Friday, January 1, 2016

ETI KIDOA AMTANGAZIA VITA ZARI KWA DIAMOND!?


Video Queen maarufu Bongo, Asha Salum ‘Kidoa’.

Musa mateja
Video Queen maarufu Bongo, Asha Salum ‘Kidoa’ amemtangazia vita mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’ akidai atafanya kila njia amnase msanii huyo.

Rafiki wa karibu wa Kidoa aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini alidai kuwa, Kidoa alikuwa akimpenda sana Diamond hata kabla ya kuwa na Zari ndiyo maana ana ndoto za kuwa naye.

“Kidoa anamzimia sana Diamond, achilia mbali kumpenda kutokana na kazi yake ya muziki lakini pia kimapenzi, maana kuna wakati anakosa raha kabisa anapowaona Zari na Diamond wakiwa kimahaba,” anadai mtoa habari huyo.

Katika kujua ukweli wa habari hii, mwandishi wetu alimtafuta Kidoa ambapo bila kuficha alianika hisia zake kwa kusema: “Kiukweli nampenda sana, najua Zari hawezi kujisikia vizuri kusikia maneno haya lakini ndiyo hivyo na niko tayari kwa lolote…

“Nilipotangazwa kuwa msanii mwenye mvuto kwa mwaka 2015, kama ilivyokuwa kwa Wema mwaka 2013, nilijiona mwenye vigezo vya kuwa naye, si yeye ni sukari ya warembo? Na mimi napenda sukari.”

Hivi karibuni Kidoa na Diamond walikutana ndani ya Ukumbi wa Dar Live na kufanikiwa kuongea, kupiga picha na kubadilisha namba za simu, jambo lililotafsiriwa na wadaku kuwa, Zari akilemaa, ameliwa.
Mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...