Mkuu
wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa
(katikati) akimsikiliza jambo Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya
Diamond Platinumz (kulia) na balozi wa Mziiki ambayo ni programu ya simu
za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania iliyozinduliwa jana wakati
wa Zari White Party iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini
Dar es Salaam jana.
Msanii
wa muziki wa Bongo Flavor Diamond Platinumz (wa pili kutoka kushoto) na
balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya
Vodacom Tanzania akiwaonyesha program hiyo waandishi wa habari (hawamo
pichani). App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani.
Wengine katika picha ni Maofisa Mawasiliano wa kampuni hiyo, Abigail
Ambweni(wa kwanza kushoto) na Glory Mtui.
Ofisa
Mawasiliano na Matukio wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni (kulia)
akihojiwa na mtangazaji wa Clouds TV wakati wa uzinduzi wa program ya
Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom
Tanzani.
No comments:
Post a Comment