Thursday, May 14, 2015

ROSE NDAUKA, MANECKY LAIVU!

MAHABA niue! Staa wa sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka na Prodyuza wa Lebo ya AM Records, Emmanuel Saimon Sawando ‘Manecky’ wamenaswa ‘laivu’ wakiwa katika mapozi ya kimahaba mazito jambo lililozua minong’ono miongoni mwa wengi.
Staa wa sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka akiwa na Prodyuza wa Lebo ya AM Records, Emmanuel Saimon Sawando ‘Manecky’.
Tukio hilo lilishuhudiwa na mwandishi wetu lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Klabu ya New Maisha, Oysterbay jijini Dar kulikokuwa na shoo kali ya Mrs. Mabeste Charity  iliyohudhuriwa na mastaa mbalimbali wa filamu na muziki.
Awali, mwandishi wetu alimshuhudia Manecky ukumbini humo akiwa mpole kwa mapozi ya ‘kusikiliza misa’ kabla ya jicho la ‘kiranja’ wetu halijamuona Rose Ndauka.
Hata hivyo, muda mfupi baadaye, Rose alitinga na kinguo cha kutafunia bata huku akionekana amechangamka kwa ‘ulabu’ (pombe), sanjari na rafiki zake.Kama kawaida yake, akiwa na akili za usiku, Rose alianza kupita sehemu tofauti ukumbini humo huku akionekana kumchangamkia kila aliyekuwa mbele yake.

Manecky akifurahia jambo.
Kama haitoshi, muda mwingi alikuwa akiutumia kucheza kila muziki uliopigwa huku mauno yake yakionekana kuwaumiza wanaume wakware.Baadaye, Rose alimfuata Manecky aliyekuwa amekaa kwa kujiegemeza ukutani kwenye moja ya kona iliyojificha huku akipata ‘mbili tatu za baridi’.
Ule utulivu wa awali aliokuwa nao Manecky kabla ya Rose, ulianza kuwa msamiati mgumu kwani walichangamkiana huku wakioneshana mapozi ya kiuchokozi ikiwemo kushikana bila kuwa na nidhamu ya mikono.Akiwa anajua anachokifanya ukumbini kwa usiku huo mnene, haraka mwandishi wetu aliseti kamera yake na kuanza kuwanyemelea lakini kabla hajafanya chochote, Rose alikurupuka huku akimuita mwandishi wetu na kumsihi asipige picha.
“Usijaribu kupiga picha kabisa, tutakosana na kuharibiana sasa hivi,” alisikika Rose kwa sauti iliyojaa hasira lakini haikumzuia mwandishi wetu kutekeleza majukumu yake.
Staa wa sinema za Kibongo, Rose Ndauka.
Baada ya kupiga picha kwa shida, mwandishi wetu aliwafuata na kuwauliza kama wameamua kuanzisha ‘edeni’ yao ambapo Rose alionekana kuwa msemaji mkubwa kwa kumfokea mwandishi wetu na kukwepa swali la msingi huku Manecky akiwa kimya.Hata hivyo, wawili hao waliachana kwa kila mmoja kushika njia yake huku Rose akiambatana na rafiki zake na Manecky kuendelea na ‘hamsini’ zake.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...