Tuesday, July 24, 2012

WEMA SEPETU ALIVYOSAIDIA WATOTO WA KITUO CHA GOOD HOPE JIJINI ARUSHA.



Balozi wa kituo cha "Good Hope" Wema Sepetu katika pose kabla ya kueleka kituoni hapo.

Mgeni rasmi Wema Sepetu akiwa amempakata mtoto mmoja wapo wa kituo cha Good Hope kilichopo Jijini Arusha

Pendo ambaye ndo aliandaa shughuli hiyo akiongea machache

Apparently watoto wa kituoni hapo walipoulizwa yeye ni nani wakajibu yeye anaitwa Wema na huwa wanamuona kwenye magazeti na TV lakini mtoto huyu pichani akawaambia wenzake wamekosea na kusema huyu anaitwa Wema "DIAMOND"

Mlezi wa kituo cha Good Hope akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Wema Sepetu

Baada ya risala kusomwa, mgeni rasmi mwanadada Wema Sepetu aliongea yake machache na kuahidi kusaidia kuhakikisha watoto hao wanapata elimu. Pamoja na hayo Wema aliwanunulia TV na kukabidhii pesa taslimu dola 1000 za kimarekani.

Pichani ni Wema akikabidhii pesa hizo $1000 kwa mlezi wa kituo hicho


Gaudensia akimshukuru Wema kwa msaada alioutoa na kwa kuitikia wito na kufika kituoni hapo

  Pendo akimkumbatia Wema huku akilia machozi ya furaha

Shosti wa Wema Snura nae alikuwepo

Watoto wa kituoni hapo wakiwa katika picha na Wema nasikia kuna kastory behind these two boys hope tutaisikia soon.....

Mambo ya Disco Malapa ndani ya A Town

  Wema akiwa katika picha ya pamoja na marafiki zake

Hongera sana Wema kwa roho yako safi, hakika wewe ni mfano wakuigwa. 

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...