Mwandishi Wetu
Mastaa wengi wamekuwa wakiingia kwenye uhusiano na kufanya siri kubwa.
Wapo ambao wanaonekana dhahiri ni wapenzi kutokana na ukaribu wao lakini
wakiulizwa wanadai wana ‘project’.Ukiuliza ni project gani utaambiwa
wana filamu wanacheza. Cha ajabu sasa unaweza kusubiria hiyo filamu na
usiione. Mwisho wa siku unajiongeza na kubaini baadhi wanatumia kivuli
cha ‘project’ kuendesha penzi lao kwa siri.
Utakumbuka hata uhusiano wa mwanamuziki Nasibu Abdul “Diamond’ na
Zarina Hassan ‘Zari’ walianza kwa staili hii. Walijifanya wana kazi ya
kisanii wanafanya lakini kumbe wameshazimikiana na mpaka leo hii ni
wapenzi wanaotarajia kupata mtoto.
Katika siku za hivi karibuni hapa Bongo kuna wasanii ambao nyendo zao
zinaonesha wazi ni wapenzi lakini wenyewe wamekuwa wagumu kuweka wazi.
Ifuatayo ni orodha ya mastaa hao ambao ni kama wako penzini lakini
ushahidi wa wazi hamna.
Juma Musa ‘Jux’ na Vanessa Mdee
Wanamuziki hawa
wamekuwa wakiongozana kila kona, wakati mwingine wakitupia picha za
kimahaba huku watu wao wa karibu wakieleza kuwa ni wapenzi.Hata hivyo,
hakuna hata mmoja kati yao aliyewahi kukiri kwamba wanatoka hivyo suala
la kwamba ni wapenzi au siyo linabaki kuwa siri yao.
Shamsa Ford na Nay wa Mitego
Hawa ni mastaa
ambao ni gumzo mjini. Uhusiano wao kiasi cha kupiga picha wakidendeka na
kuzitupia mtandaoni na hata Shamsa kulala nyumbani kwa Nay kumewafanya
wengi waamini ni wapenzi.
Majibu yao wanapoulizwa wanadai eti wako
kwenye project ya filamu. Mimi na wewe hatuwezi kujua ukweli lakini
mwenye macho haambiwi tazama. Yaani hata kama ni filamu lakini kuna kitu
zaidi ya filamu.
Aunt Ezekiel na Moze Iyobo
Kila mmoja ukimuuliza mimba ya Aunt ni ya nani atakuambia ni ya Moze lakini baadhi bado haiwaingii akilini.
Wapo wanaohisi Moze ni boya tu bali kuna mhusika wa mimba hiyo ambaye huenda hataki kujulikana.
Kilichoibua utata zaidi ni kitendo cha hivi karibuni cha Moze kumuita Aunt dada, watu wakabaki..haah! Dada tena!
Ni kweli haishindikani Aunt kuamua kuzaa na kijana huyo lakini majibu
ya Moze wakati mwingine yamekuwa yakiwafanya watu wahisi kuna ‘kafilamu’
kanachezwa. Yetu macho, sijui akizaliwa mtoto Mwarabu wakati Moze ni
mweusi itakuwaje.
Husna Sajent na Salim Ahmed ‘Gabo’
Madai kuwa
wasanii hawa ni wapenzi yamekuwa yakishika kasi kila siku hadi ikafikia
hatua ikadaiwa wamefunga ndoa ya siri na picha zao zikavuja.Kama ilivyo
kawaida, wasanii hao kwa nyakati tofauti wakadai eti picha zilizovuja
zikionesha wamefunga ndoa ni filamu. Tumebaki njia panda tusijue ukweli
ni upi. Huenda mioyoni mwao wanajua ni wapenzi lakini wanafanya siri kwa
sababu wanazojua wenyewe.
Muna na Kalala
Rose Alfonce a.k.a Muna au Pacha
wa Mainda anadaiwa kuwa kwenye uhusiano uliokolea na Mwanamuziki Kalala
Junior. Wafuatiliaji wa mambo wanadai kuwa, penzi lao limekuwa ni kama
mke na mume kwani wakati mwingine Kalala hulala nyumbani kwa Muna maeneo
ya Mwananyamala.
Wenyewe wakiulizwa wanachengachenga, hasa Muna
lakini kwa watu wenye akili zao wanaona kabisa ni wapenzi kiasi kwamba
siku tukisikia wamefunga ndoa hatutashangaa.
Kuonesha kwamba hawa
watu ni wapenzi, Kalala juzikati alianika hisia zake kwa kutunga wimbo
ulioelezwa kuwa ni maalumu kwa mpenzi wake huyo.
No comments:
Post a Comment