Musa mateja
WAKATI staa wa Bongo Movie, Wema
Sepetu akiweka wazi kuwa hawezi kupata ujauzito huku Judith Wambura
‘Jide’ naye akisumbuliwa na tatizo hilo, nyota wa muziki Rehema
Chalamila, Ray C amefunguka na kusema kuwa hali ya kukosa mtoto ambayo
ni sawa na ugumba, inamtesa, kwani katika umri wake wa miaka 33,
hajabahatika kuwa naye,Risasi Jumamosi linakujuza.
Akizungumza na gazeti hili juzikati, Ray C alisema kuwa pamoja na
hamu yake ya muda mrefu ya kupata mtoto, lakini ameshindwa ingawa
anaamini siku yoyote Mungu atamuwezesha jambo hilo.“Hao kina Jide, Wema
mi naona kama ni cha mtoto. Katika uhusiano wangu wa kimapenzi tangu
nivunje ungo, nimewahi kushika mimba mara moja tu, wakati huo nikiwa na
Mwisho Mwampamba, lakini bahati mbaya ilitoka, tokea hapo sijapata
tena,” alisema staa huyo ambaye yupo katika mapambano ya kuacha matumizi
ya madawa ya kulevya.
Alisema katika umri wake huo anatamani sana kuwa na mtoto, kwani
wasichana aliozaliwa nao wakati mmoja hivi sasa wanao watoto wawili hadi
watatu, kitu ambacho kinamuumiza.Alipoulizwa kama matumizi ya dozi ya
kuacha madawa ya kulevya inachangia tatizo lake hilo, alisema siyo
kweli, kwani miongoni mwa ‘mateja’ wenzake anaokunywa nao dawa, wapo
wajawazito na wengine wenye watoto.
Hata hivyo, alisema umri wake siyo mkubwa sana kukata tamaa ya
kutozaa kwani wapo baadhi ya watu hupata ujauzito na kuzaa katika umri
wa miaka 45 na kuendelea.“Sidhani kama umri ni sababu, nafikiri bado
nina muda wa kuzaa na kumlea mwanangu nikijaaliwa kuwa naye, lakini pia
huwa siishi kumshukuru Mungu kwa hivi nilivyo maana yawezekana kuna
jambo ananiepusha nalo,” alisema.
“Kitu kingine kinachonifanya nisipate mtoto mapema ni pamoja na
kutopata mwanaume aliyetulia ambaye ninaweza kuzaa naye, nadhani
nikimpata mambo yanaweza kwenda vizuri.”Ray C anaingia katika orodha ya
masupastaa ambao licha ya umri wao kuwa mkubwa, lakini bado
hawajabahatika kupata watoto, baadhi yao wakiwa ni pamoja na Judith
Wambura ‘Lady Jaydee’, Baby Madaha na Jacqueline Wolper.
No comments:
Post a Comment