Jamaa ambaye inasemekana ni rafiki wa karibu wa staa mkubwa wa sinema
za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ aitwaye Morris Sekwao ‘Junior’
inadaiwa amepata msala ‘hevi’ baada ya kutiwa mbaroni nchini Nigeria
akituhumiwa kunaswa na madawa ya kulevya ‘unga’.Habari kutoka kwa mtu wa
karibu wa familia ya Junior zilidai kuwa, jamaa huyo alipatwa na mkasa
huo hivi karibuni nchini humo ambapo alikuwa akitokea Bongo na mzigo
huo.
AKAMATWA UWANJA WA NDEGE NA KILO 25
Chanzo hicho kilidai kwamba
Junior alikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala
Muhammed (MMIA) uliopo Ikeja, Lagos nchini Nigeria, akiwa na madawa hayo
aina ya Ephedrine yenye uzito wa kilo 25.Ilidaiwa kwamba Junior ambaye
ni rafiki wa mastaa mbalimbali Bongo, alidakwa na polisi wa uhamiaji
uwanjani hapo baada ya kutilia shaka begi kubwa alilokuwa amelibeba.
NI BEGI ZIMA
Ilidaiwa kwamba, baada ya ukaguzi alikutwa na begi
zima la unga wenye ujazo huo wa kilo 25 ambao thamani yake haikuwekwa
wazi mara moja.
KAMA MASOGANGE
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ‘ubuyu’ kwamba aina
ya madawa aliyokamatwa nayo ni kama yale aliyokamatwa nayo video queen
wa Bongo, Agness Gerald ‘Masogange’ nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ mwaka
2013.
BOSI YULEYULE
Madai mazito yalishushwa kwamba ‘doni’
aliyembebesha mzigo (aliyemfanya punda) Junior ndiye yuleyule aliyedaiwa
kumbebesha Masogange.Ilisemekana kuwa baada ya kukamatwa, uchunguzi wa
kipolisi unaendelea nchini humo ambapo kwa sheria za Nigeria, jamaa huyo
akikutwa na hatia anaweza kwenda jela miaka kadhaa.
NDUGU WAHAHA
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba kukamatwa
kwa Junior kumewashtua baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki zake kwa kuwa
hawakuwa wanajua kama ndugu yao huyo anafanya kazi hiyo.
KAMANDA NZOWA AFIKISHIWA TAARIFA
Kamanda wa Kikosi cha Kupambana
Dawa za Kulevya Bongo, Godfrey Nzowa alipoulizwa juu ya taarifa za
kukamatwa kwa kijana huyo alisema hajazipata lakini aliahidi kufuatilia
ili kupata undani wake.
KUHUSU JUNIOR
Habari zilizo kwenye makabrasha ya gazeti hili
zinaeleza kuwa Junior ni mtoto wa mjini ambaye mara nyingi hupenda
kuambatana na wasanii mbalimbali Bongo ambapo mara nyingine husafiri nao
nje ya nchi bila kujulikana anapiga dili gani.
NDIYE ALIYEMKIMBIZA LULU USIKU WA KIFO CHA KANUMBA?
Ilidaiwa
kwamba usiku wa kuamkia Aprili 7, 2012 ambapo ndiyo siku kilitokea kifo
cha aliyekuwa mwigizaji mkubwa Bongo, marehemu Steven Kanumba, Junior
ndiye aliyedaiwa kumkimbiza Lulu kutoka nyumbani kwa Kanumba na kwenda
naye kwenye Ufukwe wa Coco kabla ya kukamatwa alfajiri yake maeneo ya
Bamaga-Mwenge jijini Dar.
No comments:
Post a Comment