Tuesday, December 18, 2012

SISTER P KITUMBO NDII!!

Rapper wa kike aliyewahi kutamba nchini na ngoma kadhaa ukiwemo‘Anakuja’, Sister P anadaiwa kuwa mjamzito, kwa mujibu wa mtu aliye karibu naye.

Msanii wa kizazi kipya, Tanzanite ndiye aliyeitoa habari hiyo kupitia Facebook kwa kuandika, “hatimae SISTER P apigwa mimba daaaaah, nangoja kuitwa anko daaah siamini.”

Tumeamua kumpigia simu Tanzanite ili kuthibitisha habari hizo ambaye alisema ni kweli kwakuwa Sister P ni kama dada yake na wapo karibu sana.

Tanzanite amesema ujauzito wa Sister P bado ni mchanga lakini amekuwa akionesha dalili zote kuwa ni mjamzito.

Kama ni habari hizo ni za kweli basi hongera kwake Sister P.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...