Mwandishi wetu
IMEBAINIKA! Kufuatia tabia yake
ya kubadili wanaume, mrembo asiyeishiwa matukio Bongo, Wema Isaac Sepetu
imefahamika kuwa chanzo cha yote ni kusumbuliwa na ugonjwa ujulikanao
kitaalamu kwa jina la Sex Maniac.
Akizungumza na gazeti hili, mtaalam wa
masuala ya utabiri na nyota, Maalim Hassan Yahya alisema kwamba suala la
Wema kubadili wanaume kila mara si kulogwa bali anasumbuliwa na ugonjwa
huo ambao mtu akiwa nao kila wakati anawaza mapenzi na raha yake ni
kufanya tendo la ndoa.
Maalim alidadavua kwamba, ugonjwa huo
hautibiwa na dawa za hospitali kama magonjwa mengine ila kama mtu
anahitaji kuondokana na tatizo hilo anatakiwa kumtafuta mwanasaikolojia
ambaye mara kwa mara atakuwa anamjenga kwa ushauri hadi atakapoona
amekuwa sawa kwa kuacha kuwaza mambo hayo.
“Watu wanashindwa kuelewa, unakuta mtu
anakuwa na wanaume wengi, anabadili kila mara alafu watu wanamsema bila
kujua kwamba ni ugonjwa ambao mtu anajikuta akipenda ngono kila wakati
na kwenye mawazo yake anatawaliwa na kutamani tendo la ndoa tu.
“Lakini wapo wengine wanabadili mabwana maarufu ili nao wawe maarufu,” alisema Maalim.
Wema aliwahi kutoka kimapenzi na wanaume
tofauti akiwemo, Herry Samir ‘Mr. Blue’, Khaleed Mohamed ‘TID’,
marehemu Steven Kanumba, Yusuf Jumbe, Tuesday Kihangala ‘Mr Chuz’,
Charles Gabriel ‘Chaz Baba’, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, CK na
Nagari Kombo.
Jitihada za kumpata Wema ili kuzungumzia
hali hiyo ziligonga mwamba baada ya simu yake kutokuwa hewani na
kukosekana nyumbani kwake hivyo jitihada zinaendelea.
No comments:
Post a Comment