MWANAMITINDO na mtangazaji maarufu Bongo, Jokate Mwegelo amewagomea wagombea urais wote waliotangaza nia cha kuingia ikulu Oktoba, mwaka huu.
Mwanamitindo na mtangazaji maarufu Bongo, Jokate Mwegelo.
Jokate aliyasema hayo alipoulizwa na Global TV Online Ijumaa
iliyopita kuhusu kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 kuwa, amejiandaaje na yupo
kambi gani kati ya wagombea urais waliotangaza nia na wale ambao
bado.“Hadi sasa sipo katika chama chochote na sitaki kuitwa wala
sitegemei kujiunga na timu yoyote ya wagombea urais wa mwaka huu,”
alisema Jokate.Wagombea wanaotarajiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha urais ni Edward Lowassa (CCM), Benard Membe (CCM), Mwigulu Mchemba (CCM), January Makamba (CCM), Dk. Slaa (Chadema), Ibrahim Lipumba (Cuf) na wengine wengi.
No comments:
Post a Comment