Akizungumza kwa njia ya simu mwanzoni mwa wiki hii, mzee huyo anayeishi Shinyanga, aliliambia gazeti hili kuwa ni jambo la kutia aibu kuona mzazi mwenzake akimlaumu Lulu wakati ukweli ni kuwa hakuwahi kuwa mke wala kuzaa na marehemu mtoto wao.
Elizabeth Michael ‘Lulu’.
“Mzazi mwenzangu amekosea, Lulu hakuwa ameolewa wala kuzaa na
Kanumba, siyo ukoo wake wala wa Mtegoha, kwa nini anamlalamikia? Amuache
awe huru na maisha yake.“Lulu kama binti anatakiwa kuwa huru kwa
kutayarisha maisha yake, mimi namuunga mkono Lulu na kumbariki katika
maisha yake,” alisema mzee Kanumba.Wiki kadhaa zilizopita, Mama Kanumba aliripotiwa kufanya misa ya kumbukumbu ya kifo cha mwanaye, lakini akatoa maneno makali kutokana na msichana huyo kushindwa kuhudhuria katika shughuli hiyo.
Ilidaiwa kuwa mama huyo alisema Lulu ameacha kuwa karibu naye tofauti na zamani ambako alikuwa akimjali na kumthamini, kitendo ambacho kilienda sambamba na kutoelewana kati yake na mama mzazi wa msichana huyo muigizaji.
No comments:
Post a Comment