWEGASHA AANDIKA MAKALA NZITO SANA JUU YA MAAMUZI SAHIHI YA KUMPOKEA YESU KABLA HUJACHELEWA

Mwandishi Grace Rwegasha +255 788 443346  au +255 788443345 au +255 654407080

TUNAISHI KATIKA NYAKATI ZA MWISHO, NI WAKATI YESU ANALIANDAA KANISA. KURUDI KWA YESU KUMEKARIBIA.

Nimejaribu kumuuliza Mungu kwa njia ya maombi, kufunga na kuomba kumtafuta Mungu kutaka kujua ukweli wa kurudi kwa Yesu na nini kinaendelea katika karne hii, na nini tufanye ili tuwe tayari kwa kumlaki mawinguni. Pia kwa kusoma makala mbalimbali ambazo YESU mwenyewe amekuwa akiwatokea watu mbalimbali na kuwaelezea kuhusu kurudi kwake kumekaribia sana. Na akiwaelekeza watueleze nini tufanye na wapi tujirekebishe ili siku atakaporudi tuwe tayari kumlaki mawinguni.

Grace Rwegasha
Jambo la kusikitisha ni kwamba kanisa limelala, ni asilimia ......20%.......kati ya ...100%...... ya waumini ndio waliotayari kumlaki Yesu mawinguni na kuingia katika ufalme wa mbinguni.

Nikaumia sana moyo wangu kwani kwa hali ya kawaida inaonyesha kama kuna mwamko mkubwa sana wa injili, kwani Yesu anahubiriwa kila mahali, mikutano mingi sana inafanyika ya kumtangaza Yesu, na ukiangalia hata makanisa yamekuwa mengi kila mtu siku hizi anaanzisha kanisa, utakuta mtaa mmoja unamakanisa zaidi ya matatu na kuendelea, mpaka ninaona kweli tuko kwenye uamsho mkuu sana.


SWALI:- KWANINI YESU ANASEMA KANISA TUMELALA? NA NI ASILIMIA NDOGO SANA YA WATU WATAKAOINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI SIKU ATAKAPORUDI?

Jambo hili liliusumbua sana moyo wangu, kwa nini iwe asilimia ndogo? Tatizo liko wapi? Ndipo nilipoamua kutafuta habari za watu ambao Yesu amewatokea na kutaka kujua ukweli kama nitaelewa ukweli huo,na amewaambia nini kuhusu kurudi kwake na nini kifanyike katika kujiaandaa kusubiri kurudi kwake.

Ndungu msomaji hebu fuatana nami katika makala mbalimbali ambazo nimezipitia kwa kuzisoma. AMBAZO YESU MWENYEWE AMEWATOKEA WATU HAWA NA KUWAELEZA YATUPASAYO KUFANYA.

Ninaamini pia wapo watu wengi wanaopinga na kusema Yesu hawezi kumtokea mtu, au hawa wanaosema Yesu amewatokea wanasema uongo, wanatudanganya. Mimi ushauri wangu ni kwamba soma habari na uelewe, kuliko kupinga wakati hujasoma hujaelewa ukweli wa habari inavyoelezea. Chamsingi wewe angalia biblia yako inasemaje­ kuhusu jambo alilolielezea. Kwani hii ndio njia sahihi pekee ya kuweza kupambanua mambo katika ulimwengu waroho pamoja na maombi, na hii itakusaidia wewe kufanya maamuzi yaliyo sahihi kabla hujachelewa. Ndungu msomaji fuatana nami katika makala hizi chache sana ambazo nimezipitia kwa kuzisoma na kuelewa YESU anataka tufanye nini katika nyakati hizi za mwisho.

TUANZE NA DADA MMOJA JINA LAKE ANAITWA, ANGELICA ELIZABETH ZAMBRANO. AMBAYE YESU AMEMPELEKA MBINGUNI NA KUZIMU. HABARI ZAKE ZINAPATIKANA KATIKA WEBSITE www.spiritlessons.com

Dada huyu ametokewa na Yesu kwa miongo mitatu tofauti. Nitaanza kwa kunukuu katika habari YESU alipomtokea kwa kipindi cha kwanza. YESU alimuonyesha nini? NA ALIMWAMBIA NINI? NA ANATAKA TUFANYE NINI? Yesu alimpeleka sehemu ya mateso kuzimu kwenye moto. Unaposoma habari hizi ndugu mpendwa ujue ya kuwa huko kuzimu ni sehemu ya mangojeo tu, japo walioko huko wanateseka na kuungua moto na mateso mengi. Kwani biblia inasema siku ya mwisho kila mtu atasimama mbele ya kiti cha enzi na kutoa hesabu ya matendo yake. Na kama jina lako halikuonekana katika kitabu cha uzima, basi utatupwa katika ziwa liwakalo moto na kiberiti, na hii ndio mauti ya pili, hapo ndipo kutakuwa na kilio na kusanga meno. Kama walioko kuzimu wanalia kwa sasa, Je siku ile itakuwaje? Wapendwa tumuogope Mungu soma Ebrania 10:26. Kwahiyo ndugu msomaji kuna ziwa la moto. Atatupa shetani wa kwanza siku hiyo na wafuasi wake watafuata na ndio maana shetani hataki kuja kukaa peke yake katika lile ziwa la moto. Anafanya juhudi kubwa sana ili apate wafuasi. Kwa kukudanganya na kukuhubiria uongo, ili usikae hata siku moja ukaelewa na kuijua kweli. Kwani biblia inasema ukiijua kweli, kweli itakuweka huru.

NINANUKUU KAMA ILIVYOANDIKWA KATIKA TAFSIRI YAKE YA KISWAHILI.

MTU ALIYESHINDWA NA DHAMBI YA KUTOKUSAMEHE

Nilimuona mwanamke akiteswa, alikuwa na funza wakimla uso wake na mapepo ya kimchoma mikuki mwilini, naye hupiga kelele hapana! Bwana nihurumie! Nisamehe mimi! Tafadhali nitoe mahali hapa, (Luka 16:24) Bwana Yesu akamjibu , hakuna nafasi ya kutubu tena kwa walioko huku kuzimu, nafasi ipo tu kwa wale walioko duniani, ndio wanaoweza kuomba toba na kusamehewa. Yesu akamwambia Angelica “Huyu yupo hapa sehemu ya mateso kwa sababu alishindwa kusamehe’’ Kwasababu hawajawasamehe wengi na ndio maana wengi wapo hapa. Wameshindwa kusamehe. Nenda kawaambie wanadamu ni wakati wa kusamehe, kila mtu amsamehe ndugu yake, jirani yake, rafiki yake, waambie waache malaumu, mafundo, chuki mioyoni mwao, kwa kuwa ni mda wa kusamehe. KAMA KIFO KIKIMSHITUKIZA MTU ALIYESHINDWA KUSAMEHE. HUYO MTU ATAKWENDA KUZIMU kwenye mateso na moto. KWA KUWA HAKUNA AWEZAYE KUNUNUA MAISHA.

Wakapita eneo jingine la kuzimu, Yesu akamwambia binti angalia yule mwanaume unayemuona mahali pale.Yuko hapa akiteswa kwasababu hakutubu. Binti hakuna mwasherati, wala mwabudu sanamu, hakuna mchoyo na hakuna muongo atakayeingia katika ufalme wa Mungu Eph 5:5, mtu huyu alikuwa muhubiri enzi za uhai wake, aliwahubiria wengi habari zangu, lakini hakusema kweli, na aliijua kweli, alipenda fedha zaidi kuliko kuhubiri ukweli , hakutoa uhalisia wa kuzimu na mbinguni kwa washirika wake, sasa alipokufa yupo mahali hapa. Sehemu ya mateso. Angelica;- nilipomuangalia mtu huyu alikuwa na joka kubwa lenye sindano nyingi mwilini mwake limemzingira shingoni na asiweze kumtoa joka huyo, nikamwambia Yesu, Bwana msaidie mtu huyu! Yule mtu alipaza sauti yake kwa nguvu akilia, akisema Bwana Yesu nitoe mahali hapa Bwana, nataka nirudi duniani nikatubu! Bwana Yesu alimtazama na kumwambia ulijua vizuri yote haya , ulijua vizuri kabisa kuzimu ni halisi na kupo, sasa angalia umechelewa hakuna nafasi tena kwa ajili yako. Yesu akasema tazama binti nitakuonyesha maisha ya mtu huyu alipokuwa duniani. Yesu akanionyesha kioo kama television (luninga) Nikaona jinsi mtu huyu alivyoongoza misa kwa umati wa watu wengi na watu wale walivyokuwa wakiabudu sanamu. Yesu akasema wapo watu wengi sana hapa kuzimu walioishi maisha ya kuabudu sanamu enzi za uhai wao wakiwa duniani, sasa wako hapa katika eneo la mateso kwenye moto, Ibada ya sanamu haiwezi kuokoa mtu yeyote, NI MIMI YESU KRISTO PEEKEE ninayeweza kuokoa na nje yangu hakuna mwingine aokoaye. Nawapenda wenye dhambi, ila nachukia dhambi. Nenda na waambie wanadamu wote kuwa nawapenda na ninataka waje kwangu.

Tulipokuwa tunaondoka hapo, akaniambia, “Nataka nikuoneshe kitu kingine…. Wapo pia watoto huku.” Na nikamjibu, “watoto huku Bwana? Kwanini wawepo watoto huku? Neno lako lasema, 'Waacheni watoto wadogo waje kwangu na msiwazuie: kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wao." (Mathayo 19:14) Yesu akajibu, “Binti, ni kweli, ufalme wa mbinguni ni wao, lakini mtoto lazima aje kwangu, kwa kuwa kila ajaye kwangu sitamtupa kamwe." (Yohana 6:37) Ghafla, Bwana akanionesha mvulana wa miaka nane akiteswa kwenye moto. Mvulana akalia, “Bwana nihurumie mimi, nitoe mahali hapa sitaki kuwepo hapa, aliendelea kupiga kelele na kulia. Nikaona mapepo yamemzunguka mtoto huyu, yaliyofanana na cartoon. Kulikuwa na aina za Dragon, BoyZ, Ben 10, Pokémon, Doral, na nyingine nyingi. “Bwana, kwanini mtoto huyu yuko huku?" Yesu akanionesha picha ya mkanda wa maisha mtoto huyu. Nilimwona anavyotumia muda karibia wote kwenye LUNINGA (TV) akiangalia cartoon.

Grace Rwegasha

Cartoon ya Ben 10: Pokemon:
Yesu akasema, "Binti, hayo maigizo ya cartoon, sinema zake, michezo mbalimbali ya kuigiza inayooneshwa kila siku kwenye LUNINGA [TV] ni vyombo vya shetani atumiavyo kuwaharibu wanadamu….. tazama, binti ilivyotokea kwa mtoto huyu." Nilimwona jinsi mtoto huyu alivyokuwa mkaidi na asiye mtii kwa wazazi wake. Wazazi wake aliposema naye alikimbia na kutupatupa vitu ovyo na kuto watii. Baada ya hapo akagongwa na gari na ukawa mwisho wa maisha yake. Yesu akasema, “Tangu hapo yupo mahali hapa.”

Nilimtazama mtoto Yule akiteswa. Yesu akasema, "Binti, nenda na uwaambie wazazi wawaelekeze watoto wao kama ilivyo katika neno langu.”(Mithali 22:6) Neno la Mungu ni halisi.

Neno la Mungu linatuambia tumwonye mtoto kwa fimbo, lakini si kila wakati, pale tu mtoto anapoonyesha ukaidi kwa wazazi. (Mithali 22:15)

Bwana akaniambia kitu cha kuhuzunisha sana na kuumiza mno. Akasema, “Binti, wapo watoto wengi sana huku kwasababu ya cartoon, kwasababu ya ukaidi.” Nikamuuliza, “Bwana, kwanini lawama ziwe hizi cartoon?” Naye akanieleza, “Kwasababu ni mapepo yanayobeba ukaidi, kiburi, ukali na chuki kwa watoto, ili wasifanye vitu vizuri na mapepo mengine huwaingia watoto ili wasifanye mambo mazuri, bali wafanye mabaya vile waonavyo kwenye LUNINGA [TV] watoto hutaka kufanya hivyo hivyo.” Kuzimu ipo, kuzimu ni halisi, na watoto lazima waamue watakwenda na nani. Nikasema, “Bwana, niambia, kwanini kuna watoto huku?” na Yesu akanijibu,

Pia alinipeleka mbinguni na kuniambia “Binti, huyu ni Maria. Maria, aliyemzaa Yesu Kristo, ambaye ni mimi. Binti, nikwambie, yeye hana habari ya yanayotokea duniani. Nataka kukwambia, nenda kawaambie wanadamu, waambie waabudu sanamu kuwa kuzimu ni halisi, na waabuduo sanamu hawata urithi Ufalme wangu, lakini waambie kama wakitubu, wataweza kuingia makao ya mbinguni. Nenda waambie nawapenda na pia waambie Maria hajui chochote (kinachotendeka duniani) na pekee wanayeweza kuheshimu ni mimi, kwasababu si Maria wala mtakatifu Gregory wala mtakatifu yeyote awezaye kuokoa. Mimi ndiye niokoaye na nje yangu hakuna yeyote, hakuna yeyote, hakuna yeyote – aokoaye!” Alirudia mara tatu kuwa hakuna yeyote awezaye kuokoa isipokuwa yeye.

Wanadamu wamedanganywa na kuamini kuwa kwa kupitia wadhaniwao ni watakatifu, sivyo ilivyo, bali ni mapepo, yafanyayo kazi kupitia sanamu zilizofanywa kwa mikono ya watu. Lakini ngoja nikueleze kwamba Bwana anataka kukupa kilicho bora. Anataka wewe uingie katika Ufalme wa Mbinguni; tubu na kuacha uabudu sanamu. Kwasababu ibada ya sanamu haitakuokoa wewe. Yesu Kristo wa Nazareti ndiye pekee aokoaye, aliyeutoa uhai wake kwaajili yako, yangu na kwaajili ya wanadamu wote. Bwana ana ujumbe mzito kwa wanadamu. Huku akilia aliniambia,Tafadhari, Binti, usikae kimya; nenda na uwaambie ukweli, nenda na uwaambie nilichokuonesha wewe.”

www Derine Reveletions.

Aliponichukua kwa mara ya pili Yesu alimuambia nenda kawaambie watu wangu, kurudi kwangu kumekaribia, ni watakatifu tu ndio watakao niona.

SOMA ZAIDI KWA KUBONYEZA "READ MORE" HAPO CHINI.


TULIELEKEA TENA ENEO LA KUZIMU

Haikuwa rahisi kwangu, nilimwambia Bwana siwezi nitoe hapa; niliwasikia mamilioni wa watu wakiwa huko kuzimu wakilia kilio kikuu, wakisema Oooh Bwana tusamehe, tusaidie, tutoe mahali hapa tupe nafasi nyingine tukatubu duniani.

AMEPOTEA MILELE KWA DHAMBI YA KUTOTOA FUNGU LA KUMI NA SADAKA

Katika watu wengi waliotoa sauti za kilio, nilisikia sauti ya mtu mmoja ikisema Bwana nakuomba, nisamehe kwa wizi nilioufanyka, nilikuibia wewe Bwana sitaki kukuibia tena, nitoe mahali hapa. Yesu akasema binti yangu nitakukonyesha ni nani mtu huyo.watu wote walioko kuzimu wana alama ya 666 katika vipaji vya uso wao.

Mtu huyo alinyoosha mkono wake akisema Bwana nisamehe Angelica;-“nikamuuliza kwa nini uko hapa? Unasema umemwibia Mungu, lakini hakuna mtu anayeweza kumuibia Mungu, hii haiwezekani, kwa nini unasema Umemuibia Mungu? Akajibu nitakuambia historia yangu:- Mimi nilikuwa kiongozi Kanisani wa Kikristo kwa muda wa miaka 20 nilimjua Yesu kristo lakini kwa miaka yote hii 20 nilisema pesa zangu zote za fungu la kumi; na sadaka zinakwenda tu kumsaidia mchungaji na familia yake, hivyo sikutoa fungu la kumi na sadaka sasa ninajuta kwani nimeelewa kuwa hazikuwa kwa ajili ya mchungaji zilikuwa ni kwa ajili ya Bwana, ili injili kazi ya Mungu iende mbele; na ndio maana ninasema nimemuibia Mungu. Na kwa wakati huu tunapoongea ninaamini wapo watu wengi sana duniani sasa hivi ambao wanamuibia Mungu kama mimi utakapo rudi duniani, waambie watu wote wale ambao hawataki kutoa fungu la kumi na sadaka, wasimuibie Mungu. Hivyo wataishia huku kuzimu, na hakuna wezi watakaoingia katikan ufalme wa Mungu, sasa nimejua neno la Mungu takatifu ninajuta, nimetambua kumbe nilimuibia Mungu . Malaki 3:8 waambie watu watu, wanapomtolea Mungu wamtolee kwa moyo wa furaha na upendo. 2cor.9:7 aliendelea kulia, Bwana nisamehe, nisamehe Yesu alimjibu umechelewa hakuna tena nafasi ya kutubu kwako.

Nikamuuliza tena yule mtu kwaninui lakini ulimuibia Mungu? Hukujua utatupwa motoni? Kweli nilijua, ila sikufuata. Kwani mimi nilikuwa ni mtu wa kujivuna na kujisikia sana Malaki 3:8 -10.

BINTI MIAKA 15 KUZIMU KWENYE MOTO

Yesu alinichukua na kuniambia nataka nikuonyeshe zaidi, tulipo kuwa tukiondoka eneo hilo nikasikia sauti ya binti akilia kwa sauti kuu, kilio cha uchungu akisema, nisaidie! nisaidie! Nikamuuliza wewe nani? Na kwa nini uko hapa? Yule binti akajibu mimi nilikuwa binti wa miaka 15 nilipokufa na kufikia eneo hili. Nakuuliza lakini kwa nini uko hapa? Akajibu akisema “ nilifikiri nilikuwa na muda mrefu wa kuishi, kwa sababu nilikuwa mdogo. Watu mara nyingi walinihubiria habari za Yesu na wokovu wake, lakini siku zote nilisema hawa wainjilisti wamechanganyikiwa, niliwacheka na kuwadharau. Sasa nimeona ya kuwa nilifanya kosa kubwa sana maishani mwangu, niangalie niko hapa ninaungua kwenye moto. Nilikufa kwa ajali ya gari, sasa ninajuta, ninajuta sana kutafuta njia jinsi ya kutoa huku na ninapoipata sewezi kutoka kwani mapepo wananitesa nikiwa hapa huja na kusema huwezi kutoka hapa, utakaa hapa maisha yako yote jamani! Nisaidieni, nisaidie! Nitoke sehemu hii ya mateso, Yesu akasema hakuna tena nafasi ya kutubu kwa wote walioko hapa, ila tu wale walioko duniani ndio wanaweza kutubu.

Grace Rwegasha

Yule binti aliendelea kusema nenda kawaambie watu wote walioko diniani na jamaa zangu wasije huku, nenda kawaambie vijana wenzangu wako duniani wanayo nafasi ya kumtafuta Yesu na kumpokea waambie waache dhambi, nilipokuwa Duniani niliishi maisha tofauti sana maisha yaliojaa dhambi za starehe mbalimbali, sikuwatii wazazi wangu,namuomba Yesu anisamehe anitoe mahali hapa, wasije huku tafadhali waambie wawatii wazazi wao, waambie wampokee Kristo ndiye awezae kuokoa. Anaokoa shetani alinidanganya na ninajua siwezi kutoka katika eneo hili ninajuta sana.

Alilia sana, alinyoosha mikono yake akimuekekea Bwana Yesu amuokoe, amtoe mahali pale kwenye moto.

Yesu akaniambia binti nenda duniani kwaambie wanadamu kuzimu ipo, kwa sababu wako wengi ambao hawaamini wanasema kuzimu hakupo. Binti yangu rudi duniani kawaambie watu wangu umefika wakati wa kuniabudu katika roho na kweli Yohana 4: 24 waambie watu waishi maisha matakatifu. Wasome neon langu na kulifuata. Pia kuna watoto wangu tena wale waliochaguliwa watadanganyika, wambie wasome nen langu takatifu ili shetani asiwadanganye na watafute uwepo wangu katika roho na kweli.

TUANGALIE YESU ALIPOMCHUKUA ANGELCA E . ZAMBRANO KWA MARA YA TATU YESU ALIMUAGIZA NINI KWA AJILI YETU.
  • Kupitia malaika Bwana alinionyesha asilimia 80% ya wakristo ya makanisa ya Kikristo wataachwa, na wataachwa kwa sababu wako baridi, na hii ni kwa sababu hawatafuti uwepo wa Mungu katikati yao, kwa sababu ya dhambi zao zinazowazunguka, pia kwa sababu wamevunjika moyo na kukata tama ni asilimia ishirini tu 20%.

Watakao nyakuliwa siku Yesu akirudi, wengi watabaki Mathayo 22:14 Yesu akanichukua na kunipeleka kuzimu tena.

MCHUNGAJI ALIYETENDA DHAMBI YA UBAGUZI / NA UPENDELEO KWA WATU.

Tulipo ingia eneo hilo, nikasikia sauti ya mtu akilia, baba , baba nitoe mahali hapa siwezi kuvumilia tenamateso haya.

Angalica:- nikamuuliza Yesu, Bwana huyu ni nani? Lazima alikuja kabla akiwa duniani, kwa sababu umesema utanionyesha watu ambao mwanzo walikutumikia kisha wakarudi nyuma; sielewi kwa nini anakuita baba na wakati yuko huku kuzimu? Yesu akajibu alikuwa ni mchungaji alipokuwa Duniani, mtu huyu hapo kuzimu alikuwa akihubiri na kusema tubuni, tubuni, tubuni kanisa la kristo , lazima mtubu.

Angelica- nikamuuliza Yesu kwa nini mtu huyu anaendelea kuhubiri akiwa huku kuzimu? Yesu akajibu mambo watu waliyoyafanya wakiwa duniani wakija huku kuzimu huendelea vilevile Galatia 6:7 – 8; Nikaanza kulia na kusema kama alikuwa mchungaji kwa nini yuko hapa?

Yesu akamjibu ni kwa sababu hii ndio maana yuko huku Yesu akanifunulia maisha yake, alipokuwa duniani, Duniani alikuwa mhubiri na alikuwa ni mtu wa kusujudu wanadamu wenye pesa, kumwangalia mwanadamu kama tegemeo lake kuliko Mungu .

Alikuwa mtu mbaguzi/upendeleo alibagua watu kutokana na nyadhifa zao, akiwa katika eneo langu takatifu (Kanisa) kuwa mtu wa ubaguzi/ upendo madhabahuni kwa hali ya ubaguzi akionyesha kuwajali wale watu wenye pesa / matajiri kanisani, akiwajali wale watu wa hali ya juu kifedha, kinyadhifa

Watu hao wana pesa lakini ni watu ambao hawaliogopi neno langu katika maisha yao.

Alionyesha kuwajali / kuwapendelea hao watu ambao hawana Mungu ndani yao ila wana pesa tu. Angelica – nikalia nikasema bwaba, bwana sikujua kama kuwa mtu wa upendeleo, ni dhambi: Yesu akajibu, ndiyo binti, watu wengi walipenda kunitumikia na kuwa sehemu ya kanisa kwa utumishi, lakini mchungaji huyu hakuruhusu watu hao wahudumu pamoja nae katika kanisa lake, kwani alikuwa mtu wa ubaguzi / na upendeleo. Mchungaji huyu hakutubu kwa dhambi yake ya ubaguzi / upendeleo na kujiona, kujisikia. Yesu akasema na kwa dhambi hii watu wengi hawawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu/ hawawezi kuja kwangu. Nahii ndio maana mchungaji huyu yuko huku kuzimu muangalie hata huku kuzimu anahubiri injili kwa ubaguzi / upendeleo. Galatia 6:7-8

Mchungaji huyu alimuangalia Yesu na kusema baba, nimechoka kuwa katika eneo hili siwezi tena, naomba nitoe, sitafanya dhambi tena, nipe nafasi.

Yesu:- akajibu umechelewa. Mpaka sasa kuna makanisa mengi duniani yanayoongozwa na roho hii ya upendeleo na ubaguzi japo kuwa inaonekana kama ni kitu kidogo au cha kawaida ndani ya kanisa, lakini ukweli ni kwamba ni dhambi kubwa sana mbele za Mungu, na ni dhambi itakayompeleka mtu jehanamu.

na kwa dhambi hii ya mchungaji huyu, watu wengi walijikwaa, hawakumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao na hata wale waliokuwa wamempokea Yesu walirudi nyuma kwa sababu yake, hivyo roho nyingi zimeingia kuzimu kwa ajili yake.Yakobo 2:8 -11

Neno la Mungu linasema katika kitabu cha Yakobo kuanzia mstari wa 9 – bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi, na kuhukumiwa na sheria kuwa mkosaji, mstari (10) maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja amekosa juu ya yote, mstari (13) maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma kwake yeye asiyeona huruma hujitukuza juu ya hukumu.

YESU – AKANIBIA ANGELICA NITAKUONYESHA DHAMBI NYINGINE INAYOENDELEA MADHABAHUNI KATIKA MAKANISA MENGI DUNIANI, Yesu akanionyesha watu wakiimba na kucheza muziki aina ya rock, rap, reggae katika madhabahu kanisani, miziki ya aina hii hainipendezi hata kidogo, ninataka watu waimbe na kuabudu mimi katia roho na kweli; hakusema anataka watu wa”rap” katika roho na kweli? Ila wamwabudu na kuimba katika roho na kweli. Tukaendelea kutembea katika maeneo mbalimbali ya kuzimu, nikamuona kijana mmoja aliyekuwa mkristo duniani ambaye alikuwa akiimba nyimbo kwa mtindo warock, rap, reggae madhabahuni kanisani nikamuuliza Bwana, kwa nini huyu kijana hupo hapa? Na kwa nini anaimba kuhu kuzimu? Nikamuuliza Yesu akanijibu ndio binti mtu huyu aliimba akiwa kanisani, Yesu hakuendelea kuongea nami tena, ndipo nilipoendelea kumuuliza maswali mtu huyu yule mtu akasema mimi naitwa Mark niko takika eneo hili kwa sababu sikumwabudu Mungu na kumuimbia katika roho na kwel, na badala yake niliimba nyimbo aina ya rap, madhabahuni na niliimba nyimbo hizi na sikupenda kuomba, sikuwa mtu wa maombi katika maisha yangu, sikupenda kutafuta uwepo wa Mungu katika huduma yangu ya uimbaji. Nia yangu ilikuwa kuwavutia vijana aje kanisani, nilitaka kanisa langu liwe na watu wengi, waje kanisani kwa kuwavutia na nyimbo zangu za rap.
Grace Rwegasha

Sikujua kuwa ni Mungu ndie anayaleta watu kanisani; Ni Mungu pekee ndiye anayeshughulika na mioyo ya watu.

Angelica, Nikamuuliza ni kwa mda gani umekuwepo hapa kuzimu? Ni miaka minne sasa imepita pia nilikuwa mtu wa majivuno na kujisikia na hii pia ni sababu ya mimi kuwepo hapa .

Hapa mapepo yananitesa sana na kunicheka ya kisema;- miziki ya kidunia ni silaha kubwa sana kwetu, kuwaleta vijana katika eneo hili la kuzimu.

Ghafla joka kubwa likatokea na kumzunguka mwili wake wote, alilia kwa kilio kikuu nisaidie nitoe hapa ninajua siwezi kutoka hapa tena. Niangalie nipo kwenye hali ya mateso makubwa, nilipokufa nilianza kuona nikidumbukia kwenye shimo lililoonekana kuto kuwa na mwisho, niliserereka katika shimo hilo kwa kushuka chini; nilipotua chini nikajikuta niko hapa kuzimu sehemu ya mateso makuu, funza na minyoo inapita na kutoboa mwili wangu wote, niko hapa eneo la mateso toka siku ile, mwiliwangu hauna umbo maalum tena, hii ni kutokana jinsi ninavyoteswa huku, moto wa hukumu unanichoma siku zote. Siwezi vumilia tena nitoeni; mapepo yananicheka na kusema huu ndio ufalme wako na shetani ndiye Mungu wako.

Angelica:- akasema ndio nimeona lakini duniani ulikuwa na nafasi ya kutubu, kwa nini huku hatutubu? Mark akalia kwa uchungu akaniambia ukirudi duniani kawaambie vijana wote wamwabudu Mungu katika roho na kweli, kumwabudu Yesu katika roho na kweli Mungu anatafuta watu wamwabudu katika roho na kweli. Tulipomaliza hayo moto alimfunika na sikumuona tena nikaondoka eneo hilo.

YESU AKASEMA WAAMBIE WATU WANGU WAMWABUDU KATIKA ROHO NA KWELI.

MKE WA MCHUNGAJI KUZIMU

Tulipoendelea kwenye eneo jingine la kuzimu nikamuona mwanamke huyu kuzimu akisema siwezi kuvumilia tena, Bwana Yesu nitoe nisaidie, mwanamke huyu alimtumikia Mungu kwa miaka mingi, alipokuwa duniani. Baada ya maisha haya kupita, hupewi ajira kwa ni miaka mingapi umemtumikia Mungu (Ezekiel 18;21 – 32 ) tunapewa / tunahesabiwa kuwa na thawabu mbele za Mungu kama tumemtumikia Mungu katika roho na kweli na kwa moyo wote (Mathayo 7, 21 – 23)

Mwanamke huyu alimjua Mungu, na alilijua neno la Mungu, hata kuwa mhubiri, kuhubiri injili ya Kristo. Lakini yuko hapa kuzimu kwa dhambi ya unzinzi (Galatia 5,19 – 21) (Efeso 5, 3 – 5) Mwanamke huyu kule kuzimu aliteswa na joka, sawasawa na makahaba wote wanavyoteswa huko kuzimu, mwanamke huyu aliyaambia mapepo na majoka, mimi ni mke wa mchungaji, msiniguse! msinifanyie hivi! Hata hivyo mapepo hayazuiliki yalimtesa tu.

Yesu akasema yupo hapa kwa dhambi ya uzinzi, duniani alikuwa mke wa mchungaji aliyehubiri habari njema za Yesu Kristo, pia alibarikiwa na baraka ya watoto, lakini hivi vyote havikumfanya atosheke na mume wake. Mpaka anamua kutoka nje ya ndoa yake na kufanya uasherati. Yesu akaendelea kusema, unajua dhambi hii ni dhambi inayoendelea katia makanisa mengi sana duniani, hata walio wahubiri wakubwa sana duniani, utakuta wako katika dhambi hii, nenda kwaambie waache, la sivyo wataishia kuzimu Galatia 5, 19 – 21

KIJANA LIYEKUWA MWINJILIST MOTONI

Pembeni ya mke wa mchungaji kulikuwa na kijana aliyesema kwa kilio nisaidie Yesu, nisaidie yesu, nitoe hapa alikuwa mwinjilisti duniani, alifanya dhambi ya unzinzi mara kwa mara na huku anaendelea, kama mtu huwezi kujizuia ni bora uoe au uolewe kuliko kuwa na tama 1 Coritho 7. Ni bora kuoa, ili uepuke kutenda dhambi kwa sababu ukiishi maisha ya dhambi, halafu ukafa utaishia kuzimu, mtu huyu alihubiri neno la Mungu, (hii inatufundisha tuombe ili tuwe kushinda hila za shetani, tuwe waombaji) kwani shetani anatafuta mbinu ili awanase watumishi wa Mungu kuna mamilioni ya mapepo waliojipanga kuwaunganisha watumishi wa Mungu, ni muhimu pia kwa washirika kuwaombea wachungaji wao, kuombea walioko nchini kwako na waliko duniani kote. Nilazima tulitii neno la Mungu 1 Yohana 23 – 5

MCHUNGAJI AKITESWA MOTONI

Eneo jingine nikamuona Mchungaji akiteswa alikuwa ameshikilia mkononi mwake kitu kama mfano akinywa pombe alionyesha tendo la kunywa pombe. Nikawaza mchungaji mlevi motoni alikuwa ni mchungaji wa kanisa kubwa sana duniani na washirika wengi sana, Pia alikuwa ni muongo na mzizi, pembeni ya mchungaji huyu kulikuwa na mapepo yaliyokuwa na umbo kama mwanamke na aliendelea kuonekana mlevi katika eneo hilo kuzimu na kuzini na mapepo yalimzunguka mwanaume huyu akasema, nilikuwa mchungaji duniani lakini sikuishi /wala kufuata/ kutii kama neno la Mungu linavyo sema. Nilienda kulewa pombe, pia nilimdanganya mke wangu, siku tubu kwa dhambi zangu, mtu huyu alijua kabisa walevi na wazinzi hawawezi kuingia katia ufalme wa Mungu, lakini aliendelea katika njia zake za dhambi – (Gal, 19 -21, Ufunuo, 21: 8)

Inaumiza sana kumuona mchungaji amemtumikia Mungu, halafu anaishi motoni. Yesu akaendelea nitakuonyesha jambo jingine linaloendelea katika kanisa la leo.

WALIOKATAA WITO WA MUNGU / NA UTUMISHI HAUKUTIMIA KATIKA MAISHA YAO
(“A CALLING REJECTED, A DESTINY DIVERTED”)

Tuliendelea katika eneo jingine la kuzimu nilimuona kulikuwa na mwanamke mmoja Yesu akaanza kuniambia habari zake mwanamke huyu nilimuita anitumikie alipokuwa na umri wa miaka 15, kwa wakati ule nilipokuwa nikimtembelea na kumwambia umefika wakati unatakiwa unitumikie aliniambia “ mimi sijawa tayari kwa utumishi kwanza bado niko mdogo. Niruhusu kwanza bwana nisome kwanza nimalize digrii, nk. Yesu akasema basi nikamuacha amalize masomo yake nikamrudia tena, nitumikie sasa, akajibu nimeolewa na lazima nijali familia yangu na watoto wangu, siwezi kukutumikia kwa sasa. Watoto wake walipokuwa wakubwa na kuoa na kuolewa na kupata wajukuu. Nikamwambia nitumikie sasa akanijibu “ninalea wajukuu wangu, bado sina nafasi wala mda wa kukutumikia. Yesu akasema nilieendelea kumuita anitumikie kwa kipindi chote cha maisha yake, lakini hakutii wala hakuitii sauti yangu na akafa bila kufanya wito wake alioitiwa anitumikie. Na akaishia kuzimu kwa dhambi ya kutokutii. Karibu watu elfu tano (5,000) wamepotea dhambini kwasababu ya kutokutii kwake, mapepo yaliyomzunguka kuzimu humwambia kwamba tazama watu hawa wote waliokuzunguka wako hapa kuzimu kwa sababu ya kutokutii kwako. Mama huyu alimuangalia Yesu na kulia kwa kuomba naomba unisamehe sikutii sauti yako na kutokukusikiliza.

ANGELICA:- Je ni watu wangapi wako katika hali hii ya kutokutii sauti ya Mungu wanapoitwa wamtumikie? Wakati Yesu anapokuchagua umtumikie ni lazima utii sauti yake. Angalia mwanamke huyu , huku kuzimu analia kwa dhambi ya kutokutii sauti ya Mungu na aliendelea kuomba Yesu msamaha lakini Yesu alimjibu hakuna tena nafasi kwa ajili yako ya kutubu. LUKA 12:4-5.

DHAMBI YA KUJIUA MWENYEWE ( SELF MUDDER )

Yesu akasema inaniumiza kuona upendo wa watu wengi duniani umepoa. Majaribu na matatizo na vikwazo vinatokea duniani. Nitakuonyesha mtu mmoja mwanzo aliokoka na kuwa mtumishi wangu. Tulipofika eneo hilo tukamkuta mtu huyu akisema kwa sauti, Bwana Yesu unajua jinsi ninavyokupenda, mara nyingi nilitaka kufanya mapenzi yako, lakini nilikuwa ni mtu wa nia/njia mbili. Nilikuwa mwaminifu na mtakatifu kutembea katika njia zako na kuwa pamoja na wewe nilipokuwa nikihubiri neno lako wewe uliniongoza, wakati huo nilikuwa mtiifu kwako. Na baada ya mda nitaacha njia zako na kurudi katika njia zangu za zamani katika dhambi. Tena nikiamua kukurudia wewe, kweli unanipokea na unaendelea kunitumia kama kawaida, katika maisha yangu sikuwa mtu niliyesimama kikamilifu mbele zako, nilikuwa mtu wa kuanguka anguka tu mbele zako na kutubu mara kwa mara , na ndio nikaamua kujiua. Mtu huyu yuko kuzimu kwa dhambi ya kujiua mwenyewe. Imeandikwa wauaji hawataingia katika ufalme wa Mungu

GALATIA 5:19-21, UFUNUO 21:8. Hakuwa katika uwepo wa Mungu na ndio maana shetani alimuingia na kumpa mawazo ya kujiua na akaamua kujiua. Napenda ujue kwamba kama wewe ni miongoni mwa watu hawa , wanaochoka kumtumikia Mungu, na kurudi nyuma mara kwa mara, unajiona huwezi kuendelea mbele na huduma uliyoitiwa, umevunjika moyo, umechoka kumtumikia Mungu, labda pia ni kwa sababu mambo ya kidunia na ulimwengu huu yanakuvutia. Kataa tama za mwili, zikatae kabisa, tembea katika roho mtakatifu na Mungu atakusaidia ukae ndani yake na ufanye mapenzi yake. Na hili si jukumu la mchungaji wako, ni jukumu lako mwenyewe, na si la mshirikika yeyote aliye karibu na wewe. Kubali kuongozwa na Mungu, kuongozwa na roho mtakatifu na Yesu Kristo. GALATIA 5: 16-21, Basi enendeni kwa roho wala hamtazitimiza kamwe tama za mwili, kwa sababu mwili hutamani kishindana na roho na roho kushindana na mwili.

HATARI YA KUGOMBANA, MGAWANYIKO , CHUKI , KATIKA KANISA LA LEO.

Tulipotembelea eneo linguine la kuzimu, niliona wanaume wawili wakigombana kuzimu, kwa mara ya kwanza kuona ugomvi watu wakigombana kuzimu. Hii ni mara ya tatu mimi kupelekwa kuzimu na Yesu lakini sikukaa kuona watu wakigombana kuzimu. Watu wazuri kanisani katika utumishi lakini moyoni mwao wako pale kuhakikisha wanagombania washirika, wanagombana wao kwa wao, na kuendelea kuishi katika hali ya vita . Jamani napenda niwaambie roho hizi mnazogombania ni mali ya Kristo, na pesa ni kwa ajili ya kazi ya Mungu. Wanaume hawa walipigana kwa hasira kali sana na mwanaume mwingine akaingilia wakaendelea kupigana vilivyo, mapepo yaliwatesa mateso makuu sana wakati wakiendelea kupigana, moto uliwachoma na walikuwa katika mateso makuu sana.

ANGELICA:-Nikamuuliza Yesu kwanini wanagombana? Yesu hakujibu , nikawageukia hawa waliokuwa wakigombana kuzimu nikawaauliza ninyi kwanini mnagombana kuzimu? Mko kwenye mateso na mnaendelea kugombana niambieni kwanini mko hapa? Mmoja wao akaniangalia na kusema tunagombana kwasababu hatuewezi kuepuka eneo hili, tupo hapa wote watatu kama tulivyokuwa duniani. Duniani tuligombana ili tupate faida, tuligombana ili tupate washirika wengi, tuligombana ili kila mtu apate vingi kuliko mwenzake. Sasa nitatubu Mungu anisamehe, ila ninajua siwezi samehewa tena. Yesu akaniambia ukirudi duniani waambie watoto wangu hapo mwanzo walikuwa katika njia zangu lakini wamegeuka wanagombana kupata washirika wengi, pesa nyingi , mali na utajiri. Waambie watubu wasije fika eneo hili. EBRANIA 12:14-15

SWALI LA KUJIULIZA LEO: JE, UMEMPA YESU MAISHA YAKO? JE, JINA LAKO LIMEANDIKWA KATIKA KITABU CHA UZIMA?

HEBU MWAMBIE YESU MANENO HAYA LEO:- NINATUBU DHAMBI ZANGU LEO NINAKUPOKEA WEWE YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINAAMINI ULIKUFA MSALABANI KWA AJILI YA DHAMBI ZANGU, NIOSHE KWA DAMU YAKO TAKATIFU, UNISAMEHE DHAMBI ZANGU, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU NA ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA. NIFANYE NIWE MTOTO WAKO HALISI AMEN.

FUATANA NAMI KATIKA MAKALA IFUATAYO YA VIJANA SABA WA COLOMBIA, WALIOTOKEWA NA YESU MWENYEWE, AKAWAONYESHA MBINGUNI NA KUZIMU. JE? YESU ALIWAONYESHA NINI KWA AJILI YETU.

Mungu alitupa ufunuo ambao ungebadili maisha yetu yote. Ni mara tuu tulikuwa tumeanza kufahamu juu ya Mungu na juu ya neno lake.Sisi ni vijana saba ambao Mungu ametupa upendeleo na jukumu kubwa la kuushirikisha ulimwengu ushuhuda huu.

Kila kitu kilianza majira kama ya saa nne asubuhi 4.00 Tulikuwa tunaomba na tulikuwa tuna jiandaa kwenda pikiniki baadaye siku ile. Ghafla majira ya saa nne (4.00) asubuhi nguvu kuu ya mwanga mweupe uliangaza kupitia dirisha mojawapo. Wakati mwanga ulipotokea, sisi sote kwa haraka tulianza kuongea kwa lugha mpya na tulibatizwa na Roho Mtakatifu . Kwenye muda ule, sisi sote tulishangazwa na kuogopeshwa na kile tulicho kiona. Mwanga ule wa utukufu ulikuwa ukiimulika chumba chote. Mwanga huu ulikuwa na nguvu kuliko mwanga wa jua.

Katikakati ya ule mwanga, tuliwaona Malaika wengi wakiwa wamevaa mavazi meupe. Malaika hawa walikuwa ni wazuri sana, warefu, na wenye mvuto wa sura.

Kari kati ya Malaika wale tuliona kitu cha kutushangaza umbo la mwanadamu. Umbo hili lilikuw ni la kiumbe maalumu sana, mtu aliye kuwa amevaa nguo nyeupe sana nywele zake ni kama nyuzi za dhahabu. Hatukuweza kuuona uso wake kwa sababu ulikuwa unang’aa sana. Hata hivyo tuliweza kuuona mshipi wa dhahabu ukiwa matiti mwake, na maandishi ya dhahabu yaliyosema: "Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana ." Alikuwa amevaa viatu vya dhahabu halisi miguuni mwake, na uzuri wake haukuwa na mfano.Tulipo uona uwepo wa mtu huyu wote kwa pamoja tulisujudu kwa kupiga magoti.

Baadaye tulianza kuisikia sauti yake. Ilikuwa ni ya kipekee na ya ajabu sana, kila neno liliingia miyoyoni mwetu kama vile upanga ukatao kuwili; kama vile ilivyo andikwa katika neno la Mungu(Waebrania 4:12). Alizungumza nasi kwa wepesi lakini kwa maneno yenye nguvu sana. Tulisikia sauti yake ikisema nasi kuwa, "Watoto wangu wadogo, msiogope, mimi ni Yesu wa Nazarethi, na nimewatembelea kuwaonyesha mambo ya ajabu ili muweze kuyaonyesha na kuyaelezea kwenye, Miji, Mataifa, majiji, makanisa na kila mahali. Pale nitakapo waambia mwende, mtaenda, na pale nitakapo waambia msiende msiende."

Bibilia takatifu, neno la Mungu, linasema katika( Yoeli 2:28) "Hata itakuwa baada ya hayo ya kwamba nitamimina Roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu waume na wake watatabiri ,wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono." Huu ni wakati ambao Bwana anauandaa kwa kila mmoja.

Baadaye kitu kigeni kilitokea, mwamba ulitokea katikati ya kile chumba, na Bwana ambaye tulikuwa pamoja naye, alitufanya kuingia ndani ya ule mwamba.Mwamba ule ulikuwa na urefu wa karibu inchi saba hivi juu ya sakafu, na shimo kubwa lilitokea pale sakafuni.Lilikuwa ni kubwa, jeusi, uwazi wa kutisha. Kwa haraka tuliweza kuwa juu ya ule mwamba na kuzama chini kupitia ule uwazi sakafuni. Ilikuwa ni giza nailituongoza hadi katikati ya dunia.

Wakati tulipo kuwa ndani ya giza lile baya, tuliogopa sana!tulitishika sana kiasi kwamba tulimwambia Bwana, "Bwana hatutaki kwenda eneo lile! Usitupeleke eneo lile Bwana! Tutoe mbali na eneo hili Bwana!" Bwana alitujibu kwa sauti nzuri na ya huruma, "Uzoefu huu ni wa muhimu sana ili muweze kuuona na kuwaelezea wengine."

Tulipo anza kutembea kwenye ukingo wa eneo hili, roho zilikuwa zikinyoosha mikono yao kwetu na kutaka rehema.Walimwomba Yesu kuwaondoa ndani ya eneo lile, lakini Bwana hata hakuwaangalia.

Baadaye tulianza kwenda katika maeneo tofauti tofauti. Tulifika katika eneo lenye kutisha zaidi kuzimu, mahali ambapo mateso makubwa sana hufanyika, katikati ya kuzimu. Eneo lenye mchanganyiko mkubwa sana wa mateso, mateso ambayo mwanadamu yeyote hawezi kamwe kuyaelezea. Watu pekee hapa ni wale tuu ambao walimjua Yesu na neno la Mungu. Walikuwepo wachungaji, wainjilisti, wamisionari na aina zote za watu ambao waliwahi kumkubali Yesu na kuujua ukweli, lakini waliishi maisha ya pande mbili.

Walikuwepo pia wale waliorudi nyuma kiimanin, mateso yao yalikuwa ni makubwa mara elfu zaidi ya wengine. Roho zile zilikuwepo pale kwa sababu zilihubiri, zilifunga , ziliimba na kuinua mikono yao kanisani lakini mitaani na manyumbani walikuwepo katika uasherati, uzinzi, uongo, unyanganyi. Hatuwezi kumdanganya Mungu. Bibilia inasema kwake ambaye alipewa vingi, atadaiwa vingi. (Luka 12:48)

Walikuwa wakipiga makelele na kuomba rehema kwa Bwana, lakini neno la Bwana linassema katika kitabu cha Waebrania 10:26-27, "Maana kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; bali kuna kuitazamia hukumu kwenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao."

"Huwezi kucheza na Mungu wala na miale ya moto wa kuzimu!" Bwana alisema, "Wanawangu, mateso yote duniani kwa pamoja SII KITU, kulinganisha na mateso yale mtu hupata katika eneo hili la kuzimu." Kama ni hatari kiasi hicho kwa yule anayeteseka kidogo kuzimu, ni mbaya kiasi gani basi kwa yule aliyeko katikati ya kuzimu ? ambao waliwahi kulijua neno la Bwana na kwenda mbali nalo. Baadaye Bwana alituambia kuwa wale wanao weza kucheza na moto duniani sii hivyo kuzimu hawawezi kamwe.

Tuliendelea kutembea maeneo tofauti tofauti na Bwana alituonyesha watu wa aina mbali mbali. Tuliweza kuona kuwa watu wote pale walikuwa na aina kama sita za mateso. Kulikuwepo na roho zilizo teswa na mapepo kwa aina zote za adhabu. Aina nyingine ni ufahamu wao uliosema, "Kumbuka wakati walipo kuhubiria, kumbuka wakati ulipo sikia neno la Mungu, kumbuka walipo kuambia habari za kuzimu na ulicheka juu ya hilo. Ufahamu wao wenyewe uliwatesa; kama vile minyoo ile iliyopita juu ya miili yao, kama vile moto ule ulao ambao ni mkali mara elfu, elfu zaidi ya tunavyojua. Hii ni zawadi ambayo shetani anayo kwa wote wanao mtafuta na kumfuata.

Neno la Bwana linasema katika Ufunuo 21:8 "Bali waoga na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakao moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili."

Kati ya roho zile milioni na milioni, Bwana alituruhusu kumwangalia mtu mmoja ambaye mwili wake nusu ulikuwa umezama katika ziwa la moto. Bwana alituruhusu kuelewa na kuyafahamu mawazo yake. Jina la mtu huyu ni Marko. Tulishangaa na yale mtu huyu aliyojisemea mwenyewe katika mawazo yake.



Tulijifunza somo ndani yetu tulipo yasikia mawazo yake yafuatayo, "Ningetoa chochote kile kuwa katika nafasi yako sasa! Ningetoa kitu chochote ili kwende duniani kwa dakika moja tuu. Singejali kama ningekuwa na hali mbaya, mgonjwa sana, ninayechukiwa sana, au mtu masikini kuliko wote duniani, ningetoa chochote kuweza kwenda duniani! kwa dakika moja tuu duniani." Bwana Yesu alikuwa ameushika mkono wangu. Yesu aliyajibu mawazo ya Marko kwa kusema, "Marko, kwanini ungependa kurudi duniani hata kwa dakika moja?" Kwa kulia na kwa sauti ya mateso, alimwambia Yesu, "Bwana! nitatoa kitu chochote kuweza kurudi duniani tuu kwa ajili ya kutubu na kuokoka."

Bwana aliposikia kile ambacho Marko alisema, niliona damuikitoka katika majeraha ya Yesu na machozi yaliyajaza macho yake na alisema, "Marko, umechelewa sana! minyoo imewekwa iwe kitanda chako na minyoo itakufunika." (Isaya 14:11) Wakati Bwana alipo mwambia hivyo, alizama kwenye ziwa lile mojakwa moja. Ni kwa huzuni kuwa roho zile zote hazina tena tumaini. Ni sisi tuu tuliopo duniani ambao tunayo nafasi ya kutubu leo na kwenda Mbinguni.

Tulisogea karibu katika moto mkubwa mbele yetu, ulikuwa mkubwa na uliwaka kwa ukali. Niliendelea kwenda chini taratibu, nikiona miali ya moto mingi na kusikia sauti za mamilioni ya roho zilizo lia kwa sauti kwa pamoja.

Baadaye niliona meza ya mti ambayo haikufikiwa na moto. Kulikuwa na kitu kama chupa za bia juu yake. Zilionekana kama ni za kuburudisha lakini zilijaa moto ndani yake. Nilipo kuwa ninaangalia, mtu alitokea kwa ghafla. Mwili wake ni kama ulikuwa umekwisha na kile kilichokuwa kimebaki ni vazi lililojaa tope na moto. Alikuwa amepoteza macho yake, mdomo na kila unywele kule motoni. Aliweza kuniona bila hata macho yake. Nina kuambia huyu ni mtu anayewaza, anayetafakari na kuona kwa kweli, sii kwa mwili wako wa asili.

Mtu huyu aliunyosha mkono wake kwa Bwana na kuanza kulia, akisema,, "Bwana nirehemu! Bwana nirehemu! Nipo kwenye maumivu! Ninaunguzwa! Tafadhali nirehemu na unitoe mahali hapa!" Bwana alimwangalia kwa huruma na nilianza kusikia kama joto kwenye mkono wangu. Niliangalia na kuona kuwa ni damu, damu ya Yesu! Damu ya Bwana ilitoka mkononi mwake alipo kuwa akimwangalia mtu huyu akiteseka na kuzungukwa na moto .

Baadaye mtu huyu aligeuka na kuelekeza mawazo yake kwenye meza na kutembea kuelekea zile chupa. Alichukua chupa na alipo kuwa karibu ya kuinywa, moto na moshi ulitoka ndani ya ile chupa. Aligeuza kichwa chake tena na kulia kwa jinsi ambavyo sijawahi tena kusikia. Alilia kwa maumivu makuu sana na masononeko na alianza kunywa kile kilicho kuwepo ndani ya ile chupa. Lakini chupa ile ilijaa asidi\ tindikali na koo lake liliaribiwa karibu na kwisha. Ungeweza kuona tindikali ile ikipita mle tumboni na kumuumiza.

Namba ile 666 ilikuwa imechimbiwa juu ya upaji wa uso wake. Juu ya kifua chake kulikuwepo na sahani iliyo fanywa na malighafi isiyo julikana mabyo hata ule moto wala minyoo isingeweza kuiangamiza. Ilikuwa na maandishi juu yake lakini hatukuweza kuyaelewa Bwana kwa neeema yake kuu, alitupa tafsiri ya kile kilicho kuwa kimeandikwa. "Nipo hapa kwa sababu mimi ni mlevi." Alimwomba Bwana rehema, lakini neno la Mungu lipo wazi sana linaposema katika 1 Wakotintho 6:10 "Wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyanganyi, hawataurithi ufalme wa Mungu."

Mungu alinionyesha hali ya mtu huyu muda mfupi kabla hajafaa duniani, kama vile sinema. Ilikuwa ni kama TV kubwa ikinionyesha sekunde zake za mwisho kabla hajafa .Jina lake aliitwa Luis na alikuwepo baa akinywa pombe. Niliona meza ileile na chupa ileile pale baa. Kuizunguka meza ile walikuwepo marafiki zake. (Naweza kukuambia jambo hili sasa kuwa yupo RAFIKI MMOJA TUU WA KWELI, na jina lake ni YESU KRISTO.Yeye ni rafiki mwaminifu.) Luis alikuwa akinywa na marafiki zake walikuwa tayari wamelewa. Rafiki yake mkubwa alichukua chupa na kuipasua na kuanza kumpiga nayo Luis. Alipoona Luis amelala chini alikimbia, na Luis alitokwa na damu hadi kufa pale sakafuni. Jambo la huzuni sana ni kuwa alikufa bila Bwana Yesu.

Katikati ya mambo haya yote, kwa jinsi roho zile zote zilivyo kuwa zinalia, nilimuuliza Bwana, "Oh Bwana, tafadhali niambie je mtu huyu alijua habari zako? Alifahamu habari za wokovu wako?" Bwana kwa huzuni alijibu, "Ndiyo, Lupe, alijua habari zangu. Alinipokea kama Bwana wake, lakini hakunitumikia." Baadaye nilijisiki uwoga zaidi. Luis alilia kwa sauti na kupiga kelele"Bwana hii inaumiza!inaumiza! tafadhali nirehemu!" Aliunyoosha mkono wake tena kwa Bwana lakini Yesu aliuchukua mkono wangu na tulitembea kutoka eneo lile la moto. Moto ulio muunguza Luis ulikuwa na ukali zaidi, na alilia kwa sauti kuu zaidi, "Nirehemu! Nirehemu!" Alitokomea baadaye kwenye ule moto.

Kwa jinsi tulivyo endelea kutembea na Bwana, niliona eneo la miraba lililojaa minyoo. Kulizunguka kulikuwepo na chuma chenye moto mwekundu. Kwenye eneo lile la miraba kulikuwepo na ubao ulio angaza kila mahali.

Ubao uliandikwa,"Karibuni waongo na wasengenyaji." Mwisho wake kulikuwa na ziwa linalo tokota. Ilikuwa ni kama uji wa kikemikali unao tokota. Baadaye niliwaona watu walio uchi kabisa wakija chini eneo lile. Walipo kuwa wanateleza kuja ngozi zao zilikuwa zinabaki kwenye kile chombo.

Walipo angukia kwenye ziwa lile, ndimi zao zilitanuka hadi kupasuka na minyoo ilitokea badala ya ndimi zile. Mateso yao yalianza. Neno la Mungu linasema katika Zaburi 73:18-19 "Hakika wewe huwaweka kwenye utelezi, Huwaangusha mpaka palipo haribika. Namna gani ukiwa mara! wametokomea na kutoweshwa kwa utisho."

Baada ya kuona hili, tulichukuliwa tena , nje ya kuzimu. Nina taka kukuambia kuwa Mbingu na kuzimu ni za kweli kuzidi hata ulimwengu wetu huu tunao ujua. Ni hapa tuu unapo weza kuamua ni upande upi unao taka kwenda; kuutumia umilele na Yesu au kuunguzwa kuzimu. Bwana aliendelea kutuambia,"Pasipo utakatifu hakuna mtu atakaye niona mimi, pasipo utakatifu hakuna mtu atakaye niona mimi." (Waebrania

Tulipo endelea, tuliwaona maelfu ya watu kwenye mateso, Wakati roho inapo mwona Bwana, zilijitahidi kumfikia kwa mikono isiyo na ngozi. Nilimwona mwanamke aliye anza kupiga makelele alipo mwona Bwana Yesu. Alilia, "Bwana tafadhali nirehemu! nitoe mahali hapa!" Alikuwa akiteseka sana na aliunyoosha mkono wake kwa Bwana.Aliendelea kumwomba Bwana amtoe eneo lile hata kwa sekunde moja.

Alikuwa yu uchi kabisa na alifunikwa na tope. Nywele zake zilikuwa ni chafu na minyoo ilikuwa ikijongea mwilini mwake. Alijaribu kuiondoa kwa mikono yake lakini kila alipo mwondoa mmoja mingine ilijizisha zaidi. Minyoo ilikuwa na urefu karibu inchi 6-8. Neno la Bwana linasema katika Marko 9:44, "Ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki."

Ilikuwa ni ya kutisha sana kumwona mwanamke huyu na kusikia kilio chake kwa jinsi minyoo ile kwa hasira ilivyo kuwa inaila nyama za mama huyu. Kulikuwepo na bango la chuma lililo kifuani

mwake ambalo lisingeweza kuharibiwa na moto. Lilisomeka , "Nipo hapa kwa ajili ya Uzinzi." Kwa jinsi ile ile ya dhambi yake, mwanamke huyu alilazimishwa kufanya uzinzi kuzimu na nyoka wa kutisha mnene. Nyoka huyu alikuwa na miiba mikubwa kuuzunguka mwili wake, ni kama ya uerfu wa inchi 6-8 hivi. Nyoka humwingia mama huyu sehemu zake za siri na kusafiri hadi mwilini mwake hadi kwenye koromeo lake. Nyoka alipo mwingilia hivi, alianza kulia kwa makelele.

Alimwomba Bwana kwa nguvu sana amtoe eneo lile, "Bwana, nipo hapa kwa ajili ya uzinzi, nimekuwepo hapa kwa miaka 7, tangu UKIMWI ulipo niua. Nilikuwa na wapenzi sita(6), na nipo hapa kwa ajili ya uzinzi." Kule kuzimu alitakiwa kuirudia dhambi yake tena na tena. Hakuna kupumzika usiku na mchana, akiteseka kwa jinsi ile ile kila mara. Alijaribu kuunyoosha mkono wake kwa Bwana, lakini Bwana alimwambi, "Blanca, kwako tayari umechelewa. Minyoo itakuwa ni kitanda chako, na minyoo itakufunika." (Isaya 14:11) Wakati Bwana alipo sema maneno hayo, blanketi la moto lilimfunika, na siku mwona tena.

Bwana alituangalia na alisema: "Angalia huu ni mshahara wa wacheza mziki." Watakuwa wakiruka kama wanyama juu na chini sawa na mapigo ya miziki. Kama ni salsa inapigwa, walitakiwa kuruka kwa mapigo yale, kama aina nyingine ya mziki ikipigwa, walitakiwa kuruka sawa na mapigo yake. Hawawezi kamwe kuacha kuruka. Lakini mbaya zaidi, viatu vyao vina misumazi ya inchi 6 chini yake. Wakati wanaporuka inawangia miguuni mwao na hawatakuwa na nafasi ya kupumzika.Wakati mtu anapotaka kuacha, pepo lingekuja maramoja na kumchoma na mkuki, likiwalaani na kusema, "Msifuni yeye sasa! Huu ndio ufalme wenu sasa, msifuni Shetani! msifuni! huwezi kuacha, msifuni!ni lazima umsifu !lazima uruke! lazima ucheze!Uwezi kuacha hata kwa sekunde moja."

Ilikuwa hatari kuwa wengi wa watu wale walikuwa ni wakristo waliomjua Bwana, Lakini walikuwa kwenye madisko ya usiku walipo kufa. Labda unauliza, "Wapi Bibilia inasema kwamba ni vibaya kucheza?" Katika Yakobo 4:4, Neno la Bwana linasema:: " Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui na Mungu? basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia kuwa adui wa Mungu." Pia katika 1 Yohana 2:15-17, "Msiipende dunia, wala mambo yaliyopo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake, maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia .Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele." Kumbuka dunia itapita, vitu vyote hivi vitaharibika, lakini yule atendaye mapenzi ya Mungu atadumu mile.

Tulipo endelea kutembea tulimwona mwanamke ndani ya chumba kingine, alikuwa akinivingirisha kwenye lile tope. Nywele zake zilikuwa chafu na zenye tope. Ndani ya chumba kile alikuwepo nyoka mnene mkubwa. Alikuwa anamsogelea na kumzunguka mwili wake, na alianza kumwingilia mwilini mwake akianzia sehemu zake za siri. Alilazimishwa kufanya uzinzi na yule nyoka. Kwenye eneo hili, wanaume na wanawake waliokuwa wazinzi walilazimishwa kufanya uzinzia. Hata hivyo walilazimika kufanya hivyo na majoka yale yaliyofunikwa na vitu vikali mwili mzima kama chuma kikali cha inchi 6.

Nyoka aliuharibu kabisa mwili wa mwanamke yule kila mara alipo mwingilia. Alilia sana kwa Bwana na kumwomba kusimamisha hali ile. Hakutaka kuteseka tena. "Simamisha! Sitaki kufanya tena!tafadhali simamisha hii hali!" Alimwomba Bwana amhurumie kila wakati nyoka alipo mwingilia na kumuharibu mwili wake tena na tena.

Tulijitahidi kuyafunga masikio yetu tusisikie kilio chake, lakini bado tulimsikia. Tulijaribu kwa nguvu zaidi kufunga masikio yetu , lakini haikusaidia. Tulisema Bwana, "Tafadhali Bwana, hatutaki kuona na kusikia hivi tena! tafadhali!" Bwana alitujibu, "Ni muhimu muone haya, ili muwaeleze wengine. kwa sababu watu wangu wanaangamizwa, watu wangu wanaukataa wokovu halisi, njia ya kweli ya wokovu."

Tuliendelea kutembea na tuliona ziwa kubwa lenye watu maelfu na maelfu ndani yake katikati ya miotoa. Walitupungia wakiomba msaada, lakini kulikuwa na mapepo mengi yakiruka juu ya eneo lile. Mapepo haya yalikuwa yanatumia mikuki yenye vichwa kama S- kuwaumiza watu wale waliokuwa wakiunguzwa katika lile ziwa. Mapepo yaliwatania na kuwalaani yakisema, "Ninyi masikini mlio laaniwa! Sasa ni lazima kumwabudu Shetani! Msifuni, msifuni kama mlivyo fanya wakati mlipo kuwa duniani!" Kulikuwepo watu maelfu kwa maelfu. Tuliogopa sana, tulihisi kama tusingeushika mkono wa Bwana tungebaki katika eneo lile la kutisha. Tuliogopeshwa na vitu tulivyo kuwa tunavihisi.

Tuliendelea kutembea na Yesu. Kwa mbali tuliona kitu fulani kikidondoka kama maumbo fulani hivi. Tulipo sogea karibu, tuliona kuwa ni watu wapya waliokuwa wakiingia kuzimu muda ule. Watu ambao ndio tuu wangekufa duniani kabla hawajampokea Yesu miyoyoni mwao, walikuwa wakiingia kuzimu.

Tulimwona kijana mmoja, mapepo mengi yalimkimbilia na kuanza kuuharibu mwili wake. Mara mwili wake ulianza kujawa na minyoo. Alipiga kelele, "Hapana! Ni nini hii? Acha! Sitaki kuwa eneo hili! Simamisha hii! Hii lazima itakuwa ni ndoto!" Hakujua kuwa amekufa, na ya kuwa amekufa bila ya Yesu moyoni mwake. Mapepo yalikuwa yakimchezea na kuuharibu mwili wake. Baadaye namba 666 ilitokea kwenye upaji wa uso wake, na bango la chuma kifuani mwake. Japo hatu kuweza kuona sababu ya yeye kuja kuzimu lakini tulijua kuwa hataweza tena kutoka mle tena.

HEBU TUMUONE PIA MTU MWINGINE ALIYETOKEWA NA YESU, JE YESU ALIMWAMBIA NINI ? KWA AJILI YETU. ANAITWA MARY K. BAXTER. HABARI YAKE KAMILI WAWEZA IPATA KATIKA WEBSITE HII.... www.Devine Revelation.info/SWAHILI.

Katherine Baxter alichaguliwa na Mungu ili kuujulisha ulimwengu juu wa UHALISI wa Kuzimu. Yesu Kristo alimtokea Mary Baxter wakati wa usiku, siku 40 mfululizo na kumtembeza kuzimu na Mbinguni. Alitembea na Yesu na kuona mambo ya kutisha ya Kuzimu na alizungumza na watu wengi. Yesu alimwonyesha ni kitu gani

kinatokea roho zinapokufa na mambo gani yanatokea kwa wasioamini na watumishi wa Mungu ambao hawatii wito walioitiwa.

Yesu alimtokea na kumwambia mimi ni YESU KRISTO BWANA WAKO nataka kukupa ufunuo wa kuwaandaa watakatifu kwa ajili ya kurudi kwangu. Na kuwageuza wengi kwenye haki. NGUVU ZA GIZA NI HALISI, NA HUKUMU NI HALISI.

YESU ALIMTEMBEZA MARY BAXTER KUZIMU, FUATANA NAMI KATIKA HABARI YA KUSIKITISHA , KWELI INABIDI TUTUBU NA KUMPOKEA YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WETU KABLA HATUJA CHELEWA KWA GARAMA YOYOTE ILE BILA KUPOTEZA MUDA.

Nilisikia sauti ikitoka katikati ya shimo la kwanza. Niliona umbo kwa mfano wa mifupa (skeleton) ikilia, “Yesu, nihurumie!”

"O, Bwana!" Nilisema. Ilikuwa ni sauti ya mwanamke. Nilimwangalia na kutaka kumvuta kutoka kwenye shimo la moto. Hali yake iliniuma sana moyo.

Mifupa ya mwanamke iliyokuwa na na rangi ya zambarau na ukungu ndani ilikuwa inazungumza na Yesu. Nilimsilikiza kwa mshangao. Nyama iliyooza ilining’inia kwa vipande vipande kwenye mifupa yake, na ilipokuwa inaungua iliangukia chini ya shimo. Mahali ambapo awali palikuwa na macho palikuwa mashimo matupu. Hapakuwa na nywele.

Moto ulianza kwenye miguu yake kama moto mdogo na ukaendelea kukua ulipokuwa unapanda kwenye mwili. Ilionekana kama mwanamke yule aliendelea kuungua tu, hata wakati moto umepungua sana. Kutoka ndani yake kabisa yalitoka mayowe na vilio vya kukata tamaa.”Bwana, Bwana, nataka kutoka humu!”

Alijaribu mara nyingi kumfikia Yesu. nilimtazama Yesu, alikuwa na huzuni kubwa katika sura yake. Yesu aliniambia, "Mwanangu, upo hapa pamoja nami ili kuujulisha ulimwengu kwamba malipo ya dhambi ni mauti, kwamba kuzimu ni halisi.”

Nilimwangalia tena yule mwanamke, na mafunza yalikuwa yanatoka kwenye mifupa ya skeleton yake. Hayakudhurika na moto. Yesu aliniambia, "Anafahamu na anayasikia mafunza hayo katika mwili wake."

“Mungu mhurumie!” Nililia moto ulipofikia kilele chake na ule uchomaji ulianza kwa mara nyingine. Kilio kikubwa na kwikwi kilitingisha mwanamke roho. Alikuwa amepotea. Hapakuwa na njia ya kutokea. “Yesu, kwanini yupo hapa?” Niliuliza kwa sauti ndogo, maana nilikuwa naogopa kwelli kweli.

Yesu aliniambia, "Njoo."

Njia tuliyokuwa tunapita ilikuwa na mizunguko, ikizunguka kwenye mashimo haya kwa kadri ya upeo wa macho. Vilio vya wafu waishio, vikichanganyikana na mayowe, vilikuja kwenye masikio yangu kutoka kila upande. Hakukuwa na wakati wa utulivu kuzimu. Harufu nzito ya uozo wa nyama ilitapakaa hewani.

Tulifika kwenye shimo lingine. Ndani ya shimo hili, ambalo ukubwa wake ulikuwa sawa na lile lingine, kulikuwa na skeleton nyingine. Sauti ya mwanaume ililia kutoka shimoni, ikisema, “Bwana, nihurumie.” Ni pale tu walipozungumza ndipo nilipoweza kujua kama ni mwanamke au mwanaume.

Vilio vikubwa vya mayowe vilitoka kwa mwanaume huyu. “Nimekosa, Yesu, nisamehe. Nitoe humu. Nimekuwa mahali hapa pa mateso miaka mingi. Ninakusihi, nitoe.” Kilio cha kwikwi kilitisa skeleton hii. “Tafadhali Yesu, nitoe.” Nilimtaza Yesu nikaona kwamba naye alikuwa analia.

“Bwana Yesu,” mtu huyo alilia kutoka shimo la moto, “nimeteseka vya kutosha kwa dhambi zangu? Imepita miaka arobaini tangu nilipokufa.”

Yesu alisema, "Imeandikwa, Wenye haki wataishi kwa imani!’ Wenye dharau wote na wote wasioamini watakuwa na fungu lao katika ziwa la moto. Hukutaka kuamini kweli. Mara nyingi watu wangu walitumwa kwako kukuonyesha njia, lakini hukuwasikiliza. Uliwacheka na uliikataa injili. Ingawaje nilikufa msalabani kwa ajili yako, ulinikebehi na hukutaka kutubu dhambi zako. Baba yangu alikupa fursa nyingi za kuokolewa. Heri ungelisikiliza.” Yesu alilia.

"Najua Bwana, Najua Bwana!” Yule mtu alilia. “Lakini sasa natubu.”

"Umechelewa," Yesu alisema. "Hukumu imekwishatolewa."

Yule mtu aliendelea, “Bwana, baadhi ya watu wangu watakuja huku, kwa maana nao hawatatubu. Tafadhali, Bwana niruhusu niende nikawaambie kwamba ni lazima watubu dhambi zao wangali duniani. Sitaki waje huku.”

Yesu alisema, "Wanao wahubiri, waalimu, wazee wa kanisa-wote hao wanahubiri injili. Vile vile wana bahati ya kuwa na njia za kisasa za mawasiliano na njia nyingine nyingi za kujifunza kuhusu Mimi. Niliwapelekea watumishi ili waweze kuhubiriwa na kuokoka. Kama hawaamini wanaposikia injili, basi hawatasikia hata mtu akifufuka katika wafu.”

Aliposikia hivi mtu yule alighadhabika sana akaanza kutukana. Maneno machafu ya kufuru yakatoka kwake. Nilitazama kwa mshangao nilipoona moto ukipanda kwenye skeletoni na nyama iliyooza ikaanza kuungua na kudondoka. Ndani ya mifupa hii ya mtu, niliona roho yake. Ilikuwa kama ukungu wa zambarau na uliijaza mifupa yake.

Yesu alisema, "Kuzimu ni halisi, na hukumu ni halisi. Nawapenda sana, mwanangu. Huu ni mwanzo tu wa mambo ya kutisha nitakayokuonyesha. Kuna mambo mengi zaidi yanakuja. Uambie ulimwengu kwa niaba yangu kwamba kuzimu ni halisi, kwamba wanaume na wanawake lazima watubu dhambi zao. Njoo, nifuate. Lazima tusonge mbele.”

Nilisikiliza mwanamke mmoja alipokuwa anazungumza na Yesu kutoka kwenye shimo lingine la moto. Alikuwa ananukuu Neno la Mungu. “Bwana mpendwa, anafanya nini hapa?” Niliuliza. "Sikiliza," Yesu alisema.

Mwanamke alisema, "Yesu ni Njia, Kweli na Uzima. Mtu haji kwa Baba bila kupitia kwake. Yesu ni nuru ya Ulimwengu. Njoo kwa Yesu naye atakuokoa.”

Alipozungumza, roho nyingi zilizopotea zilimsikiliza. Nyingine ziliapa na kumlaani, nyingine zilimwambia kunyamaza, nyingine zilisema, “hivi kweli kuna tumaini?” au “Tusaidie Yesu.” Vilio vya huzuni kubwa vilijaa hewani.

Sikuelewa kitu gani kilikuwa kinatokea. Sikujua kwanini mwanamke yule alikuwa akihubiri injili hapa.

Bwana aliyajua mawazo yangu. Alisema, “Mtoto, nilimwita mwanamke huyu akiwa na umri wa miaka thelathini kuhubiri Neno langu na kuwa shahidi wa injili. Nawaita watu tofauti kwa ajili ya makusudi mbalimbali katika Mwili wangu. Lakini kama mwanaume au mwanamke, mvulana au msichana hamtaki Roho wangu, nitaondoka.

"Ndio, alijibu wito wangu kwa miaka mingi, na alikuwa katika kumjua Bwana. Alikuja kuitambua sauti yangu, na alitenda mambo mengi mema kwa ajili yangu. Alijifunza Neno la Mungu. Aliomba mara nyingi, na maombi mengi yalijibiwa. Aliwafundisha watu wengi njia ya utakatifu. Alikuwa mwaminifu katika nyumba yake

“Miaka ilikwenda hata siku moja aligundua kwamba mume wake alikuwa anatembea na mwanamke mwingine. Ingawaje alimwomba msamaha, alikuwa na hasira na hakutaka kumsamehe na kuokoa ndoa yao. Kweli, mume wake alikosea, na alifanya dhambi kubwa.

“Lakini mwanamke huyu alilifahamu Neno langu. Alijua kusamehe, na alijua kwamba kila jaribu lina njia ya kutokea. Mume wake alimwomba amsamehe. Alikataa. badala yake hasira iliota mizizi. Hakutaka kuileta kwangu. Hasira iliongezeka kila siku na alisema moyoni mwake, “Nipo hapa namtumikia Mungu kwa moyo wote, na mume wangu anatembea na mwanamke mwingine! ‘je hiyo ni sawa’ aliniuliza.

“Hapana sio sawa. Lakini alikuja na kuomba msamaha na kusema kwamba asingerudia tena.

“Nilimwambia, ‘Binti, jikague mwenyewe, uone kama sio wewe mwenyewe uliyesababisha haya”

“Sio mimi Bwana,” alisema, mimi ni mtakatifu, yeye ndiye mkosaji.’ Hakutaka kunisikiliza.

“Muda ulizidi kwenda, hakuweza kuniomba au kusoma Biblia. Alikuwa na hasira si kwa muwe wake tu, bali na kwa wale waliomzunguka. Alinukuu maandiko, lakini hakuweza kumsamehe.

"Hakutaka kunisikiliza. Moyo wake ullizidi kuwa na uchungu, na dhambi kubwa ilimwigia. Uuaji uliingia katika moyo wake mahali ambapo zamani palikuwa na upendo. Na siku moja, katika hasira yake alimuua mume wake na yule mpenzi wa mume wake. Shetani alimwingia kabisa akajiua.”

Niliitazama roho ile iliyokuwa imepotea na kumwacha Kristo na kuhukumiwa moto na mateso milele. Nilisikiliza alivyomjibu Yesu. “Sasa nitasamehe Bwana,” alisema. “Nitoe huku. Sasa nitakutii. Ona Bwana, sasa nahubiri Neno lako. Baada ya saa moja mapepo yatakuja na kunitesa zaidi. Yatanitesa kwa masaa mengi. Kwa sababu nilikuwa nahubiri Neno lako mateso yangu ni makubwa zaidi. Tafadhali, Bwana, nakuomba unitoe.”

Nililia pamoja na yule mwanamke aliyekuwa katika shimo na kumwomba Bwana aniepushe na machungu yote ya moyo. “Usiruhusu chuki iingie katika moyo wangu, Bwana Yesu.” Nilisema

"Haya, tuendelee mbele.” ‘Yesu alisema.’

Tulitembea hadi futi kumi na tano kutoka shughuli hii. Niliviona viumbe vidogo vimevaa nguo nyeusi vikitembea kuzunguka kitu kama sanduku. Baada ya kuchunguza zaidi niliona kwamba sanduku lile lilikuwa jeneza na viumbe vilivyokuwa vinazunguka vilikuwa mapepo. Lilikuwa jeneza la kweli na kulikuwa na mapepo kumi na mawili yakitembea kulizunguka. Walikuwa wanalizunguka jeneza wakiimba na kucheka. Kila mmoja alikuwa na mkuki mkali mkononi mwake, ambao alikuwa akichoma kwenye jeneza kupitia vitundu vidogo.

Kulikuwa na hali ya hofu kuu hewani na nilitetemeka nilipoona yaliyokuwa mbele yangu.

Yesu aliyatambua mawazo yangu, kwa maana alisema, “Mtoto, kuna roho nyingi zikiwa kwenye mateso hapa, na kuna aina nyingi za mateso kwa ajili ya roho hizi. Kuna adhabu kubwa zaidi kwa wale ambao walikuwa wahubiri wa injili halafu wakaanguka katika dhambi, au ambao hawakuitikia wito wa Mungu katika maisha yao.”

Nilisikia kilio kilichoujaza moyo wangu na hali ya kukata tamaa. “Hakuna tumaini, hakuna tumaini!” aliita. Kilio hiki cha kukata tamaa kilitoka kwenye jeneza. Ulikuwa mlio mfululizo wa kukata tamaa.

“Mungu, inasikitisha kweli!” Nilisema. “Njoo.” Yesu alisema, “Twende karibu zaidi.” Baada ya kusema hayo alisogea karibu na jeneza na kutazama ndani. Nami nilifuata, nikatazama ndani. Ilionekana kwamba wale pepo wachafu walikuwa hawatuoni.

Ukungu mchafu wa kikahawia uliijaza jeneza. Ilikuwa roho ya mtu. Mapepo walichoma mikuki yao ndani ya jeneza huku nikiangalia.

Sitasahau kamwe kuteseka kwa roho hii. Nilimlilia Yesu, “Mtoe Bwana, mtoe.” Mateso ya roho yake yalikuwa ya kusikitisha. Laiti kama angelitoka. Nilimvuta mkono Yesu na kumwomba amtoe mtu yule kwenye jeneza.

Yesu alisema, “Mwanangu, amani, tulia.”

Yesu aliposema hivyo, yule mtu alituona. Alisema, “Bwana, Bwana, nitoe. Nihurumie.” Nilitazama ndani ya jeneza na kuona roho. Ndani ya roho kulikuwa na moyo wa mwanadamu, na damu ilibubujika kutoka kwenye moyo huo. Kule kuchomwa mikuki kulikuwa kunaichoma roho yake.

“Sasa nitakutumikia Bwana.” Alisihi, “Nakuomba nitoe.” Nilijua kwamba mtu huyu alisikia uchungu wa kila mkuki uliomchoma.

“Anateswa usiku na mchana.” Bwana alisema, “Aliwekwa hapa na Shetani, na Shetani ndiye anayemtesa.”

Yule bwana alilia,”Bwana, sasa nitahubiri injili ya kweli. Nitahubiri juu ya dhambi na kuzimu. Lakini nakuomba nitoe hapa.”

Yesu alisema, “Mtu huyu alikuwa mhubiri wa Neno la Mungu. Kuna wakati alinitumikia kwa moyo wake wote na kuwaongoza wengi kwenye toba. Baadhi ya watu waliookolewa wananitumikia hadi leo, na miaka mingi imepita. Tamaa ya mwili na udanganyifu wa mali ulimpotosha. Alimruhusu Shetani amtawale. Alikuwa na kanisa kubwa, gari zuri na kipato kizuri. Alianza kuiba sadaka. Alizungumza zaidi nusu uongo na nusu kweli. Hakutaka nimsahihishe. Nilimpelekea wajumbe wangu kumwambia atubu na kuhubiri kweli, lakini alipenda zaidi anasa za dunia hii kuliko maisha ya Mungu. Alijua kutokufundisha au kuhubiri ukweli wowote isipokuwa ule uliofunuliwa katika Biblia. Lakini kabla hajafa alisema kwamba ubatizo wa Roho Mtakatifu ulikuwa ni uongo na wale waliosema kuwa wanaye Roho Mtakatifu walikuwa wanafiki. Alihubiri kwamba unaweza kuwa mlevi na ukaenda mbinguni, hata bila kutubu.

“Alisema kwamba Mungu asingempeleka mtu yeyote kuzimu – kwamba Mungu alikuwa mwema sana asingefanya hivyo. Alisababisha watu wengi kukosa neema ya Bwana. Hata alisema hanihitaji, kwa sababu alikuwa kama Mungu. Alikwenda hadi kiasi cha kuendesha semina kufundisha mafundisho haya ya uongo. Alilikanyaga Neno langu takatifu chini ya miguu yake. Hata hivyo, niliendelea kumpenda.

“Mwanangu, heri kutokunijua kabisa kuliko kunijua halafu ukageuka na kuacha kunitumikia,” Bwana alisema

“Heri kama angelikusikiliza, Bwana!” Nililia. “Heri kama angeijali roho yake na roho za watu wengine.”

“Hakunisikiliza. Nilipokuwa namwita hakusikia. Alipenda maisha ya raha. Nilimwita na kumwambia atubu, lakini hakutaka kunirudia. Siku moja aliuawa na akaja hapa moja kwa moja. Sasa Shetani anamtesa kwa sababu aliwahi kuhubiri Neno langu na kuwaokoa watu wengi kwa ajili ya ufalme wangu. Haya ndio mateso yake.”

Niliangalia mapepo yalivyozidi kuzunguka jeneza. Moyo wa mtu yule ulidunda na damu ya kweli ilichirika. Sitasahau kamwe kilio chake cha maumivu na huzuni.

Yesu alimtazama yule mtu kwenye jeneza kwa huruma kubwa na kusema, “Damu ya roho nyingi zilizopotea iko kwenye mikono ya mtu huyu. Wengi wao wamo katika mateso hivi sasa.” Kwa mioyo ya huzuni mimi na Yesu tulisogea mbele.

Tulipokuwa tunaondoka, niliona kundi lingine la mapepo likienda kwenye jeneza. Yalikuwa na urefu wa kama futi tatu, yamevaa nguo nyeusi, na vitambaa vyeusi kuziba nyuso zao. Walikuwa wanabadilishana zamu kuitesa roho hii. Tunakataa kutubu na kujishusha, utadhani sisi tu ndio tuko sawa wakati wote. Lakini sikiliza roho, kuzimu ni halisi. Tafadhali sana usiende mahali kule.

Mungu alizungumza kama tarumbeta, na sauti yake kama ya maji mengi. “Sililiza ambayo Roho ayaambia makanisa,” alisema. “Iweni tayari, maana kwa wakati msiodhania, nitakuja tena. Nasikia saa ikilia. Ni saa sita. Bwana harusi amekuja kwa ajili ya bibi harusi wake”

Je uko tayari kwa ajili ya kuja kwa Krsito, rafiki yangu? Au uko sawa na wale wanaosema, “Sio leo, Bwana?” Je unaweza kumwita ili uokolewe? Je unaweza kumpa roho yako leo? Kumbuka, Yesu anaweza kukuokoa kutoka maovu yote kama utamwita leo, na kutubu. Omba kwa ajili ya familia yako na wapendwa wako ili wamwendee Yesu wasije wakachelewa.

Sikiliza Yesu anavyosema, “Nitakulinda na mabaya. Nitakuchunga katika njia zako zote. Nitakuokoa. Nitawakoa unaowapenda. Niite leo upate kuishi.”

Tulipozidi kutembea kwenye ile ngazi, sauti zilizidi kukua. Vilio vikubwa vilitoka ndani ya selo. Nilitembea karibu na Yesu, tukafika kwenye selo ya tatu. Mwanga mkali uliimulika selo ile. Ndani yake kulikuwa na mwanamke amekaa kwenye kiti cha kubembea. Akibembea na kulia kama kwamba moyo wake ungepasuka. Sijui kwa nini, lakini nilishtuka kuona kwamba alikuwa binadamu kweli mwenye mwili.

Selo haikuwa na kitu chochote isipokuwa yule mwanamke kwenye kile kiti. Kuta za selo zilikuwa zimejengwa kwa udongo, zimesimama kwenye ardhi. Upande wake wa mbele ulikuwa ni mlango. Ulitengenezwa kwa chuma cheusi na nondo za chuma na kutiwa kufuli. Kwa sababu nondo zilikuwa zimewekwa mbalimbali mimi na Yesu tulikuwa na nafasi ya kuiona selo yote.

Ngozi ya yule mwanamke ilikuwa na rangi ya majivu na madoa meusi kiasi. Alikuwa anabembea mbele na nyuma. Huku akibembea, machozi yalichirizika kwenye shavu zake. Kutokana na mtazamo wake wa huzuni nilijua kwamba alikuwa katika mateso makubwa ya kimya kimya. Nilijiuliza kosa lake lililomfikisha hapa.

Ghafla, mbele ya macho yangu, yule mwanamke alianza kugeuka kuwa maumbo mbalimbali. Kwanza aligeuka kuwa mwanaume kikongwe, kisha kuwa msichana, halafu kuwa mwanamke wa makamu, kisha kuwa mwanamke mzee niliyemwona mwanzoni. Kwa mshangao mkumbwa nilimuona mwanamke huyu akifanya mabadiliko haya, moja baada ya jingine.

Alipomwona Yesu alilia, “Bwana, nihurumie. Nitoe mahali hapa pa mateso. Aliinama kwenye kiti chake ili amfikie Yesu, lakini hakuweza. Mabadiliko yaliendelea. Hata mavazi yake yalibadilika, alivaa kama mwanaume, halafu kama msichana, halafu kama mwanamke mzee. Mabadiliko haya yalionekana kuchukua muda mfupi tu.

Nilimuuliza Yesu, “Kwa nini, Bwana?”

Alipiga kelele tena, “O Bwana nitoe kabla hawajarudi.” Sasa alisimama mbele ya selo, akishikilia nondo za selo kwa nguvu. Alisema, “Najua upendo wako ni kweli, najua upendo wako ni halisi. Nitoe!” Mwanamke yule alipokuwa analia kwa uchungu, niliona kitu fulani kikianza kunyofoa nyama yake.

“Hayuko kama anavyoonekana.” Bwana alisema.

Mwanamke yule alikaa kwenye kiti na kuanza kubembea. Lakini sasa ni skeleton ndio ilikaa kwenye kiti cha kubembea, mifupa ikiwa na ukungu mchafu ndani yake. Mahali ambapo dakika chache zilizopita palikuwa na mwili uliovaa nguo, sasa palikuwa na mifupa mieusi iliyoungua na mashimo ya macho badala ya macho. Roho ya mwanamke yule iliugua na kumlilia Yesu katika toba. Lakini kilio hicho kilikuwa bure, alichelewa.

“Alipokuwa duniani,” Yesu alisema, “mwanamke huyu alikuwa mchawi na akimwabudu Shetani. Alikuwa mchawi na aliwafundisha wengine uchawi. Tangu akiwa mtoto mdogo, familia yake ilishiriki vitendo vya kishirikina. Walipenda giza kuliko mwanga.”

“Mara nyingi,” Bwana alisema, “nilimwita atubu. Alinidharau na kuniambia, ‘Napenda kumtukia Shetani. Nitaendelea kumtumikia.’ Alikataa kweli na alikataa kutubu uovu wake. Aliwafanya watu wengi kumwacha Bwana, baadhi yao wapo hapa kuzimu pamoja na huyu. Angelitubu ningemuokoa pamoja na watu wengi wa familia yake, lakini hakutaka kusikiliza.”

“Shetani alimdanganya mwanamke huyu kwa kumwambia kwamba angepokea ufalme wake mwenyewe kama zawadi ya kumtumikia. Alimwambia kwamba asingekufa, lakini angeishi na Shetani milele. Alikufa akimtukuza Shetani na alikuja hapa na kudai apewe ufalme wake. Shetani, baba wa uongo, alimcheka na kumwambia, ‘ulidhani ningekata ufalme wangu na kukugawa? Huu ni ufalme wako.’ Ndipo alipomfungia kweli selo hii na anamtesa usiku na mchana.

“Akiwa duniani mwanamke huyu aliwafundisha watu wengi uchawi, wachawi weupe na wachawi weusi. Mojawapo ya ushirikina wake ulikuwa kugeuka kutoka msichana, kuwa mwanamke wa makamo, kuwa bibi kizee, na hata kuwa mwanaume. Ilikuwa raha katika siku hizo kujibadilisha hivyo na kuwatishia wachawi wadogo. Lakini sasa anapata maumivu kuzimu, na nyama yake inanyofolewa kila badiliko linapotokea. Sasa hawezi kumudu hali hiyo, na anaendelea kugeuka kutoka umbo moja hadi lingine, lakini hali yake halisi ni ile roho ya ukungu ndani ya mifupa. Shetani anamtumia kwa makusudi yake maovu akimtania na kumdhihaki. Mara kwa mara hupelekwa mbele ya Shetani ili kuteswa na Shetani afurahi.

“Nilimwita mara nyingi, na ningemwokoa. Lakini hakunitaka. Sasa anabembeleza na kuomba msamaha, lakini amechelewa. Sasa amepotea pasipo matumaini.”

Nilimwangalia mwanamke huyu ambaye alikuwa amepotea milele katika mateso na kuugua, ingawaje alikwa mwanamke mwovu, nilimwonea huruma. “Bwana, angalia inavyosikitisha!” Nilisema kwa machozi.

Halafu, kana kwamba Yesu na mimi hatukuwa pale, pepo chafu la kijivu lenye mabawa yaliyovunjika, lenye umbo na ukubwa wa dubu mkubwa alikuja na kufungua mlango wa selo kwa funguo. Alikuwa anapiga makelele kama kwamba kumtia hofu yule mwanamke. Mwanamke yule alipiga kelele za woga mkubwa yule pepo alipoanza kumshambulia na kumtoa kwenye selo.

Yesu alisema, “Pepo hili huja kumtesa mara kwa mara.” Niliona akivutwa kutoka kwenye selo na kupelekwa mahali.

“Bwana Mpendwa,” nilisema, “hatuwezi kufanya kitu chochote?” Nilimwonea huruma sana.

“Amechelewa" Yesu alijibu, “Amechelewa”

Tulitembea kupanda mlima mrefu, mkavu. Tukiwa juu ya mlima tulitazama chini na kuona mto ukitembea. Hakukuwa na mashimo ya moto wala mapepo wabaya, ila mto tu ukitembea kati ya kingo ambazo zilikuwa hazionekani. Kingo za mto zilifichwa katika giza. Yesu na mimi tulitembea karibu na mto, na niliona kuwa ulijaa damu na moto.

Nilipochunguza zaidi, niliona roho nyingi, zimefungwa pamoja. Uzito wa minyororo ulizizamisha hadi chini ya ziwa la moto.

Roho za kuzimu zilikuwa katika moto wa kuzimu. Niliona pia kuwa zilikuwa skeleton zikiwa na roho ya ukungu wa kikahawia.

“Hiki ni kitu gani?” Nilimuuliza Bwana.

“Hizi ni roho za wasioamini na wasioishi maisha ya utakatifu, hawa waliipenda miili yao wenyewe kuliko kumpenda Mungu. Walikuwa ni wanaume waliokuwa wanawapenda wanaume, na wanawake waliokuwa wanawapenda wanawake, ambao hawakutaka kutubu na kuokolewa kwenye dhambi zao. Waliyafurahia maisha yao ya dhambi na kuudharau wokovu wangu.”

Nilisimama karibu na Yesu na kutazama kwenye moto. Moto ulianza kuunguruma kama tanuru kubwa, ukienda na kuharibu kila kitu katika njia yake. Muda si muda ulijaza karibu mkono mzima wa kuume wa kuzimu.

Moto ulisogea hadi futi moja kutoka pale tuliposimama, lakini haukutugusa. Moto ulikuwa unaunguza kila kitu katika njia yake. Niliutazama uso wa Yesu, ulikuwa na huzuni na mwororo. Upendo na huruma kwa roho zilizopotea bado ulikuwa unasomeka kwenye sura yake. Nilianza kulia na kutamani kutoka kwenye sehemu ile ya mateso, kuendelea kukaa pale ilikuwa haivumiliki.

Nilizitazama tena roho zilizokuwa katika moto. Zilikuwa zinawaka kwa wekundu, na mifupa yao ilikuwa mieusi na imechomeka. Nilizisikia roho zao zikilia kwa uchungu na masikitiko.

Bwana alisema, “Haya ni mateso yao. Mnyororo baada ya mnyororo, zimeunganishwa pamoja. Hawa walipenda jinsia moja, waume kwa waume, wake kwa wake, wakifanya mambo yasiyo ya kawaida. Walivuta wasichana na wavulana wengi kwenye vitendo vya dhambi. Walisema ni mapenzi, hatima yake ni dhambi na mauti.

"Najua kwamba wavulana wengi na wasichana wengi, wanaume na wanawake, walifanya vitendo hivi vya aibu kwa kulazimishwa bila kupenda. Najua na sitawahukumu kwa dhambi hii. Lakini kumbuka.”

Yesu alisema, “Nayajua mambo yote, na watu waliosababisha vijana hawa kufanya dhambi wana adhabu kubwa zaidi. Nitahukumu kwa haki. ‘kwa mwenye dhambi nasema, ‘tubu, nami nitakuwa na rehema. Niite, nami nitakusikia.’

"Mara nyingi nimeziita roho hizi zitubu na zije kwangu. Ningezisamehe na kuzitakasa, na katika Jina langu zingekuwa huru. Lakini hawakutaka kunisikiliza. Walipenda raha za mwili zaidi kuliko kumpenda Mungu aishiye. Kwa sababu mimi ni mtakatifu, ni lazima muwe watakatifu. ‘usiguse kitu kichafu, nami nitakupokea.’” Alisema Bwana.

Nilijisikia vibaya nilipokuwa nazitazama roho kwenye ziwa la moto.

“Kama tu wangenigeukia bila kuchelewa,” Yesu aliendelea, “damu yangu ingeliwaosha ili kila mtu aje kwangu. Nilitoa maisha yangu ili hata mwenye dhambi mbaya kuliko wote apate kuishi.”

Tulikuwa hatujakwenda mbali Yesu aliposimama mbele ya selo nyingine. Tulipochungulia ndani, mwanga ulikuja (Yesu alifanya nuru). Nilisimama na kuitazama roho ambayo nilijua ilikuwa katika mateso makubwa. Alikuwa mwanamke mwingine, na rangi yake ilikuwa samawia. Nyama yake ilikuwa imekufa, na sehemu za nyama ambazo zilikuwa zimeoza zilikuwa zikidondoka kutoka kwenye mifupa. Mifupa yake ilikuwa imeunguzwa na kuwa mieusi, na alikuwa na vipande vipande vya nguo. Funza walikuwa wakitambaa kwenye nyama na mifupa yake. Harufu mbaya ilijaza selo yake.

Sawa na yule mwanamke wa kwanza, huyu naye alikuwa amekaa kwenye kiti cha kubembea. Alipokuwa anabembea, alilia na kukumbatia mdoli kifuani pake. Kilio cha kwikwi kilitikisa mwili wake, na kilio kilitoka kwenye selo.

Yesu aliniambia, “Huyu naye alikuwa mtumishi wa Shetani. Alimuuzia roho yake, na ilipokuwa hai alifanya kila aina ya ubaya. Uchawi ni jambo halisi.” Yesu alisema. “Mwanamke huyu alitumia na kuwafundisha watu wangu uchawi na kuwageuza wengi kuelekea njia ya dhambi. Waalimu wa uchawi wanapewa upendeleo na nguvu zaidi kutoka kwa Shetani kuliko wachawi wa kawaida. Alikuwa mtabiri na alipewa pepo la utambuzi na bwana wake.

“Alipendwa sana na Shetani kwa maovu yote aliyoyafanya. Alijua namna ya kutumia nguvu za giza kwa ajili yake na kwa ajili ya Shetani. Alikwenda kwenye ibada za wamwabuduo Shetani na kumtukuza Shetani. Alikuwa mwanamke mwenye nguvu kwa ajili ya Shetani.”

Niliwaza kwamba sijui kazidanganya roho ngapi kwa ajili ya Shetani. Niliitazama roho hii ndani ya mifupa, ikililia mdoli-kipande kichafu cha nguo. Huzuni uliujaza moyo wangu, na machozi macho yangu. Aliushikilia mdoli kama kwamba unaweza kumuokoa, au kwamba angeweza kuusaidia. Harufu ya mauti ilizagaa mahali pale.

Halafu nilimuona akianza kubadilika kama yule wa kwanza. Alikuwa mwanamke mzee wa miaka ya 1930 kisha kuwa msichana wa leo. Mara nyingi alifanya mabadiliko haya mbele ya macho yetu.

“Mwanamke huyu,” Yesu alisema, “alikuwa kama mhubiri wa Shetani. Kama vile ambavyo injili ya kweli inahubiriwa kwetu na wachungaji wa kweli, Shetani naye ana wachungaji wake wa uongo. Alikuwa na nguvu za kishetani kubwa sana, ambazo ilibidi auze roho yake ili azipate. Vipawa viovu vya Shetani ni kama upande wa pili wa shilingi wa vipawa vya kiroho ambavyo Yesu anagawa kwa waumini. Hii ni nguvu ya giza.

“Wafanyakazi hawa wa Shetani wanafanya katika ushirikina, maduka ya vitu vya kishirikina, waonaji kutumia viganja vya mikono, na njia nyingine nyingi. Msemaji wa Shetani ni mtumishi wa Shetani mwenye nguvu. Watu hawa wamedanganyika kabisa na wameuzwa moja kwa moja kwa Shetani. Wafanyakazi wengine wa giza hawawezi kusema na Shetani mpaka wasemaji waseme kwa ajili yao. Wanatoa kafara za wanadamu na wanyama kwa Shetani.

“Watu wengi wanatoa roho zao kwa Shetani. Wanachagua kumtumikia yeye kuliko Mimi. Chaguo lao ni mauti ila kama watatubu dhambi zao na kuniita, Mimi ni mwaminifu, nitawakoa na dhambi zao. Wengi wanauza roho zao kwa Shetani wakidhani kwamba wataishi milele, lakini watakufa kifo kibaya.

“Shetani anadhani kwamba anaweza kumpindua Mungu na kuharibu mpango wa Mungu, lakini alishindwa msalabani. Nilichukua funguo kutoka kwa Shetani, na nina nguvu zote mbinguni na duniani.

“Baada ya mwanamke huyu kufa, alikwenda moja kwa moja kuzimu. Mapepo yalimleta mbele ya shetani, ambapo kwa hasira aliuliza kwanini mapepo yalikuwa na uwezo juu yake, ambapo duniani alidhani ana uwezo juu yao. Duniani yalimtii. Vile vile alimwambia Shetani ampe ufalme aliokuwa amemwahidi.

“Shetani aliendelea kumdanganya hata baada ya kifo chake duniani. Alimwambia kwamba angelimfufua na kumtumia kwa makusudi yake tena. Kwa mbinu za uongo alimpatia roho nyingi, kwa hiyo uongo wake ulionekana kama kweli kwake.

“Ndipo mwishoni, Shetani alimcheka na kumdhihaki. Alimwambia, ‘Nilikudanganya na kukutumikisha miaka yote hiyo. Sitakupa kamwe ufalme wangu’”

Shetani alipunga mikono yake kwa yule mwanamke, na ilionekana kama nyama yake inanyofolewa kutoka kwenye mifupa yake. Alipiga kelele kwa uchungu huku kitabu kikubwa cheusi kikiletwa kwa Shetani. Alikifungua na kupitisha kidole chake kwenye kurasa mpaka alipoliona jina la huyu mwanamke.

"O, ndio, “Shetani alisema, “ulinitumikia vizuri duniani. Uliniletea zaidi ya roho 500.” Alimdanganya na kusema, “Adhabu yako haitakuwa mbaya kama za wengine.”

Kicheko cha hila kilisikika.Shetani alisimama na kumnyoshea kidole mwanamke, na upepo mkali ulivuma na kupajaza mahali pale. Sauti ya mvumo kama radi ilimtoka.

“Ha-ha,” Shetani alisema, “chukua ufalme wako kama unaweza.” Halafu nguvu fulani isiyoonekana ilimbwaga chini.

"Hapa napo unakwenda kunitumikia.” Shetani alicheka mwanamke alipojaribu kunyanyuka. Mwanamke alipiga kelele kwa uchungu nyama ilipokuwa inachanwa na mapepo kutoka kwenye mifupa yake. Aliburuzwa tena mpaka kwenye kifungo chake. Alikumbuka ahadi za Shetani. Alikuwa amemwambia kwamba angekuwa na nguvu zote. Alikuwa amemwambia kwamba asingekufa. Alimwambia kwamba alikuwa na mamlaka juu ya uzima na mauti, na alimwamini. Aliambiwa kwamba Shetani alikuwa na mamlaka ya kuzuia kitu chochote kisimuue. Shetani alimwambia uongo mwingi na kumuahidi mambo mengi.

Yesu alisema, “Nilikuja kuwaokoa watu wengi. Nataka kwamba wote waliopotea watubu na kuliitia jina langu. Sio mapenzi yangu kwamba mtu yeyote apotee, lakini kila mtu awe na uzima wa milele. Inasikitisha, wengi hawatatubu dhambi zao kabla ya kufa, na watakwenda kuzimu. Lakini njia ya kwenda mbinguni ni moja kwa watu wote. Ni lazima uzaliwe mara ya pili ili kuingia ufalme wa Mungu. Lazima uje kwa Baba kwa jina langu na kutubu dhambi zako. Lazima umpe Mungu moyo wako kwa dhati na kumtumikia.

Mtoto,” Yesu alisema, “jambo ninalokwenda kukufunulia sasa ni baya zaidi. Najua litakusikitisha. Vile vile nataka ulimwengu usikie na kujua mambo ambayo Roho anayaambia makanisa.

"Katika selo hizi, kwa kadri ya upeo wa macho yako, kuna roho ziko kwenye mateso. Kila mara selo zinapojaa, kuzimu kunajipanua ili kupokea roho zaidi. Roho ikiwa kuzimu inakuwa na fahamu zake zote. Kama ulikuwa kipofu duniani, utakuwa kipofu kuzimu. Kama ulikuwa na mkono mmoja tu duniani, utakuwa na mkono mmoja tu kuzimu. ”Yesu alisema, “Nilimnyang’anya Shetani funguo za kuzimu miaka mingi iliyopita. Nilifungua selo hizi na kuwatoa watu wangu. Kwa maana wakati wa Agano la Kale kabla sijatoa maisha yangu msalabani, paradiso ilikuwa karibu na kuzimu. Selo hizi zamani zilikuwa paradiso; sasa Shetani anazitumia kwa makusudi yake mabaya na ametengeneza nyingi zaidi.

"O msomaji, tubu kabla hujachelewa milele. Kwa maana wote watakuja kwangu kwa ajili ya hukumu. Paradiso iliondolewa mahali pake karibu na kuzimu nilipokufa na kufufuka tena kwa nguvu za Mungu, Baba yangu.”

Yesu alisema, “Sikuruhusu usikie vilio hivyo kabla mpaka sasa, mtoto. Lakini sasa

nataka nikuonyeshe namna ambavyo Shetani anakuja kuiba, kuua na kuharibu.

Kuzimu huku kuna mateso tofauti kwa roho tofauti. Shetani anatoa mateso haya

mpaka siku ya hukumu, mpaka mauti na kifo vitakapotupwa katika ziwa la moto.

Vile vile, mara nyingine ziwa la moto linakuja kuzimu.”

Katika shimo lililofuata kulikuwa na skeletoni nyingine. Nilisikia harufu ya mauti hata kabla hatujafika. Mtu huyu alikuwa sawa na wengine.

Nilijiuliza roho hii imefanya nini hata kupotea na kutokuwa na tumaini, bila matumaini

isipokwa umilele mahali hapa pa kutisha. Kuzimu ni milele. Niliposikia roho zikilia kwa

mateso, nililia vile vile. Nilisikiliza mwanamke mmoja alipokuwa anazungumza na Yesu kutoka kwenye shimo la moto. Alikuwa ananukuu Neno la Mungu. “Bwana Mpendwa, anafanya nini hapa?” Niliuliza. "Sikiliza," Yesu alisema.

Mwanamke alisema, "Yesu ni Njia, Kweli na Uzima. Mtu haji kwa Baba bila kupitia kwake. Yesu ni nuru ya Ulimwengu. Njoo kwa Yesu naye atakuokoa.”

Alipozungumza, roho nyingi zilizopotea zilimsikiliza. Nyingine ziliapa na kumlaani.

Nyingine zilimwambia kunyamaza. Nyingine zilisema, “hivi kweli kuna tumaini?” au “Tusaidie Yesu.” Vilio vya huzuni kubwa vilijaa hewani.

Sikuelewa kitu gani kilikuwa kinatokea. Sikujua kwanini mwanamke yule alikuwa akihubiri injili hapa. Bwana aliyajua mawazo yangu. Alisema, “Mtoto, nilimwita mwanamke huyu akiwa na umri wa miaka thelathini kuhubiri Neno langu na kuwa shahidi wa injili. Nawaita watu tofauti kwa ajili ya makusudi mbalimbali katika Mwili wangu. Lakini kama mwanaume au mwanamke, mvulana au msichana hamtaki Roho wangu, nitaondoka. "Ndio, alijibu wito wangu kwa miaka mingi, na alikuwa katika kumjua Bwana. Alikuja

kuitambua sauti yangu, na alitenda mambo mengi mema kwa ajili yangu. Alijifunza Neno la Mungu. Aliomba mara nyingi, na maombi mengi yalijibiwa. Aliwafundisha

watu wengi njia ya utakatifu. Alikuwa mwaminifu katika nyumba yake

“Miaka ilikwenda hata siku moja aligundua kwamba mume wake alikuwa anatembea na mwanamke mwingine. Ingawaje alimwomba msamaha, alikuwa na hasira na hakutaka kumsamehe na kuokoa ndoa yao. Kweli, mume wake alikosea, na alifanya dhambi kubwa. “Lakini mwanamke huyu alilifahamu Neno langu. Alijua kusamehe, na alijua kwamba kila jaribu lina njia ya kutokea. Mume wake alimwomba amsamehe.

Alikata, Badala yake hasira iliota mizizi. Hakutaka kuileta kwangu. Hasira

iliongezeka kila siku na alisema moyoni mwake, “Nipo hapa namtumikia Mungu kwa moyo wote, na mume wangu anatembea na mwanamke mwingine! ‘je hiyo ni sawa’ aliniuliza. “Hapana sio sawa. Lakini alikuja na kuomba msamaha na kusema kwamba asingerudia tena. “Nilimwambia, ‘Binti, jikague mwenyewe, uone kama sio wewe mwenyewe uliyesababisha haya” “Sio mimi Bwana,” alisema, mimi ni mtakatifu, yeye ndiye mkosaji.’ Hakutaka kunisikiliza. “Muda ulizidi kwenda. Hakuweza kuniomba au kusoma Biblia. Alikuwa na hasira si kwa muwe wake tu, bali na kwa wale waliomzunguka. Alinukuu Maandiko, lakini hakuweza kumsamehe. "Hakutaka kunisikiliza. Moyo wake ulizidi kuwa na uchungu, na dhambi kubwa ilimwigia. Uuaji uliingia katika moyo wake mahali ambapo zamani palikuwa na upendo. Na siku moja, katika hasira yake alimuua mume wake na yule mpenzi wa mume wake. Shetani alimwingia kabisa akajiua.”

Niliitazama roho ile iliyokuwa imepotea na kumwacha Kristo na kuhukumiwa moto na mateso milele. Nilisikiliza alivyomjibu Yesu. “Sasa nitasamehe Bwana,” alisema. “Nitoe huku. Sasa nitakutii. Ona Bwana, sasa nahubiri Neno lako. Baada ya saa moja mapepo yatakuja na kunitesa zaidi. Yatanitesa kwa masaa mengi. Kwa sababu nilikuwa nahubiri Neno lako mateso yangu ni makubwa zaidi. Tafadhali, Bwana, nakuomba unitoe.” Nililia pamoja na yule mwanamke aliyekuwa katika shimo na kumwomba Bwana aniepushe na machungu yote ya moyo. “Usiruhusu chuki iingie katika moyo wangu, Tulisimama, na alisema, “Tazama na amini.” Niliangalia na kuona maono ya wazi. Katika maono Yesu na mimi tulikuwa juu sana juu ya dunia tukitazama angani. Niliona duara la kiroho juu ya dunia. Duara lilikuwa halionekani kwa macho ya kawaida, ila ya kiroho, niliweza kuliona vizuri. Nilifahamu kwamba maono hayo yalihusika na vita vyetu kupambana na wafalme na wakuu wa anga. Nilipoendelea kuangali niliona kwamba, kumbe, kulikuwa na maduara mengi. Katika duara la kwanza kulikuwa na roho nyingi chafu na ovu. Niliona roho chafu zikichukua umbo la wachawi, na zilianza kuruka angani na kufanya uharibifu mwingi wa kiroho. Nilisikia sauti ya Yesu ikisema, “Katika Jina langu, nawapa watoto wangu mamlaka juu ya wabayahawa. Sikiliza na jifunze jinsi ya kuomba.”

Niliona kitu kingine kikiinuka kutoka duara lingine na kuanza kuzunguka na kutawanywa uchawi. Kisha niliona pepo limeinuka na lilikuwa likifanya mambo maovu duniani. Pepo lilikuwa na roho ya mchawi. Aliweza kugeuka na kucheka, na kutoka katika fimbo mkononi mwake, alimwaga roho wachafu kwa watu mbalimbali. Niliona roho nyingine chafu zikiungana na yule mchawi, na Shetani alimpa nguvu zaidi. “Angalia, mnayofunga duniani, nitayafunga mbinguni,” Yesu alisema. “Shetani lazima afungwe kama maombi ya watakatifu yanataka kuwa na nguvu katika siku hizi za mwisho.”

Kutoka duara lingine niliona mfanya mazingaombwe akiinuka, na alinza kutoa amri. Mvua na moto vilianguka kutoka mbinguni alipokuwa anazungumza. Alizungumza mambo mabaya mengi, na aliwadanganya watu wa dunia. Nilipoendelea kutazama, niliona pepo 64 wengine wawili wakiungana na huyo mfanya mazingaombwe juu ya anga la dunia. Hawa wote walikuwa wafalme wabaya na nguvu za anga.

Hawa waliwapa nguvu wachawi waliojikusanya pamoja mahali fulani ili kufanya uovu. Watenda kazi wa giza waliwazunguka. Mapepo yaliingia na kutoka kama yalivyopenda. “Angalia kwa uangalifu, “Yesu alisema, “maana Roho Mtakatifu anakufunulia ukweli mkubwa.”

Katika maono niliona mambo mabaya sana yakitokea duniani. Uovu ulikuzwa na dhambi ilitapakaa. Nguvu za uovu zilisababisha watu kuiba, kusema uongo, kudanganya,kuumizana, kusema uovu na kushindwa na tamaa ya mwili. Kila aina ya uovu ulimwagwa duniani.

Nilisema, “Yesu, haya ni vigumu mno kuendelea kutazama.” Yesu alisema, “Mwanangu, katika Jina langu, uovu lazima ukimbie. Vaeni silaha zote za Mungu ili muweze kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.”

Roho chafu zilipomwaga uovu wao na matusi juu ya dunia, niliona watu wa Mungu wakianza kuomba. Waliomba kwa Jina la Yesu na kwa imani. Walipokuwa wanaomba, Neno la Mungu lilipambana na mapepo, nayo yalianza kupoteza nguvu. Watakatifu walipoomba, nguvu za uovu zilianza kushindwa. Nguvu za uovu zilivunjika. Wale waliokuwa wamedhoofishwa na nguvu za kuzimu walipata nguvu. Waliopoomba kwa sauti moja, malaika wa mbinguni waliingia katika mapambano. Niliwaona malaika watakatifu wakipigana na wafalme waovu na nguvu za anga, na malaika wa Mungu walikuwa wakiziharibu nguvu za uovu.

Niliangalia, tazama, kulikuwa na mstari juu ya mstari wa jeshi la malaika, kila mstari ukiwa na malaika kama 600. Watu walipokuwa wanamwamini Mungu, malaika walikuwa

wanasogea mbele. Mungu ndiye alitoa amri, na nguvu yake ilikuwa kubwa sana. Aliwapa nguvu nyingi watu wake na malaika kuharibu kazi za Shetani. Mungu alikuwa akipigana na ouvu katika anga. Watu walipoomba na kumwamini Mungu, nguvu za uovu zilikuwa zikiharibiwa. Lakini kulipokuwa na kutokuamini, nguvu za uovu zilianza kushinda.

“Watu wangu ni lazima waamini, na lazima wakubaliane wao kwa wao na mimi,” Bwana alisema, “mambo yote lazima yawekwe chini ya miguu ya Baba” Mbingu na dunia ni lazima zikubaliane kama tunataka kuwaangamiza maadui wetu. Sifa za watu wa Mungu zilipoanza kupanda kutoka duniani, nguvu za uovu zilirudi nyuma. Niliwaona watakatifu wa Mungu wakiomba kwa moyo wao wote kupinga hila za mwovu. Walipofanya hivyo, nguvu za uchawi na laana zilivunjika, na watakatifu walipata ushindi. 65 Ilitokea namna hii. Malaika watakatifu walipopigana na mapepo na nguvu za kuzimu, watakatifu waliokolewa kwa njia ya maombi. Watu walipookolewa, sifa nyingi zilitolewa kwa Mungu na sifa zilileta ushindi zaidi. Ni pale tu ambapo matokea ya maombi hayakuonekana mara moja ndipo sifa zilikoma na ouvu ulianza kushinda vita.

Nilimsikia malaika akisema kwa sauti kubwa, “O Bwana, imani ya watu wako ni dhaifu. Ni lazima wawe na imani kama unataka kuwaokoa kutoka majeshi ya Shetani. Bwana uwe na rehema kwa warithi wa wokovu.”

Sauti ya Mwenyezi ilijibu, “Bila imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Lakini Bwana ni mwaminifu, atawasimamisha.”

Tena katika maono niliona Bwana akimwaga Roho wake kwa wote wenye mwili, na watu waliamini kwamba angefanya yote waliyoomba kwa sababu walikuwa watu wake na walimpenda kweli. Walikuwa na imani kwa Mungu na waliliamini Neno lake, na Mungu aliwaokoa. Na Neno la Mungu lilikua katika nchi.

BWANA ALISEMA, “YOTE YANAWEZEKANA KWA WAO WANAOAMINI. NALIANGALIA NENO LANGU NIPATE KULITIMIZA. FANYENI SEHEMU YENU, NANYI MNAJUA KWAMBA NA MIMI NITAFANYA YANGU. KAMA WATU WANGU WATASIMAMIA KWELI NA KUPIGANA VITA NJEMA, MAMBO MAZURI YA AJABU YATATOKEA KAMA SIKU YA PENTEKOSTE. NIITE NAMI NITAKUITIKIA. NITAKUWA MUNGU WENU NANYI MTAKUWA WATU WANGU. NITAWATHIBITISHA KATIKA HAKI, KWELI NA UAMINIFU.”

KATIKA MAONO HAYA, NILIWAONA WAKRISTO WAKIZALIWA KAMA WATOTO WACHANGA. NILIWAONA MALAIKA WAKISIMAMA JUU YAO KUWALINDA WASIPATWE NA MABAYA. NILIMWONA BWANA WA MABWANA AKIPIGANA VITA VYAO NA KUSHINDA KWA AJILI YAO. NILIWAONA WATOTO HAO WAKIKUA NA KUVUNA MASHAMBA YA BWANA WA UTUKUFU. WALIKUWA WANAFANYA KAZI YA BWANA KWA MOYO WA FURAHA NA WA KUMPENDA MUNGU, WAKIMWAMINI MUNGU NA KUMTUMIKIA. NILIONA MALAIKA NA NENO LA MUNGU WAKIUNGANA KUTEKETEZA UBAYA KUTOKA USO WA DUNIA. NILIONA AMANI DUNIANI WAKATI HATIMAYE KILA KITU KIMEWEKWA CHINI YA MIGUU YA MUNGU.

NDUGU MSOMAJI WEWE AMBAYE UMESOMA HABARI HII NA UMEJIULIZA SWALI , NIFANYEJE? ILI NIWEZE KUEPUKA ENEO HILI BAYA LISILO NA MATUMAINI NA MATESO MAKUU? JIBU:- UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KUMPOKEA YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO. RUDIA SALA HII POPOTE ULIPO.

“ BWANA YESU NAKUPOKEA WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINAAMINI KUWA ULIKUFA MSALABANI KWA AJILI YA DHAMBI ZANGU, ILI MIMI NISIPOTEE BALI NIWE NA UZIMA WA MILELE. NINAKUOMBA YESU ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU NA ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, UNISAFISHE NIWE SAFI MBELE ZAKO, UNIFANYE MTOTO WAKO. AMEN.”

KWA KUSALI SALA HII UTAKUWA UMESAMEHEWA, TAFUTA KANISA LOLOTE LA KIROHO KARIBU NA WEWE SALI PAMOJA NA WATU WA MUNGU, TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO KABLA HUJACHELEWA.

23 Minutes in Hell by Bill Wiese (Bill'swifeAnnettespeaking)
It was about 3:23 in the morning when I woke up. I just remember that because I looked at our digital clock, and I noticed Bill was not next to me, and I heard screaming coming from our living room. I proceeded to go down the hallway. I found my husband in a way I'd never seen him before. If anyone gets to know Bill, he's very conservative by nature, very calm, and a professional man. He's just not the type to get excited or get real emotional over anything, unless it's God at times. But, anyway, I saw him there traumatized, literally traumatized holding his skull, holding his head between his hands and crying out and screaming. He was in a fetal position on our living room floor. I didn't know what to do. I thought he was having a heart attack. I just started to pray and he cried out and said, "Pray that the Lord would take this out of my mind! The Lord took me to Hell. I feel like my body is dying, I can't handle this." So I proceeded to pray over him, and in about ten to twenty minutes he began to calm down. He was literally in a traumatized state, like someone who went to Vietnam and has a reoccurrence, or a horrible car accident where they're reliving it. It was not just someone who had a bad dream and woke up. So I just wanted to testify to that.

(Bill Wiese speaking)

But I was just dropped into a prison cell, just like a regular prison cell, like you imagine, with rough huge stone walls and bars on the door. I didn't know where I was yet. All I knew was that it was extremely hot, terribly hot. It was so hot, I couldn't believe, that I was alive. I felt like I should have disintegrated with this heat, but I was still alive. It was light in the room for a little while, and I believe the Lord's presence was there for me to see the scenery better, but then it got dark after about a minute. I found myself in the cell, and these 4 creatures were in the cell with me. I didn't know they were demons at the time, because I went there as an unsaved person. God took it out of my mind that I was a Christian. I didn't understand why, but He explained it to me on the way back. These creatures, I didn't realize that they were demons, but they were enormous. They were about 12 or 13 feet tall, I was lying on the floor in this cell and I had absolutely no strength in my body. I wondered, "Why can I hardly move, what is wrong with me?" I was just aware of no strength, and I was helplessly lying there.

One Demon just grabbed me and picked me up, and threw me into the wall like a glass. He just picked me up like a glass. That was how light I was, or how strong he was. And threw me into the wall, and every bone in my body just broke. And I felt pain! I just began to lie on the floor there, crying out for mercy, but these creatures don't have any mercy at all, absolutely no mercy. Then one of the demons grabbed me, and drug me back into the cell and began all these torments again, which I really hate to talk about, because I don't like to have to re-live the torment. They began to crush my skull. One demon grabbed me and tried to crush my head. I was screaming and begging for mercy, but no mercy! About this time they each grabbed an arm and a leg and were about to tear off my legs and my arms. I thought, "I can't endure this, I can't endure this!"

(Demons)

I was along side this pit of fire and I saw all these demons all lined up along the walls, all sizes and shapes of every kind, deformed, ugly creatures, you can imagine. They were twisted, deformed creatures, huge ones, small ones. There were giant spiders, huge spiders this big. (5 feet tall) Rats, snakes and worms, because the Bible talks about worms that cover thee (Isaiah 14:11). There are all kinds of abominable creatures everywhere and they seemed to be chained to the walls. I wondered

"Why are these things chained to the walls". I didn't understand that, but there's a scripture on that in Jude 1:6 says, "And the angels who did not keep their proper domain, but left their own abode, He has reserved in everlasting chains under darkness for the judgment of the great day;"

There were things that I am going to say, that I don't know how I knew. In Hell your senses are keener, you are just aware of more than our physical bodies are. I was aware of distances, I was aware of time, and so forth, much more than you are here. I knew these things were assigned to me, to torture me forever in this place.

The one picked me up, and the other one, with his razor-sharp claws; he just shredded my flesh right off. He just tore it off, and had absolutely no care what so ever for this body that God so wonderfully made. It had a hatred that was so intense against me. I wondered, "Why am I alive, why am I living through this? I don't understand why am I not dead." My flesh just hung there in ribbons. And there was no blood, just flesh hanging, because life is in the blood, and there is no life in Hell. And there is no water in Hell. I was there as an unsaved person, so I didn't know these things. I just went there as if I had never accepted the Lord. I was placed over next to the fire that I had seen. I was standing along side that pit. I was beneath a cavern, like a giant cave, with a tunnel going up.

Along side the fire I could see through the flames, just enough to see bodies, people in the fire screaming, screaming for mercy, burning in this place! And I knew I didn't want to go in there. The pain I'd endured already was bad enough, but the heat from that flame I knew was worse. These people were begging to get out.

There were these big creatures lined all around the edge of this Pit, and as the people crawled up trying to get out, they would be shoved back in to the fire and not allowed out. I thought, "Oh, this place is so horrible, so horrible and horrendous." There is no life whatsoever in Hell. It is so strange to be in a world where there is no life. Here we enjoy trees and fresh air, but there it is absolutely all dead. There is no life whatsoever in Hell. It is so strange to be in a world where there is no life. Here we enjoy trees and fresh air, but there it is absolutely all dead.

That's what is going on in Hell, it is so hot. All these things should kill you, but you don't die! You had to keep enduring all these things. I wanted peace of mind, to get away from the screams and to get out of there. It's like when you want to go home at night, when you had a rough day, you just want peace of mind. But there you endured all the screaming and all the torment. And you never ever get away from it, ever. In Isaiah 57:21 it says: "There is no peace," Says my God, “for the wicked?

You are also naked in Hell. It is just another thing to have to endure. Shame! In Ezekiel 32:24 it talks about shame in the pit.

There is Elam and all her multitude, all around her grave, all of them slain, fallen by the sword, who have gone down uncircumcised to the lower parts of the earth, who caused their terror in the land of the living; Now they bear their shame with those who go down to the Pit. And in Job 26:6

Sheol is naked before Him, and Destruction has no covering. That means God can see into Hell, so it is observable to Him. But also you are naked in Hell, just another thing you have to go through.

All this is going on at the same time. You're thirsty, you're hungry, and you're exhausted. You don't get to sleep in Hell either. You need sleep just as you do now. Your body needs sleep. Rev 14:11 says,

And the smoke of their torment ascends forever and ever; and they have no rest day or night,... You never get to sleep. You can imagine how that is, never sleeping. Regarding the water, in Zechariah 9:11, ...I have sent forth thy prisoners out of the pit wherein is no water. Absolutely no water in Hell.

I knew that Hell's location is in the center of the earth. That's were it's at, in the center of the earth. I understood that I was about 3700 miles deep in the earth. We know that the earth's diameter is 8000 miles. Half way would be about 4000. I was about 3700 miles down. In Ephesians 4:9 it says that Jesus descended into the lower parts of the earth.

In Numbers 16:32 says,

and the earth opened its mouth and swallowed them up, with their households and all the men with Korah, with all their goods.

That's were Hell is right now. Later Hell and Death will be cast into the Lake of Fire and then cast into Outer Darkness. That's after Judgment Day, but right now it is in the earth.

God has made mankind the highest form of creation, and these demons are the lowest form of creation. As men we work hard to get ahead in life, we better ourselves, we study. But in Hell, your life is run by demons. These creatures have a zero IQ, absolute ignorant creatures. All they know is hatred for God, hatred for you and torture. And they run your life, and you can't do anything about it.

(No Hope)

The worse thing in Hell, the worse thing, worse than all the torments, was I understood that, first of all, that there was life going on up here on the earth. And that people up here, most people, had no idea that this world even existed down here! They don't even know this is a real world down here and there's billions of people suffering and begging for one chance, if they had an opportunity to get out. But they never get a chance to get out, and being mad at themselves for not taking the opportunity to have received Jesus Christ as lord and savior of their lives, that they are stuck there forever.

This is the worse thing about Hell, that there was absolutely no hope of ever getting out. I understood that. I grasped eternity. I could understand eternity. Here on earth, we can't quite, can't get a hold of it. But there I understood it. I knew I would be there forever and ever, and had no hope of getting out. I thought about my wife. I could never get to my wife! I've always told her that if we were ever separated by any kind of earthquake or something horrible, I said "I'll get to you. I will find you. I'll get to you if we're ever apart." But here I couldn't get to her. I could never see her again. She would never have any idea were I was, and I just could never ever talk to her again. That thought just absolutely bothered me terribly! To not be able to talk to her, get to her, and for her not to know where I was, and have no hope to ever get out! You understand, you never get out of here, ever! See on earth there's always hope. Even people in concentration camps had a hope of getting out, or dying at least, to get out of it. But we've never experienced a totally hopeless situation. In Isaiah 38:18 it says,

"Those who go down to the pit cannot hope for Your truth."

No hope, and the truth is Jesus christ. He is the truth.

(Jesusappears)
About this time, I'm going up this tunnel, and I'm just in absolute fear, hopelessly lost, and fearing these demons. All of the sudden, just all of the sudden, Jesus showed up! "Praise you Lord", Jesus showed up. This bright light lit up the place. I only saw His outline, the outline of a man. I couldn't see his face, it was so bright. I just looked into this light and saw His outline. And I just fell on my knees and collapsed. I couldn't do anything but worship Him. I was so grateful. One second ago I was lost forever, and now all of the sudden I'm out of this place, because I had already known Jesus. Those people can't get out, but I could because I was already saved. I knew and understood that there was no way out of this place, only by Jesus. He is the only way to keep from going to this place.

In Rev 1:6 it says John, when he went to heaven, he saw Jesus that His countenance was as the sun shining in its strength. And when he saw Him, he fell at His feet as a dead man. That's just how I did. I fell at His feet like a dead man. Now you would think that I had a million questions to ask him, but when you're there, all you can do is worship Him and praise His Holy Name, and thank Him for what He saved us from. I said, "Lord why did You send me to this place? Why did you send me here?" He said to me "BECAUSE PEOPLE DO NOT BELIEVE THAT THIS PLACE EXISTS." HE SAID "EVEN SOME OF MY OWN PEOPLE DO NOT BELIEVE THIS PLACE IS REAL." I was shocked at that statement. I thought every Christian has got to believe in Hell. But not everyone believes in a literal burning Hell. I said Lord "why did you pick me?" But He didn't answer me on that question. He said to me, "GO TELL THEM THAT I HATE THIS PLACE, THAT IT'S NOT MY DESIRE FOR ONE OF MY CREATION TO GO TO THIS PLACE, NOT ONE! I NEVER MADE THIS FOR MAN. THIS WAS MADE FOR THE DEVIL AND HIS ANGELS. YOU HAVE TO GO AND TELL THEM! I'VE GIVEN YOU A MOUTH, YOU GO AND TELL THEM." "IT'S NOT YOUR JOB TO CONVINCE THEM. IT'S THE HOLY SPIRIT’S JOB! YOU JUST GO AND TELL THEM!" "TELL THEM I AM COMING VERY, VERY SOON." "TELL THEM I AM COMING VERY, VERY SOON."

(announcer speaking)

The Bible is real plain, we are all sinners, and whoever will call on the name of the Lord will be saved. Jesus said if you will confess me before men, publicly, then I will in turn; confess your name before my heavenly Father and the Holy angels. But if you deny me before men, I will deny you before my Father. I want to ask you to do something. If you've never publicly, in front of other people, if you've never publicly declared Jesus Christ as your Savior, and made Him the Lord of your life, or if you're unsure

whether heaven is your eternal home, remember Jesus hung naked on a cross, in a market place, he hung there for you, He endured your shame.

If you'll pray this prayer from the depths of your heart, God will save your soul, and He'll give you an opportunity in the not to distant future for you to make it public. Pray with us, especially those who are in the congregation and know you should:-

"GOD I BELIEVE IN YOU. YOU ARE MY CREATOR. I AM A SINNER. I SINNED IN MANY POINTS, WILLFULLY, AND UNCONSCIOUSLY. I'VE FALLEN SHORT. I'VE MISSED THE MARK. I'M STAINED WITH SIN. JESUS I BELIEVE IN YOU. YOU ARE THE ETERNAL SON OF GOD. YOU'RE THE LAMB OF GOD, WHO TAKES AWAY THE SIN OF THE WORLD, WHO TAKES AWAY MY SIN. I BELIEVE YOU DIED ON A CROSS. SHEDDING YOUR INNOCENT BLOOD FOR MY GUILTY SOUL. I BELIEVE YOU WERE BURIED AND ON THE THIRD DAY YOU AROSE. YOU ARE ALIVE FOREVER MORE. I CALL YOU MY LORD. I CALL YOU MY SAVIOR. I GIVE YOU MY LIFE. I WILL LOVE YOU, SERVE YOU FOR THE REST OF MY DAYS. I BELONG TO YOU, THE GOOD PARTS, THE BAD PARTS, THE SINFUL PARTS, ALL MY PLANS, ALL MY DREAMS, I GIVE EVERYTHING TO YOU. THY WILL BE DONE IN

ME. I BELIEVE I'M SAVED. NOT BY GOOD WORKS, BUT BY FAITH, BY TRUSTING IN YOU. IN JESUS I PRAY.

AMEN."

>>>>> LOUD, LONG APPLAUSE<<<<<

HITIMISHO.

HAYA NI MAMBO MACHACHE TU AMBAYO NIMEWEZA KUNUKUU KUTOKA KATIKA MAKALA CHACHE ILA ZIKO NYINGI, NI VIZURI UCHUKUE MDA WAKO NA USOME UWEZE KUELEWA. USIWE MIONGONI MWAO HAO WAPINGAO, KAMA ILIVYOANDIKWA KATIKA KITABU CHA EBRANIA 10:26. KWANI HATA YESU ALIPOZALIWA KATIKA KIZAZI KILE WALIPINGA NA KUSEMA SIO MWANA WA MUNGU. WAKAMTESA MSALABANI NA KUMUUA. NA WALIFANYA HIVYO KWASABABU HAWAKUJUA UKWELI. NA SIJUI KAMA YESU ANGEZALIWA KATIKA KIZAZI HIKI TULICHOPO INGEKUWAJE? NAFIKIRI WANGEMCHOMA YESU NA MATARI YA GARI JINSI WANAVYO PINGA UKWELI. NDUNGU MSOMAJI NINAKUOMBEA NEEMA YA MUNGU IWE JUU YAKO UWEZE KUELEWA KWANI IMEANDIKWA TWAOKOLEWA KWA NEEMA TU. NA HAYA MAMBO AMBAYO NIMENUKUU NI BAADHI TU YA MAMBO AMBAYO YESU AKILIANGALIA KANISA ANAONA NI ASILIMIA NDOGO SANA WATAKAOINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI. HII INAMAANA BADO WATU WA MUNGU TUKO KATIKA HALI HIZO NILIZONUKUU KATIKA MAISHA YETU, EEEE MWENYEZI MUNGU TUSAIDIE AMEN.

BY GRACE CHRISTIAN RWEGASHA.

TELL 0788443345 / 0654407080. Email grwegasha@gmail.com














No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...