Safi sana! Mwigizaji Wastara Juma Issa Abeid na Mtangazaji Lulu
Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’, wamepatana baada ya kuwepo kwa mkwaruzo
kati yao kwa muda mrefu, kisa kikielezwa ni mwanaume ambaye ni mwigizaji
wa Bongo Movies, Bond Bin Sinan, Ijumaa Wikienda limehusika.
Mwigizaji Wastara Juma Issa Abeid na Mtangazaji Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu wakiwa katika pozi.
Kwa mbwembwe na mapozi tofauti, huku wakiachia sentensi zilizoashiria
kila dalili na ishara za ubongo kuchanganyikana na ‘maji ya Ilala’
(pombe) wawili hao walinaswa katikati ya wiki iliyopita ndani ya Ukumbi
wa Escape One, Mikocheni jijini Dar kulikokuwa na harusi ya msanii
mwenzao, Haji Adam ‘Baba Haji’.
Awali, mastaa hao walikuwa wameketi viti tofauti huku shamrashamra za
sherehe zikiendelea, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida wakati wa
kuondoka, Wastara alimfuata Anti Lulu kwa madai ya kumuaga, ndipo
wakasindikizana hadi nje ya ukumbi.
Kabla
ya Wastara kuingia kwenye gari lake, wawili hao walikumbatiana kwa
furaha huku wakiangua vicheko vya ‘kushabikia ushindi’, jambo lililozua
miguno na viulizo miongoni mwa wasanii wenzao.
Ndani ya dakika sifuri, Ijumaa Wikienda lililokuwa limepenyeza
‘kijumbe’ wake kwenye pati hiyo, liliwafotoa picha kisha kuwahoji
kulikoni wawe na furaha ya namna hiyo licha ya kuwepo kwa tetesi
zikiwahusisha na bifu?
“Sisi ni wanawake, hatuwezi kununiana,” alisema Wastara na Anti Lulu kushadadia.
No comments:
Post a Comment