Musa Mateja
KUFUATIA
sintofahamu kati ya wapenzi wawili, Emmanuel Eribariki ‘Nay wa Mitego’,
ambaye ni msanii wa Bongo Fleva na Siwema Edson juu ya mtoto wao mwenye
umri wa miezi mitatu, mwanaume huyo amesema yupo tayari hata kwa vipimo
vya vinasaba (DNA) ili kuthibitisha kuwa Curtis ni mtoto wake wa damu.
Siwema ambaye Nay anadai kumfumania kitandani akiwa na mwanaume
mwingine mjini Mwanza hivi karibuni, alisema Curtis si mtoto wa Nay,
bali wa mwanaume mwingine ambaye hata hivyo hamtaji.
Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Nay alisema katika mambo
yanayomshangaza na kumfedhehesha ni pamoja na ishu ya mzazi mwenzake
kuropoka kuwa Curtis si mwanaye, kwani anaamini hayo ni maneno ya hasira
na yeye ataendelea kumpenda mtoto wake.
“Ujue najiuliza sana maana ya kuongelea hili jambo mitandaoni, kusema
Curtis siyo mwanangu, kiukweli ninamuacha aongee anavyotaka lakini
nasisitiza kuwa ninampenda sana mwanangu,” alisema Nay wa Mitego.
“Niko tayari kupigana hadi tone la mwisho ili mwanangu aweze kuishi
kwa amani na upendo na wala sioni tena kama kuna haja ya kuyapa nafasi
maneno ya mtandaoni kwa sababu naamini Curtis ni mwanangu na nipo tayari
hata kupima DNA nikibaini siyo wangu nitajua la kufanya,” alisema Nay.
No comments:
Post a Comment