Mkurugenzi
wa Global Publishers LTD, Shigongo Eric James (kulia), akishikilia
vitabu vyake baada ya kumpatia jukumu la uzinduzi huo Mhariri Kiongozi
wa Magazeti Pendwa ya Kampuni hiyo, Oscar Ndauka. Tukio hilo limefanyika
mapema leo ndani ya jengo la ofisi za GlobalPublishers zilizoko
Mwenge-Bamaga jijini Dar es Salaam.
Meneja
Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia), akiwa
amenyanyua moja ya vitabu hivyo baada ya zoezi la kukata utepe wa
uzinduzi kukamilika. Katikati ni mtunzi wa kitabu hicho, Shigongo Eric
James na Oscar Ndauka, wote wakiwa wamenyanyua vitabu hivyo. Vitabu
vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka
Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to
Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni ’26 Secrets – How to
Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.
Shigongo
akimkabidhi jukumu la kukata utepe Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa
Oscar Ndauka (wa kwanza kushoto) huku Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo
Abdallah Mrisho anashuhudia zoezi hilo.
Shigongo
akiwaonyesha mojawapo ya vitabu hivyo baadhi ya wanahabari waliokuwa
wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo (hawapo pichani).
Meneja Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho, akiwakaribisha wanahabari katika uzinduzi huo.
Afisa
Masoko wa Global Publishers Ltd, Benjamin Mwanambuu, akiongea jambo na
waandishi wa habari kabla ya zoezi la uzinduzi huo kuanza.
Shigongo akisaini moja ya vitabu hivyo tayari ya kukitoa kama zawadi kwa baadhi ya wanahabari walioshuhudia uzinduzi huo.
MHAMASISHAJI na mjasiriamali wa kimataifa, Eric
James Shigongo, amewaasa Watanzania kutokata tamaa katika kufuatilia
ndoto zao huku wakiamini kuwa wao ni watu muhimu katika maisha yao na ya
jamii.Akizungumza na vyombo vya habari mapema leo ndani ya ofisi za Global Publishers zilizoko Mwenge-Bamaga jijini Dar katika uzunduzi maalumu wa vitabu vyake vitatu, Shigongo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kusoma vitabu ili kupata maarifa mengi ya juu ya mafanikio maishani.
“Kila mmoja ana ndoto za kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na kuondoka mahali alipo. Wengi hushindwa kupiga hatua za mafanikio maishani kwa sababu nyingi yakiwemo mazingira waliyokulia wakiaminishwa kuwa hawawezi kufanya chochote maishani, jambo ambalo si la kweli kwani kila mmoja anaweza kufikia ndoto zake akiamua tu kubadili fikra na namna ya kutenda mambo maishani,” alisema Shigongo.
Vitabu vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni ’26 Secrets – How to Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.
Uzinduzi wa vitabu hivyo ni kuashiria kwake kuingia rasmi mitaani na kusambazwa kwenye kona mbalimbali ndani na nje ya nchi ambapo vinatarajiwa kubadilisha maisha ya maelfu ya wasomaji watakaofanikiwa kupata siri za mafanikio.
Bei ya vitabu hivyo ni Jumla sh 7,000/=, Rejareja sh 10,000/= Kitauzwa pia kwa Tigo Pesa na M - Pesa. Kwa maelezo zaidi piga namba hizi 0715 063 989, 0759 399 526
(PICHA: MUSA MATEJA, RICHARD BUKOS/GPL)
No comments:
Post a Comment