Tuesday, February 21, 2012

 DKT BILAL AKABIDHIWA UCHIFU WA KABILA LA KIKONONGO

Makamu Wa Rais wa Jamhuti ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakiwa na mavazi ya asili ya kabila la Kikonongo baada ya kuvishwa na kutunukiwa uchifu wa Kabila la Kikonongo na machifu wa Kijiji cha Inyonga Wilaya ya Mpanda wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Rukwa na Katavi jana.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Mtemi na Chief Mkuu wa Kijiji cha Inyonga, George Mbaula (kulia) na Mtendaji Mkuu wa Machief wa Inyonga, baada ya kumvisha nguo za asili ya Kabila la Kikonongo na kumkabidhi mikoba ya kuwa Chief wa Kabila hilo, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa jana.



Makamu a Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Inyonga Mkoa wa Katavi wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa katavi jana.



Makamu wa Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Inyonga, baada ya kumaliza kuwahutubia katika mkutano wa hadhara akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi jana.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...