Friday, February 26, 2016

SKY LIGHT BAND YAWAPAGAWISHA MASHABIKI ZAKE NDANI YA MAISHA BASEMENT

Badhi ya mashabiki wa Sky Light Band  wakicheza kwa staili ya pamoja ndani ya ukumbi wa Maisha Basement.

 USIKU wa kuamkia leo Sky Light Band iliendeleza kutoa burudani zake ndani ya Ukumbi wa Maisha Basement Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ambapo mashabiki kibao walihudhuria na kujumuika kwa pamoja kupata muziki muzuri uliokuwa ukipigwa na bendi hiyo.
Waimbaji wa Sky Light Band wakiwapagawisha baadhi ya mashabiki zao waliojitokeza kufuatilia burudani zao ndani ya Ukumbi wa Maisha Basement Kijitonyama jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo.
Muimbaji wa Bendi hiyo Sone Massamba (katikati), akiongoza burudani hizo huku mmoja wa mashabiki zake akionyesha hali ya kupagawishwa na sauti yake.
Waimbaji wa Sky Light Band wakiimba kwa hisia kali.
Badhi ya mashabiki wa bendi hiyo wakicheza kwa staili ya pamoja.
Sone Massamba akiwaonyesha mashabiki zake staili ya kucheza mmoja ya wimbo wa bendi hiyo.
Mashabiki wakijaribu kuiga staili walizoonyeshwa.
…Wakionyesha uelewa wao baada ya kufundishwa kucheza.




No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...