Friday, February 28, 2014

MESS JACOB CHENGULA KUFANYA TAMASHA LA KUZINDUA ALBAMU YAKE YA MUNGU HABADILIKI - UBUNGO PLAZA HAPA BONGO


KUELEKEA BONANZA LA JOGGING DAR LIVE, ACB, WARATIBU WAWEKA WAZI MIKAKATI YAO







Meneja Masoko wa Global Publishers, Innocent Mafuru (kushoto) akiwatambulisha wageni waliofika ofisi za Global Publishers kuelezea maandalizi ya Bonanza la Jogging litakalofanyika Dar Live Jumapili hii.


Kutoka kushoto ni waratibu wa Bonanza la Dar Live, Rajab Mteta 'KP', Mshauri Barandu wakiwa na Mkuu wa Masoko wa Akiba Commercial Bank (ACB), Innocent Ishengoma.


Mhariri Mtendaji wa Global Publishers Ltd, Richard Manyota akiwakaribisha wageni Global.


Mkuu wa Masoko wa Akiba Commercial Bank (ACB), Innocent Ishengoma akiongea na wafanyakazi wa Global (hawapo pichani) kuhusu walivyojipanga kulidhamini Bonanza la Jogging Dar Live.


Mratibu wa Bonanza la Dar Live, Rajab Mteta 'KP', akieleza mikakati waliyonayo kuelekea Bonanza la Jogging Jumapili.


Mratibu wa Bonanza la Dar Live, Mshauri Barandu akiongea na wanahabari (hawapo pichani).


Mhariri wa Gazeti la Ijumaa, Amran Kaima akiuliza jinsi waandaaji walivyojiandaa katika Bonanza la Jogging.

Mwakilishi wa mmoja wa wadhamini wa Bonanza la Jogging litakalofanyika Dar Live Jumapili hii, Innocent Ishengoma kutoka Akiba Commercial Bank (ACB), pamoja na waratibu wa bonanza hilo leo wametembelea ofisi za Global Publishers Ltd kuelezea walivyojipanga kuelekea katika bonanza hilo litakalofanyika ndani ya Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakheem, Dar.

Bonanza hilo ambalo hukusanya maelfu ya wanajogging jijini Dar limedhaminiwa pia na Mfuko wa Pensheni (PSPF) na Damu Salama.

(PICHA NA ERICK EVARIST / GPL)

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, ATEMBELEA MRADI WA MAJIKO SANIFU NA KUZURU KABURI LA SOKOINE MONDULI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka ndani ya moja ya nyumba zinazotumia majiko sanifu wakati alipotembelea katika kijiji cha Enguiki Wilaya ya Mondoli Mkoani Arusha

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Zakia Bilal, akicheza ngoma ya kimasai na wananchi wa kijiji cha Enguiki Wilayani Monduli Mkoani arusha walipofika kijijini hapo kwa ajili ya kuzungumza na wananchi hao

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Dkt. Binilith S. Mahenge, akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Enguiki Wilayani Monduli Mkoani Arusha, ambapo ameambatana na Makamu wa Rais kwenye ziara hiyo.

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Zakia Bilal, akisalimiana na Wananchi wa kijiji cha Enguiki Wilayani Monduli Mkoani arusha walipofika kijijini hapo kwa ajili ya kuzungumza na wananchi hao

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea kifimbo kutoka kwa wazee wa kijiji cha Enguiki Wilaya ya Mondoli Mkoani Arusha mara baada ya kusimikwa kuwa kiongozi wa kabila la kijiji hicho.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkuu wa karakana ya utengenezaji Majiko Sanifu Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha Prof. Robert V. Lange


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa karakana ya utengenezaji Majiko Sanifu Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha Prof. Robert V. Lange juu ya kusafisha na kuyafanya maji kuwa salama, wakati alipotembelea sehemu ya karakana hiyo inayotumia umeme wa nguvu za jua (Solor Power Energe)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa karakana ya utengenezaji Majiko Sanifu Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha Bw. Kisioki Moitiko kuhusu utengenezaji wa majiko hayo, wakati alipotembelea kwenye karakana hiyo

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Zakia Bilal, akiweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekua Waziri Mkuu wa awamu ya kwanza Marehemu Edward Moringe Sokoine, wakati alipozuru kijijini kwa marehemu Monduli juu Mkoani Arusha

SPORTS! TFF YASITISHA MKATABA WA KOCHA KIM POULSEN



                                                   Timu ya Taifa ya Tanzania

Hatimaye Shirikisho la Kabumbu nchini Tanzania TFF limetangaza kuvunja mkataba wake na Kocha mkuu wa Timu ya taifa ya soka ya Tanzania Taifa Stars Kim Poulsen kwa kile kilichoelezwa maafikiano ya pamoja baina ya kocha huyo,TFF, na Serikali.
Jamal Malinzi ambaye ni Rais wa Shirikisho la soka Tanzania amesema kuwa huo ni utaratibu wa kawaida hasa baada ya wadau mbali mbali kuona kuwa huu ni wakati wa kufanya mabadiliko ya lazima katika benchi la ufundi la Taifa Stars ambayo inajiandaa kwa mechi za kufuzu kwa Fainali za kombe la mataifa Afrika hapo mwakani zitakazofanyika nchini Morocco.
Kuhusu gharama za kuvunja mkataba na Kocha huyo Bwana Malinzi amesema serikali haitagharamia uvunjaji huo wa mkataba na kocha huyo na badala yake wapo wadau waliojitokeza kugharamia kutokana na kuona umuhimu wa kufanya mabadiliko katika kipindi hiki kwa faida ya soka la Tanzania.
Kwa Upande wake Kocha Kim Poulsen amesema na rekodi yake inaonyesha kuimarika kwa soka la Tanzania katika kipindi cha takriban miaka miwili aliyokuwa akikinoa kikosi cha Taifa Stars lakini kusitishwa mkataba ni jambo la kawaida kwa kocha yeyote baada ya kipindi fulani kutoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine na ndiyo sehemu ya maisha.
“Kama kocha unapoona ndiyo umefanya kazi yako,unapaswa kuangalia mbele zaidi baada ya kufanya kazi yako si lazima uendelee kuwa hapo, mnakaa na kujadiliana na kuachana kwa amani kisha unapaswa kusonga mbele,ninaondoka nikiwa najivunia kipindi nilichofundisha soka hapa,na ninawatakia kila la kheri Tanzania na Taifa Stars kwa ujumla.”alisema Poulsen.
Kuhusu Kocha mpya wa Taifa Stars Jamal Malinzi ambaye ni Rais wa TFF amesema hadi sasa wapo makocha watatu raia wa Uholanzi ni wawili na Mjerumani mmoja wanaosailiwa kwa ajili ya kumrithi Kim Poulsen,lakini moja ya vigezo Malinzi amesema kuwa ni lazima kocha huyo awe amewahi kuipeleka kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika moja ya nchi zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara.
Katika hatua nyingine kocha Salum Madadi ameteuliwa kukaimu nafasi iliyoachwa wazi na Kim Poulsen ambapo kocha huyo akisaidiwa na Hafidh Badru kutoka Zanzibar watasimamia Taifa Stars kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia iliyoko kwenye kalenda ya FIFA baadaye mwezi ujao.

MAREKANI KULETA UMEME AFRIKA( HASA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA)



Marekani inasema umeme utawafikia zaidi ya watu milioni 50
Wabunge nchini marekani wameidhinisha mpango wa kuleta umeme kwa zaidi ya watu millioni hamsini katika jangwa la Sahara barani Afrika na hivyo basi kutoa fursa kwa mradi huo wa serikali ya Obama kuanza kutekelezwa.
Mswada huo uliopitishwa na kamati ya maswala ya kigeni nchini humo unalenga kujenga megawati elfu ishirini barani Afrika ifikiapo mwaka 2020 na kuwafikia watu elfu hamsini ambao wanaishi bila umeme.
Mpango huo ulitangazwa na rais Obama wakati wa ziara yake barani afrika mnamo mwezi juni mwaka jana.
Mswada huo utahitajika kupitishwa na bunge la wawakilishi pamoja na lile la sineti lakini hatua hiyo ya kamati ya maswala ya kigeni ni dhihirisho tosha kwamba unuangwa mkono na pande zote za kisiasa.

KAMPENI ZINAVYOENDELEA JIMBONI KALENGA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrfod Slaa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Kiwele katika mkutano wa kampeni wa uchaguzo mdogo wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa juzi.
Juu na chini Mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Grace Tendega, akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Kiwele katika mkutano wa kampeni juzi.

Wananchi wa kijiji cha Kiwele wakiitikia moja ya salama za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wakati wa mkutano wa kampeni za chama hicho za uchaguzo mdogo wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa juzi.
Mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Grace Tendega akisalimiana na mmoja wa wazee wa kijiji cha Kiwele, baada ya mkutano wa kampeni uliofanyika kijijini hapo juzi.





Tuesday, February 25, 2014

MZUNGU ALIYEKAMATWA NA KILO 5 ZA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE DAR-ES-SALAAM





Raia wa Henellic, Alexamdrios Atanasios, amekamatwa maafisa wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Jumapili usiku Februari 24, 2014, akiwa na kilo tano za madawa ya kulevya.

Habari zinasema mzungu huyo alikamatwa wakati wa upekuzi, akijiandaa kupanda ndege ya Swiss air kueleke jijini Zurich, Uswisi. Madawa hayo yalikutwa yakiwa yamefichwa kwenye “sakafu” ya begi lake baada ya mitambo ya kisasasa yaupekuzi, kugundua kuwa kulikuwa na ‘mzigo’.

Habari zinasema, kwa sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwenye kituo cha polisi cha uwanjani hapo akisubiri taratibu za kisheria ili afungukliwe mashtaka.

FAMILIA YA MISS TZ YAGOMBANIA MAITI....MKASA HUU HAPA


FAMILIA ya Miss Tanzania 1999, Hoyce Nambuo Temu, inadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa wapi pa kumzikia mwanafamilia mwenzao, Emmanuel Lewi Nambuo Temu (33) aliyefariki dunia Februari 15 mwaka huu katika Hospitali ya Temeke, Dar.

Miss Tanzania 1999, Hoyce Nambuo Temu.

Mama wa marehemu Emmanuel, Hilda Lewi Nambuo ameshikilia msimamo kwamba, mwanaye akazikwe kwenye makaburi waliyozikwa mababu zao yaliyopo kwenye Kijiji cha Kikarara, Old Moshi, Kilimanjaro lakini mjomba mtu aitwaye Jacob Nambuo Temu anapinga.
Jacob na Hilda ni mtu na mdogo wake, Hilda akidaiwa kuwa mkubwa. Jacob ni mjomba wa Hoyce na Hilda ni shangazi yake.

Sakata hilo lilifikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam na kupewa jalada namba 7/2014 ambapo mama wa marehemu anaitaka korti iamuru mwili wa marehemu ukazikwe huko kwa kuwa huo ndiyo wosia wa marehemu.

“Kutoruhusu mwili huo kuzikwa tunakokutaja kutaongeza uhusiano wa ugomvi wa mama wa marehemu na kaka ambaye ni mlalamikiwa,” imesema sehemu ya hati ya mahakama hiyo iliyosainiwa na Hakimu K. Mkwawa.

Mheshimiwa Mkwawa alisema kutokana na ombi la mama wa marehemu, mahakama hiyo imezuia kuchukuliwa kwa mwili huo kutoka katika Mochwari ya Hospitali ya Temeke, Dar hadi Februari 25, mwaka huu (leo) ambapo atasikiliza pande zote mbili kuhusiana na sakata hilo.
Kwa upande wake mjomba mkubwa wa marehemu, Dk. M. Nambuo Temu aliyeko nje ya nchi ametuma ujumbe akisema ameridhia marehemu akazikwe kwenye makaburi ya mababu huko Old Moshi.

Katika barua yake (nakala tunayo) aliyowaandikia ndugu zake, Hoyce na Rachel Temu na wahusika wengine wa mgogoro huo, Dk. Temu alisema amesikitika kusikia kuwa, Jacob hataki Emmanuel azikwe nyumbani kwao Old Moshi kama yeye marehemu alivyoagiza katika wosia wake.
“Yeye (Emmanuel) mwenyewe kabla ya kufariki dunia aliwahi kumwelezea rafiki yake Noel kuwa akifa akazikwe kwa Watemu (ukoo wa Temu) na si mahali pengine popote pale. Hatuna sababu ya kubishana juu ya mahali pa kumzika Emmanuel,” alisema Dk. Temu.

Dk. Temu alihitimisha waraka wake kwa kusema kuwa, mdogo wake (Jacob) hana haki yoyote ya kudai kuwa shamba la baba yao (marahemu mzee Temu) ni lake yeye kwa sababu hawajaligawa.

MREMBO AFIA GESTI ARUSHA..USHIRIKINA WHUSISHWA JUU YA KIFO CHAKE




MREMBO mmoja ambaye alihu-dumu kwenye nyumba ya kulala wageni na baa (jina tunalo) iliyopo Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Blandina Michael (33) amekutwa amekufa kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo huku chanzo cha tukio hilo kikihusishwa na vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu mmiliki wa nyumba ya wageni moja ambaye pia anajihusisha na biashara za madini (jina tunalo) kwamba alimtoa kafara mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa, kila mwaka mtu mmoja katika biashara zake hupoteza maisha ghafla.

Hata hivyo, mfanyabiashara huyo alipoongea na Uwazi juzikati alikanusha vikali tuhuma hizo na kueleza kuwa yeye ni muumini mzuri wa imani yake.
‘’Hao watu wanapotosha sana, unajua kuna mwaka mwanaume mmoja alikufa ghafla kwenye nyumba yangu ya kulala wageni, alikuja na mpenzi wake ila alimeza Viagra ambazo hata polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na mimi tukio hilo wanaliunganisha na hili kwamba nawatoa kafara,” alisema.

Kifo cha Blandina kilitokea ndani ya chumba huku mtu mmoja anayedaiwa kuwa mpenzi wake aliyejulikana kwa jina moja la Timo, mkazi wa eneo hilo akihojiwa na polisi.
Marehemu Blandina ambaye ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga, anaelezwa na bosi wake huyo kwamba alikuwa kama mtoto wa familia yake kwa vile alimwamini sana. Alifanya kazi hapo kwa miaka 8 na hakuwa na tatilo la kiafya.

Bosi huyo alisema mwili wa marehemu uligundulika baada ya mfanyakazi mwenzake wa kiume kumpigia simu saa 2 asubuhi ambapo simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ndipo alipoamua kwenda kumgongea katika chumba hicho.
Alisema baada ya kufika alishangaa kukuta mlango wa chumba chake uko wazi na alipochungulia alibaini kwamba Blandina alikuwa amefariki dunia.

Hata hivyo, polisi baada ya kufika na kuufanyia uchunguzi wa awali mwili huo hawakugundua kuwepo kwa jeraha lolote linaloashiria kuuawa, ingawa mwili huo ulipelekwa kufanyiwa uchunguzi wa kitaalam katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo.

TASWIRA YA MH RAIS KIKWETE NDANI YA SARE ZA JESHI ENZI HIZO



Pichani ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ndani ya Sare zake za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kipindi hiko. Picha hii inatajwa kupigwa Mwanzoni mwa Miaka ya 80 wakati huo Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete akiwa Jeshini. Picha ni kwa hisani kubwa ya Mdau wa Ukurasa aliyeko Mkuranga.

Monday, February 24, 2014

UZINDUZI WA ALBAMU YA EXTRA BONGO: RED CARPET YA DAR LIVE!


Baadhi ya safu ya wanenguaji mahiri wa kiume wa Extra Bongo.


Amini akishoo Love na Linah (kushsoto) pamoja na mwimbaji wake.


Baadhi ya safu ya wanenguaji wa kike mahiri wa Extra Bongo.


Wanenguaji katika pozi poa.


Khadija Kopa na Abdul Misambano wa TOT.


Khadija Kopa, Misambano na 'Okwi' shabiki wa Yanga.


Lina na 'back-up singer' wake.


Mamaa Winnie Masanja, mama watoto wa mwanamuziki Banza Stone.


Mke wa 'Mkubwa' Said Fela (kulia).


Mmoja wa wanamuziki wa Mashujaa Band, Gado.


TX Moshi Jnr wa Msondo Music Band.












Wadau wa Dar Live.


Wasanii Linah na Amini.

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...