Monday, March 30, 2015

DIAMOND, ZARI HATARINI KUMALIZWA

 
TAHADHARI ichukuliwe! Habari zikufikie kuwa, baada ya staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz‘ na mpenzi wake, Zarinah Hassani ‘Zari’, kuhamia kwenye mjengo wake mpya uliopo Madale jijini Dar, imebainika kuwa familia hiyo inaishi roho mkononi kufuatia ulinzi sifuri, jambo linalowafanya kuishi kwa hofu tupu.
Nyumba mpya ya Diamond aliyohamia hivi karibuni.
TUJIUNGE NA CHANZO CHA HABARI
Kikizungumza kwa hofu juu ya familia hiyo, chanzo chetu makini kilipasha kwamba, pamoja na Diamond kutumia mamilioni ya fedha kujenga nyumba hiyo ya gharama kubwa, sasa changamoto imehamia kwenye ulinzi na usalama wao.
Muonekano wa eneo ilipo nyuma ya Diamond iliyopo Madale jijini Dar.
“Jamani watu wanampongeza Diamond kwa kuhamia nyumba mpya lakini wale jamaa aisee wanapaswa kuombewa kila kukicha.
“Pamoja na kushusha mjengo wa maana bado changamoto ni juu ya ulinzi wao.
DIAMOND ANAISHI KIZAMANI?

“Huwezi kuamini Diamond bado anaishi kizamani sana na sijui kwa nini anajiamini kiasi hicho wakati anajua wazi kuwa yeye ni staa wa Afrika na hapaswi kuishi kwa ulinzi hafifu.
MAENEO HATARISHI?
“Nasema hivi kwa sababu hata maeneo anayoishi ni hatari sana kwake hivyo anatakiwa kuwa na ulinzi mkali ili tu siku moja asije akafanyiwa kitu ambacho taifa likaingia kwenye hasara ya kumpoteza nyota mkubwa kama yeye.
“Nina uhakika asilimia mia moja Diamond hadi leo hajaanza hata kufanya process (taratibu) za kuchukua silaha (bastola).
“Mimi naijua vizuri Madale ni sehemu ambayo watu huwa wanavamiwa mara kwa mara na wanaishi kwa hofu kama Diamond anavyoishi.
HIKI NDICHO KINACHOMPONZA
“Kitu kingine kinachomponza Diamond ni ishu ya kuweka kila kitu kilichopo ndani kwake mitandaoni. Usione kila mtu anasifia lakini kuna wengine wanavitolea macho.
“Kwa mfano katupia picha za toilet (choo) ambacho kimepakwa dhahabu na kusema kimegharimu shilingi milioni 70.
“Hajakaa sawa akatupia picha za jikoni kwake kuna vitu vingi vya thamani kubwa kila mahali mpaka kwenye korido kuna flat screen (runinga). Huko si ni kuwakejeli watoto wa mbwa? Ni vizuri akaacha kufanya hivyo kwa sababu anawapa watu tamaa,” kilitiririka chanzo hicho.
ANA ULINZI GANI?
Juu ya ulinzi wa nyumbani kwa Diamond, chanzo hicho kilidai kwamba, mbali na baunsa anayewalinda aitwaye Mwarabu hakuna askari wa silaha anayelinda nyumbani hapo hivyo jamaa anatakiwa kufanya haraka kuajiri walinzi wenye silaha.
BOFYA HAPA KUMSOMA DIAMOND
Baada ya habari hizo na uchunguzi wa kutosha, Ijumaa Wikienda lilimsaka Diamond a.k.a Dangote au Chibu ili kujua namna anavyoishi na jinsi anavyoimarisha ulinzi wake na familia kwa jumla.
Diamond, mbali na kukiri kuwa na hofu, alikuwa na haya ya kusema: “Suala la ulinzi wangu nalijua mwenyewe lakini zaidi watu wanatakiwa kujua mimi nipo na mlinzi na ninaendelea kuimarisha ulinzi wa nyumbani kwangu.
“Sidhani pia kama ni suala zuri sana kwa watu kujua siri za ulinzi wangu ila mambo mengi ya kujilinda niko kwenye michakato ya mwisho kukamilisha na soon (haraka) mambo yote yatakaa levo maana huwezi ukafanya kila jambo kwa wakati mmoja,” alisema Diamond huku akikubaliana na ushauri wa gazeti hili juu ya kuongeza ulinzi alionao wa baunsa.
ILIWAHI KUMTOKEA SUGU
Huko nyuma iliwahi kumtokea Mwanamuziki Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) ambapo alikuwa amerejea kutoka nchini Uingereza.
Akiwa amepanga nyumba nzima maeneo ya Tegeta, Dar, Sugu alifanyiwa makala ya runingani na kuonesha vitu vya thamani vya nyumbani kwake.
Siku chache baada ya kipindi hicho kuruka runingani, jamaa huyo alivamiwa na kuporwa kila kitu lakini yeye hakudhurika

PLATINUM YA YANGA YAZIDI KUPOTEA MABOYA ZIMBABWE

WANAISUBIRIA Yanga? Ni suala la kujiuliza kwa harakaharaka kwa klabu ya FC Platinum ya Zimbabwe, jana kufungwa kirahisi katika mchezo wa ligi kuu nchini humo, dhidi ya Caps United.
Timu hiyo ilikuwa ugenini ambapo ilikubali kichapo cha
bao 1-0, ukiwa ni mchezo wa raundi ya pili ambapo kichapo hicho kimeifanya kushika nafasi ya 10 na pointi moja, baada ya kutoa sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa ufunguzi wa ligi hiyo. 
Muuaji wa Platinums,  Ronald Pfumbidzai wa Caps
Kichapo hicho kimemuweka kocha wa Platinum, Norman Mapeza, kutokana na matokeo mabaya katika
michezo ya hivi karibuni.
 Duru za michezo kutoka nchini humo zinasema kuwa 
huenda kocha huyo akafungashiwa virago huku 
kichapo cha Yanga kikitajwa kuwa chagizo kuu.

Matajiri hao wa madini, hawajashinda katika michezo mitatu ambapo mkosi ulianzia kwa Yanga, kisha kulazimishwa sare ya mabao 2-2 kabla ya jana Jumapili kula mweleka mbele ya watoto wa mjini, Caps.
Roho mkononi... Kocha wa Platinum Mapeza huyo hatarini kufukuzwa kutokana na matokeo mabaya
Timu hiyo itakwaana na Yanga Jumamosi wikiendi hii, katika mkondo wa pili wa michuano ya Kombe la Shirikisho hatua ya mtoano, lakini Yanga ina faida ya ushindi wa mabao 5-1, hivyo Platinum inahitaji ushindi wa mabao 4-0.

Friday, March 27, 2015

LADY JAYDEE AJICHAGULIA JENEZA

Uchuro? Baada ya kutundika mtandaoni kwa mara nyingine picha za jeneza alilojiandalia litakalotumika siku akiaga dunia, mwanamuziki Judith Daines Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee au Jide, amelaaniwa vikali na mashabiki wake kwa kitendo hicho.
Mwanamuziki Judith Daines Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee au Jide.
ABADILI RANGI
Mwaka 2012, Jide alitupia mtandaoni picha za jeneza lake lenye mchanganyiko wa rangi ya zambarau na nyeupe lakini safari hii amebadilisha na kutupia mengine mawili yenye rangi ya krimu na nyeupe.
MANENO KUNTU
Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo anatumia jina la jidejaydee, juzi, mwanadada huyo, pamoja na picha hizo mbili, alisindikiza na maneno kuntu kwa chini yaliyosomeka, ‘Nimebadilisha mawazo yangu, sitaki tena lile la zambarau. Moja kati ya hayo hapo juu. Msinimaindi. Kila mtu atakufa. Nilikuwa nafikiria pia iwe kwa waalikwa tu. Sitaki kufunuliwa’.
MASHABIKI WAMLAANI
Risasi Jumamosi liliinyaka ishu hiyo sekunde chache baada ya Jide kuitupia ambapo ndani ya muda mfupi ‘posti’ hiyo ilikuwa na maoni mengi ya kulaani kitendo hicho.
Baadhi ya mashabiki walieleza waziwazi kuchukizwa na jambo hilo alilolifanya staa wao wanayempenda.
SEHEMU YA MAONI
“Kifo kipo kwa kila binadamu lakini hatutakiwi kukifikiria hivyo dada (Jide) unamkosea muumba wako.
“Wewe ni kioo changu, ila kwa hili kwa kweli sijalipenda.
“Jamani dada mbona unatutisha au haupo sawa leo?
“Wewe wajina umefikiria nini lakini?
“Kama umeshaona unakufa sema tujue.
Muonekano wa jeneza hilo.
“Duh! Dada fanya maombi hiyo ni roho ya umauti.
“Dada nini tena mbona unamkufuru Mungu?                      Hata kama una machungu kiasi gani, huwezi kufanya hivyo kwani ni mipango ya Mungu. Muombe akusamehe.
“Wewe Jide wewe huogopi lakini?
“Najua sote tupo njia hiyo lakini kwa nini leo umeamua kutuandikia hivyo? Naomba mipango ya shetani ishindwe!” ilisomeka sehemu ya maoni hayo iliyoungwa mkono na baadhi ya mashabiki wake waliojawa na simanzi.
MCHUNGAJI AMUUNGA MKONO
Akizungumzia tukio hilo, mchungaji maarufu jijini Dar alisema kuwa, kila mtu anatakiwa kujiandaa kwa kuwa kila nafsi itaonja umauti hivyo ni vema kujiandaa kwa kutenda mema.“Maandalizi yanayopaswa kuwa makubwa ni ya kiroho kwa kuhakikisha unatenda mema ili kupata tiketi ya kwenda peponi na kukwepa adhabu ya Jehanamu,” alisema mchungaji huyo.
KUTOKA RISASI JUMAMOSI
Kifo ni haki yetu lakini si vema kumchuria mtu au kujichuria kwa kuwa ni tukio lisilozoeleka katika maisha ya mwanadamu.

MZIMU WA KANUMBA WADAIWA KUUA WAWILI

HII ni habari ya kutisha! Takriban miaka mitatu imekatika tangu kifo cha aliyekuwa staa wa Bongo Movies, Steven Kanumba huku watu wawili wakifariki dunia kwa nyakati tofauti lakini nyuma ya pazia ya vifo vyao, mzimu wa Kanumba unatajwa kuhusika kutokana na watu hao kutaka kuishi mahali pa marehemu huyo, endelea kusoma Risasi Jumamosi.
Aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba.
SOMA TUKIO HILI LA KUSHANGAZA
Itakumbukwa kwamba, baada ya kifo cha Kanumba, mama yake mzazi, Flora Mtegoa ndiye aliyeshika jukumu la kusimamia mali za marehemu mtoto wake (alikuwa na haki).
Miongoni mwa mali hizo ukiachilia mbali, magari, vifaa vya kurekodia filamu, viwanja na filamu zilizokuwa hazijalipwa, mama Kanumba aliimiliki ofisi ya Kanumba iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Kanumba The Great Film iliyokuwa Sinza.Hata hivyo, hivi mapema Februari, mwaka huu, mama Kanumba alitoa vitu kwenye ofisi hiyo kwa madai ya kushindwa kulipa pango, hivyo ofisi ikawa wazi.
KILICHOTOKEA SASA
Habari ambazo gazeti hili ilizipata zilidai kwamba, mpangaji mwingine aliikodisha ofisi hiyo kwa mkataba wa mwaka mmoja lakini hivi karibuni mtu huyo amefariki dunia.Msikilize shuhuda: “Kuna jamaa alipanga kwenye ofisi iliyokuwa ya Kanumba mara tu baada ya mama Kanumba kuondoka vitu kwa kushindwa kulipia mkataba mpya.

HUKUMU DNA MTOTO WA NAY APRILI 8 MWAKA HUU

LILE sakata la mtoto si wa Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kwa mujibu wa madai yaliyotolewa na mzazi mwenzake, Siwema limeingia hatua nyingine baada ya ofisi ya mkemia mkuu wa serikali kusema majibu kamili ya kipimo cha vinasaba ‘DNA’ yatatolewa Aprili 8, mwaka huu.
Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa na mzazi mwenzake Siwema pamoja na mtoto wao.
Akizungumza na Risasi Jumamosi juzi jijini Dar, Nay alisema kila kitu kimekwenda sawa, hivyo anachosubiri ni hayo majibu ili ajue moja kwamba mtoto huyo mwenye miezi mitatu  ni wa nani kati yake yeye na mwanaume aliyetajwa na Siwema mwenyewe.
“Ndiyo natoka sasa kwenye ofisi ya mkemia. Hukumu ya DNA ile ni baada ya wiki mbili kuanzia leo (juzi Alhamisi). Lakini we acha tu. Mh! Nimeshafanya kila kitu, ni wao tu,” alisema Nay.
Aliongeza: “Ila mimi nashangaa. Yule mkemia aliyenipima, kaniambia, ‘Nay hukuwa na haja ya kupima DNA, mbona kwa uzoefu wetu hapa ukimwangalia mtoto anaonekana ni wako, ila kwa sababu umeamua kupima mwenyewe sawa.
‘Nay wa Mitego’ akiwa na Siwema.
“Nimeamua hivi ili mtoto aje kuwa na amani ukubwani, maana ujue atakapokua atakumbana na madai ya mama yake kwenye mitandao, sasa ni bora aje ajue ufumbuzi ulipatikanaje. Kama baba ni mimi au yule mzee anayemsema Siwema atajua.”
Risasi Jumamosi: “Hivi Nay, ikithibitika mtoto si wako utafanya nini?”
Nay: “Namrudisha kwa mama yake maana mimi nitakuwa baba haramu.”
Nay alisema siku ya kupima damu, alikwenda yeye na mtoto huyo ambapo walitumia dakika saba kutolewa damu kwa wote wawili. Bado mtoto huyo anaishi naye nyumbani kwake, Kimara, Dar.

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...