Saturday, May 17, 2014

KAULI ZA WASANII MBALIMBALI WAKIELEZEA KWA UCHUNGU KIFO CHA ADAM KUMBUANA



Baadhi ya wasanii wa filamu akiwemo Yobnesh Yusuphn(Batuli),Bondi Bin Salim aka Bond, Deogratius Shija na Kulwa Kikumba ‘Dude’wameelezea jinsi walivyopokea kwa uchungu taarifa za kifo cha msanii mwenzao Adam Kumbiana aliyefariki dunia asubuhi ya leo. Wakizungumza leo wasanii hao kwa nyakati tofauti tofauti kila mmoja ameonesha kuguswa na taarifa hiyo huku kila mmoja akielezea jinsi alivyopokea taarifa hizo kwa majonzi makubwa.

Dude
“Adam Kuambiana amefariki kweli,chanzo hakijajulikana zaidi lakini kwa taarifa tulizozipata mwanzo inasemekana asubuhi alijisikia vibaya akaona kama mwili unaishiwa nguvu hivi,kwahiyo watu wakachukua gari kumpelea hospitali ndo akafia kwenye gari. Nawapigia sasa hivi simu Mtitu na Stive Nyerere wanaupeleka mwili hospital, wengi wanasema alianza usiku vidonda vya tumbo.”
Batuli

“Msiba unauma sana, ghafla halafu kijana,inauma sana ninachoweza kuongea kwa sasa hivi, ni swala moja kwanza kukubali matokeo la pili ni kumuombea, ameondoka na sisi tunafuata.”
Bondi
“Kweli na mimi nimesikia hivyo, Adam Kuambiana amefariki akiwa location mitaa ya Sinza, kwahiyo
msiba tumeupokea kwa huzuni kubwa ila tumuombee kwa mungu.” Deogratius Shija “Nimesikitishwa na kifo cha Adam Kuambiana,lakini pengo la Adam Kuambia ni kubwa sana, jamaaa alikuwa jembe kwenye filamu, unajua imekuwa ghafla labda ata angeumwa lakini duh ndiyo hivyo hakuna jinsi tumuachie mungu.”

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...