Monday, January 25, 2016

IDRIS AJITOA FAHAMU KWA WEMA, ATANGAZA KIMAFUMBO KUWA MKEWE!

Wema na Idris katika pozi.
Idris & Wema

Kumekuwa na uvumi mkubwa kuwa Idris Sultan na Wema Sepetu wana uhusiano wa kimapenzi na pengine very soon wawili hao watamkaribisha duniani mtoto wao wa kwanza! Kama wewe ni miongoni mwa watu wanaompenda Idris ama Wema Sepetu na utapenda kufahamu aliyoyasema mshindi wa Big Brother Africa 2014, Idris Sultan kuhusu Wema Sepetu na vichwa vya habari za ujauzito, yapo mapya.
Wema Sepetu na Idris Sultan.
Kupitia page yake ya Instagram @Idris Sutlan kafunguka na kusema haya kuhusuWema…

 “ Mimi na wewe sio kama watu wengine. Nalala, nakula na naamka nikiwa nakufikiria wewe. Unafikiri una bahati ya kuwa na mimi ila hapana hapana mimi ndio mwenye bahati ya kuwa na wewe. Mara ya kwanza ilikuwa ajabu kwangu kuangalia ndani ya kabati langu la nguo na kuona nguo zako na viatu au ukiwa unaongea na mimi unaniambia “Hivi baby unahisi akiwa wa kiume utafanyaje maana naona umekazana na wa kike“ au ukiingia jikoni kwangu na kuitawala nyumba yangu na vyakula vizuri. Jinsi unavyowatazama wanawake wengine wakinisogelea, jinsi vile unavyojua ni wakati gani nahitaji kupewa a kiss au kumbatio zito. Jinsi unavyonilazimisha kuangalia channel ya Disney, jinsi unavyoniamsha mapema siku hizi kunitengenezea chai. Naweza nikakuletea ua zuri la waridi lakini halitaweza kufikia uzuri wako. Ukiwa na wivu unasonya sonya, nikiwa na wivu natabasamu. Naweza kufanya lolote hata kuhamisha milimia kwa ajli yako. Nitakulinda, nitakupenda, nitakudekeza, nitakupikia, nitagombana na wewe, tutaangalia movies pamoja, nitakaa na wewe kuangalia nyota. Wewe ni zaidi ya kile nilichokiomba, wewe ni kila kitu changu “My Wife

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...