Tuesday, July 24, 2012

KAMPUNI YA PRIME TIME PROMOTIONS LTD YATOA RAMBI RAMBI YA SHILINGI MILIONI MOJA KWA SERIKALI YA ZANZIBAR KUFUATIA AJALI YA KUZAMA KWA MELI YA MV SKAGIT.



Mratibu wa Coconut Fm Ali Khatib Dai (kushoto) akimkabidhi rambirambi makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/-) ofisini kwake Vuga mapema leo

Meneja wa Coconut Fm Husna Abdul akisalimiana na Makamu wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar walipokwenda kukabidhi rambirambi kufuatia ajali ya meli ya MV Skagit.

Makamu wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa maelezo kwa mratibu wa Coconut Fm Ali Khatib Dai kuhusiana na hali inayoendelea kuhusiana na ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagit

Prime Time Promotion kupitia kituo chake cha redio Coconut Fm kimekabidhi rambirambi ya kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/-) kwa makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kufuatia na kuguswa kwake ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagit.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...