Wednesday, January 27, 2016

BELLE 9: KOLABO YANGU NA CHRIS BROWN,AUGUST ALSINA INAWEZEKANA!

Staa wa Ngoma ya Shauri Zao, Abednego Damian ‘ Belle 9’
STAA anayetamba kwa sasa na wimbo wa  Shauri Zao, Abednego Damian ‘ Belle 9’ amesema kuwa kwa muda mrefu amekuwa na shauku ya kutaka kufanya kolabo na mastaa wa muziki wa Marekani, August Alsina pamoja na Chris Brown na kwamba jambo hilo linawezekana kufanyika soon.

Akichonga na mwandishi wetu, Belle9 anayebamba pia na Ngoma ya Burger Movie Selfie, alisema kuwa mastaa hao ni kati ya wasanii ambao amekuwa akiwakubali sana.

“Muziki wetu kwa sasa unakubalika kimataifa na wasanii wameamka sana. Ndoto zangu kubwa si kukimbilia Nigeria wala Sauz kufanya kolabo ila ni kukamilisha ndoto ya kufanya ngoma na Chris pamoja na Alsina,” alisema Belle 9.
 Belle 9


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...