Wednesday, June 10, 2015

JOKATE AWAGOMEA WAGOMBEA URAIS 2015


 

MWANAMITINDO na mtangazaji maarufu Bongo, Jokate Mwegelo amewagomea wagombea urais wote waliotangaza nia cha kuingia ikulu Oktoba, mwaka huu.
 
Mwanamitindo na mtangazaji maarufu Bongo, Jokate Mwegelo.
Jokate aliyasema hayo alipoulizwa na Global TV Online Ijumaa iliyopita kuhusu kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 kuwa, amejiandaaje na yupo kambi gani kati ya wagombea urais waliotangaza nia na wale ambao bado.“Hadi sasa sipo katika chama chochote na sitaki kuitwa wala sitegemei kujiunga na timu yoyote ya wagombea urais wa mwaka huu,” alisema Jokate.
Wagombea wanaotarajiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha urais ni Edward Lowassa (CCM), Benard Membe (CCM), Mwigulu Mchemba (CCM), January Makamba (CCM), Dk. Slaa (Chadema), Ibrahim Lipumba (Cuf) na wengine wengi.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...