Sunday, April 19, 2015

MASTAA WANAOONGOZA KWA SKENDO ZA NGONO


Mwandishi wetu
Mastaa mbalimbali wa Bongo wamekuwa wakiandamwa na skendo huku baadhi wakiona ndiyo njia ya kujing’arisha kisanii.Skendo zao zimekuwa za aina mbalimbali lakini wengi wamekuwa wakiandamwa na skendo za ngono.Katika makala haya utaipata Top 10 ya mastaa wa kike waliondamwa na skendo za ngono. Baadhi wamekumbwa na skendo za kunaswa kwenye mitego ya kujiuza na wengine wakiingia kwenye listi hii kutokana na tabia ya kubadili wanaume kama nguo.
Jokate Mwegelo.
Kwa maana hiyo kumi bora hii itawagawa katika Kundi A na B ambapo Kundi A ni la wale ambao walikanyaga skendo ya kujiuza na Kundi B ni la waliogandwa na skendo ya ngono kwa tabia zao za kubadili wanaume.
KUNDI A
Mmoja kati ya mastaa wanaoingia kwenye kundi hili ni Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’. Huyu aliwahi kuwekewa mtego na kunaswa baada ya kukubali kujiuza kwa mwanaume aliyemtajia dau kubwa na hatimaye akaingia mkenge.
Lulu Semagongo; aliwahi kuingia kichwakichwa kwenye mtego kama wa Jack Chuz ambapo naye aliwahi kutegeshewa mwanaume na kuulizwa kama anaweza kukubali kuuza ngono kwa kiasi gani.
Wema Sepetu.
Kuashiria kuwa ndo’ zake, akitoa dau lake na mchezo ukaenda hadi gesti ambapo alifumwa laivu na mwanaume huyo kitandani.Baby Madaha; Licha ya kipindi f’lani kudaiwa kuwa kwenye uhusiano na meneja wake aitwaye Joe Kairuki, aliwekewa mtego kwa kutumiwa meseji na mwanaume kuulizwa kama wanaweza kukutana faragha na kwa kiasi gani ambapo naye alitoa dau lake.
Jacqueline Pentzel ‘Jack wa Chuz’.
Hata hivyo, baadaye alishtukia mchezo licha ya mawasiliano yake na mwanaume huyo kuonekana wazi kwamba alikuwa anaelekea kuingia kingi. Isabella Francis ‘Vai wa Ukweli; Naye aliwahi kudaiwa kuyaendesha maisha yake kwa kuigiza na kujiuza pia, akawekewa mtego kama ilivyo kwa wenzake na siku ya tukio, alifika hadi ‘kiwanja’ huku akisisitiza kwamba fedha mbele. Kutokana na maelezo yake hayo, ikaonekana ni kweli huwa anafanya k’abiashara hako’ haramu.
Elizabeth Michael ‘Lulu’.
KUNDI B
Hili ni wale ambao wanasifika kwa katabia ka’ kubadili wanaume kama nguo.
Elizabeth Michael ‘Lulu’; Kiumri anaonekana mdogo lakini naye yumo. Huyu aliwahi kuripotiwa kuwa kwenye uhusiano wa siri na marehemu Steven Kanumba kisha baadaye akadaiwa kutoka na mheshimiwa John Komba (marehemu ambaye aliwahi kukanusha uvumi huo).
Pia binti huyo anadaiwa kuwa eti alikuwa mpenzi wa huyu bilionea wa Arusha aliyefariki dunia, juzikati aitwaye Lusekelo Samson ‘Seki’ ambaye kuna kipindi pia Husna Maulid na Lulu waliwahi kudaiwa kugombana kisa kikiwa ni mwanaume huyo.
Wema Sepetu
Ukiacha wale ambao sisi hatuwajui, Wema amekuwa na msururu wa wanaume huku staili yake ikiwa ni ile ya bandika-bandua. Wanaume ambao wengi ni mastaa waliowahi kumgusa ni Herry Samir ‘Mr Blue’, marehemu Steven Kanumba, Hartman Mbilinyi, Yusuf Jumbe, Chaz Baba, CK na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Huyu pia aliwahi kupiga picha za utupu kadhaa katika kipindi chake cha ustaa, hali inayomfanya afiti kwenye Top 10 hii.
Jacqueline Wolper.
Jokate Mwegelo; ni mwanadada anayeonekana mpole sana lakini naye hawezi kukosekana kwenye orodha hii. Ni kati ya mastaa waliowahi kuwa na uhusiano na wanaume mbalimbali wakiwemo Hasheem Thabit, Diamond aliyempora kutoka kwa Wema na wengine ambao amekuwa akifanya siri.Pia ni kati ya mastaa wanaopenda sana kupiga picha za nusu utupu, tabia inayomfanya wakati mwingine atafsiriwe kuwa anatangaza biashara.
Jacqueline Wolper; Anaingia kwenye orodha hii kutokana na ukweli kwamba amekuwa akibadili wanaume mara kwa mara huku wakati mwingine akiingia kwenye migogoro ya kugombea wanaume.Aliwahi kuingia kwenye mvutano na Husna Maulid wakimgombea mwanaume aitwaye Radjabu Mwami. Pia mwanadada huyu amekuwa akihusishwa na kale kamchezo ka’ usagaji ambapo mwenyewe amekuwa akikanusha mara kwa mara.
Agness Gerald ‘Masogange’.
Agness Gerald ‘Masogange’; Nani asiyemjua mwanadada huyu kwa kupiga picha za nusu utupu huku akidaiwa kuwa ni mmoja wa mastaa ambao wanaendesha maisha yao kwa kutegemea wanaume?Mkanda wake wa ngono uliwahi kuvuja na mwenyewe amekuwa hajali kulianika umbo lake tata.
Stara Thomas; ni staa ambaye amekuwa kwenye gemu la muziki kwa muda mrefu.  Naye anaingia kwenye orodha hii kutokana na madai kuwa, aliwahi kuwa kwenye uhusiano wa siri na marehemu Adam Kuambiana. Pia hivi karibuni mwanaume aliyedaiwa kuwa ni mumewe aitwaye Raumu Ally alimfumania na mwanaume mwingine.
Hao ni baadhi ya mastaa ambao wanaingia kwenye orodha.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...