Thursday, March 17, 2016

Kadja Nito adaiwa kuchumbiwa


KADJA NITO (5)
Staa wa Bongo fleva Khadija Maige ‘Kadja Nito’.
Mayasa Mariwata
MWANADADA anayefanya poa kwenye ulimwengu wa Bongo Fleva, Khadija Maige ‘Kadja Nito’ anadaiwa kuchumbiwa na kigogo mmoja (jina kapuni) hali inayomfanya kukaa kimya kimuziki.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kilicho karibu na msanii huyo, bi’shosti huyo aliyekuwa akibamba na Wimbo wa Sina Maringo amekuwa akionekana viwanja mbalimbali akijiachia na kigogo huyo. “Sasa hivi mambo yake yamemnyokea, ndiyo maana siku chache zilizopita alionekana akila bata Sauzi, japo haonekani akipiga dili zozote zinazohusiana na kazi zake za kimuziki,” kilisema chanzo chetu.
Baada ya kunasa madai hayo, Showbiz Xtra ilimvutia waya Kadja kujua kama kuna ukweli ambapo alifunguka;“Hilo la kuchumbiwa siyo kweli jamani, ni kweli sionekani kupata dili za shoo hivi karibuni lakini siyo kwamba nimefichwa na mtu, hapana! Niwaambie tu mashabiki wangu, soon mtaona mambo makubwa kutoka kwangu sababu Sauz nilienda kikazi siyo kuuza sura kama wengi wanavyodhani.”

Pokea habari na matukio ya mastaa katika simu yako

Global Publisher_17cm x 25cm_Ad1 copy

Wednesday, March 16, 2016

Wasanii Bongo Movie wampongeza Makonda


Makonda (16)
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisalimiana na msanii wa Bongo Movie, Aunt Ezekiel.
Makonda (15)
Mboni Masimba akimpatia Paul Makonda zawadi ya keki.
Makonda (14)
Steve Nyerere akitoa neno katika hafla hiyo.
Makonda (13)
RC Paul Makonda akiongea na mastaa mbalimbali wa Bongo katika hafla hiyo ya kumpongeza.
Makonda (11)
Mwanamuziki Mrisho Mpoto naye akitoa nasaha zake kwa Mhe. Paul Makonda.

Tuesday, March 15, 2016

Usikose Usiku wa kuimba Maisha Basement leo....Kiingilio 5,000 tu


BETHDEI YA MWANA-FA NA BARAKA DA PRINCE MAISHA ILIVYOFANA MAISHA BASEMENT CLUB WEMA NDANI


JUMAPILI ya jana mastaa kibao wa muziki wa Bongo Fleva walihudhuria sherehe ya kuzaliwa kwa msanii Baraka Da Prince na Mwana-FA iliyofanyika katika Ukumbi wa Maisha Basement ulipo Kijitonyama jijini Dar.
Sherehe hiyo ilipambwa na burudani kutoka kwa wasanii Mirror, Mo Music, Ali Kiba, T.I.D, Ommy Dimpoz, Barnaba Boy na wengine kibao sambamba na burudani ya nguvu kutoka kwa DJ Ommy Craizy, Ally B na Tass.














POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...