Saturday, May 2, 2015

VODACOM TANZANIA YAZINDUA PROGRAMU YA MZIIKI NDANI YA ZARI WHITE PARTY


Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa (katikati) akimsikiliza jambo Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz (kulia) na balozi wa Mziiki ambayo ni programu ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom  Tanzania iliyozinduliwa jana wakati wa Zari White Party iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana.
Msanii wa muziki wa Bongo Flavor Diamond Platinumz (wa pili kutoka kushoto) na balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania akiwaonyesha program hiyo waandishi wa habari (hawamo pichani). App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani. Wengine katika picha ni Maofisa Mawasiliano wa kampuni hiyo, Abigail Ambweni(wa kwanza kushoto) na Glory Mtui.
Ofisa Mawasiliano na Matukio wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni (kulia) akihojiwa na mtangazaji wa Clouds TV wakati wa uzinduzi wa program ya Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzani.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...