Wednesday, October 10, 2012

JOKATE MWEGELO, AJA KIVINGINE HII NDIO HABARI ALIYOITANGAZA LEO MCHANA.




Mrembo Jokate Mwegelo baada ya watanzania wengi kumfahamu kwa kujihusisha na ishu za urembo, leo mchana ametangaza goodnews kwa kuzindua kampuni yake ya KIDOTI ambapo pia bidhaa yake mpya ya nywele imezinduliwa.

Ni kampuni ambayo haikua rahisi yeye kuianzisha kutokana na kukatishwa tamaa, alitamani kuwa na hii kampuni toka miaka minne iliyopita lakini mwaka jana ndio akapata mtu wa kumsaidia kutengeneza hizo bidhaa ambazo mtaji wake ni zaidi ya dola za kimarekani elfu thelathini ambazo ni zaidi ya milioni 40 za Tanzania.

Kabla ya kuanza kuzitengeneza hizi nywele, Jokate ambae ana masters ya mambo ya siasa alifanya utafiti wa hiyo biashara kwa karibu mwaka mzima, na sasa zitakua zinauzwa kwenye saluni mbalimbali za kike Tanzania.
Hizi nywele zinatengenezwa hapahapa Tanzania ambapo J amesema sehemu ya faida yake ataitumia kusaidia wasichana wa Ruvuma ambapo timu nzima ya kampuni ya Kidoti ni watu sita.











Team Kidoti.


Millard Ayo na Jokate.

Habari/picha: Milard Ayo blog

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...