Thursday, March 27, 2014

HATIMAYE COLONEL MUSTAPHA AWAOMBA RADHI WANAWAKE WA AFRIKA MASHARIKI


Baada ya Nyota Ndogo wiki iliyopita kufanya maandamano na wanawake wengine mjini Mombasa Kenya kupinga kile walichokiita ‘udhalilishaji dhidi yao’ uliofanywa na rapper Colonel Mustafa na kumtaka awaombe radhi, mkali huyo wa ‘Lenga Stress’ amekuwa mpole na kuomba radhi

Mustafa ameliambia gazeti la The Star la Kenya:

“Wana sababu za msingi kama wanawake. Nawaomba radhi wanawake wote wa Afrika Mashariki waliochukizwa na picha lakini ningependa kusema kuwa, wanawake kwenye picha hizo hawakulazimishwa kupose. Siku hizi uanamitindo umeingia kwenye kugeuza mwili kuwa sanaa.”

Picha zilizoleta utata ni zile alizopiga Huddah Monroe.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...