Wednesday, January 20, 2016

BONDE LA MKWAJUNI LADHIHILISHA UBORA WAKE KATIKA KUJAA MAJI!

Sehemu zilimobomolewa nyumba za wakazi wa bonde la Mkwajuni kufuatia kuwa eneo hatarishi wakati wa kipindi cha mvua.
 MVUA kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo umelifanya Bonde la Mto Msimbaji jijini Dar es Salaam, kufurika kwa maji jambo ambalo limedhihilisha wazi kuwa sehemu hiyo ambayo hivi karibuni  ilishuhudiwa nyumba kibao zikivunjwa ili kuokoa wakazi wa sehemu kuendelea kupata aza ya kuingiliwa na maji ya mafuriko hatimaye sasa imetoa  ishara ya wazi kuwa shehemu hiyo ni hatari kwa  kufanywa makazi ya binadamu.
Mwandishi wetu amefanikiwa kufika eneo hilo na kujionea hali halisi ya maji yakijaa  eneo hilo ambapo zilikuwepo nyumba za wakazi wa sehemu hiyo ambao wamekuwa waking’ang’ania kuendelea kukaa eneo hilo hatarishi.
Mamlaka  zinazohusika na uangalizi wa hali ya hewa  zimesema kuwa mvua zitaendelea kunyesha kwa wingi katika kipindi hiki cha ukanda wa Pwani hivyo wananchi waishio mabondeni wanatakiwa kuchukua tahadhali kubwa ili kuepusha maafa yasiyokuwa ya lazima.
Taswira ya Mto Msimbazi unaotiririsha maji yake katika bonde la Mkwajuni baada ya kunyesha mvua. 
Maji yakiwa yamefurika eneo zilimobomolewa nyumba kufuatia mvua ziliyoanza kunyesha usiku wa kuamkia leo Dar. 
Muonekano wa nyumba zilizosalia eneo hilo baada ya zilizokuwa bondeni kubomolewa. 
Maji yakiwa yamejaa sehemu ya bonde ambapo nyumba zilivunjwa na serikali hivi karibuni. 
Baadhi ya vipande vya mbao vilivyokuwa mapaa ya nyumba zilizo bondeni.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...