Tuesday, May 27, 2014

MAPICHA:MWILI WA MSANII RECHO KUSAFIRISHWA KWAO SONGEA KWA MAZISHI


MASTAA wa Bongo Muvi wamemlilia msanii mwenzao, Rachel Haule 'Recho' aliyefariki jana saa mbili usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar baada ya kujifungua ambapo mtoto wake alifariki muda mfupi na baadaye yeye akafariki.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve ‘Nyerere’, mwili wa Rachel utasafirishwa kwenda kwao Songea kwa ajili ya maziko. Habari nyingine za msiba zitatolewa wakati wowote na mtandao huu mara tu zinapopatikana.

Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve Nyerere akilia kwa uchungu.

Huzuni tele ikiwa imetawala wasanii waliokuwa viwanja ya Leaders.

Bi. Mwenda akilia kwa uchungu.

Mume wa Rachel aitwaye Saguda akiwa na majonzi.

Mwigizaji Johari akiwa na huzuni.

Cathy Rupia akiomboleza.

Steve akizungumza na wanachama wa Bongo Muvi, viwanja vya Leaders.

Bongo Muvi wakijadili cha kufanya.

Wasanii wakipanga utaratibu wa msiba wa mwenzao.

Wasanii wa Bongo Muvi wakiwa Muhimbili baada ya kupata habari za kifo cha mwenzao.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...