Monday, May 18, 2015

PATI 2 YA PADRI ALIYENASWA NA MREMBO

KISA cha Padri Anatoly Salawa (pichani) ambaye pia ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, Tec), kunaswa hivi karibuni kichakani akiwa na mrembo, kimechukua sura mpya, Gazeti la Kufichua Maovu, Uwazi linakokotoa.
Padri Anatoly Salawa akitaharuki baada ya fumanizi hilo.
TUJIKUMBUSHE
Tukio hilo la kushangaza lilijiri hivi karibuni majira ya saa 8: 02 usiku ambapo padri huyo na mrembo walinaswa ndani ya gari aina ya Toyota RAV 4 lenye namba ya usajili T 674 ADA kwenye kichaka kilichopo maeneo ya viwanda na gereji za magari makubwa, Kurasini jijini Dar.

Gazeti ndugu na hili, Ijumaa la Mei 15, mwaka huu liliandika kwa kina habari hiyo ikiwa na kichwa kisemacho; PADRI WA KATOLIKI ANASWA KICHAKANI!
YALIYOJIRI SASA
Kabla ya tukio hilo halijapachikwa kwenye Gazeti la Ijumaa, Padri Salawa alipigiwa simu mara kadhaa ili kupewa nafasi ya kujitetea lakini hakupokea na hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwa simu ya mkononi, hakujibu.

Gari aina ya Toyota RAV 4 lenye nambari ya usajili T 674 ADA alilonaswa nalo Kiongozi huyo wa dini.
GAZETI LATOKA, AWEKWA KITI MOTO
Kwa mujibu wa mtu wa karibu kutoka ofisi za Tec, Kurasini jijini Dar (jina tunalo) aliliambia gazeti hili juzi kuwa, baada ya Gazeti la Ijumaa kuingia mtaani, Ijumaa iliyopita, wakuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki walimuweka kikao padri huyo kwenye Ofisi za Tec na kumtaka aweke wazi kisa chote.


“Jamani mmeua bendi huku Tec. Mnajua kama Padri Salawa amewekwa kitimoto kikali sana? Yaani ni tatizo kubwa,” kilisema chanzo hicho.Kikaendelea: “Baada ya Gazeti la Ijumaa kutoka, maaskofu, mapadri nchini kote walishtuka! Kumbe magazeti yenu yanafika nchi nzima! Mimi nilikuwa sijui.
“Ilibidi awekwe kikao na kuulizwa nini kilitokea mpaka ametoka kwenye gazeti tena kichakani na mrembo halafu mbaya zaidi usiku mnene, ndipo akaanika kisa chote.”
Mrembo aliyenaswa kichakani na Kiongozi wa dini.
PADRI ASIMULIA
Kwa mujibu wa chanzo hicho, padri huyo alisimulia kilichompata ambapo alisema kuwa usiku wa siku ya tukio, yeye alikuwa kwenye baa moja iliyopo maeneo ya Kurasini ambapo huwa kunakuwa na muziki.“Alisema akiwa kwenye baa hiyo, alitokea msichana huyo na kumwomba ampeleke nyumbani kwake maeneo yaleyale kwa vile yeye ana gari na ni usiku.

“Akasema alimkubalia lakini alimwambia anamchukua mtu mwingine waongozane wote, yule msichana akakataa, akasema waende wawili tu.”
PADRI AINGIA LAINI, WAONDOKA
“Padri akazidi kusimulia kwamba, waliingia kwenye gari na msichana huyo, waliondoka kuelekea alikoomba kupelekwa ambako si mbali sana na baa hiyo.”

ENEO LA TUKIO
“Maaskofu waliendelea kumsikiliza. Huku akidondosha machozi, akasema kuwa walipofika eneo lililotokea tukio, alisimamisha gari kwa lengo la kumshusha msichana huyo, ndipo ghafla akavamiwa na watu na kuanza kupigwa picha, wengine kutaka kumshika.”

Mrembo huyo akifaa nguo baada ya kunaswa.
ALITUMIA KARETI KUJIOKOA!
“Padri alisema kabla ya kudhibitiwa alicheza kareti kwa vile anazijua ili awasambaratishe lakini kwa vile watu hao walikuwa zaidi ya wanne walimzidi nguvu.”

TURUDI KWA OFM
Uwazi liliwageukia wapiga picha wa Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global Publishers na kufanya nao mahojiano kwa kupitia utetezi wa padri huyo.OFM: “Siyo kweli, baada ya walinzi Wamasai kutupigia simu na sisi kwenda pale ulipita muda. Kwa hiyo kama ni msichana kushuka angeshashuka. Pia, wakati wanakurupushwa ndani ya gari, padri alitaka kujua sisi ni nani, tukatoa vitambulisho vya kazi kuonesha ni waandishi wa habari wa OFM.

Kumbe walinzi wale wa Kimasai, waliwapigia simu polisi ambao tulikutana eneo la tukio. Kingine ni kwamba, walinzi walisema gari hilo limekuwa likienda mahali pale mara kwa mara na walikuwa wakilitilia shaka kwamba huenda ni la wahalifu.“Baada ya kuwafumania kichakani na kuwapiga picha, polisi walichukua namba zetu na kutuambia kwamba watakapotuhitaji watatuita, hivyo padri na mrembo huyo tuliwaacha na polisi.”
Padri Anatoly akijistili baada ya tukio hilo.
MASWALI KWA PADRI
Utetezi wa Padri Salawa unapingana na akili za kawaida. Kwamba, aliombwa lifti na mrembo huyo na alikubali! Je, kama angekuwa adui angetambuaje hilo hususan kwa kitendo cha kumwambia aondoke na mtu mwingine wawe watatu lakini msichana akamkatalia!

Pili, kama kweli alivamiwa, kwa nini yeye alikutwa suruali iko nusu mwilini na msichana hana nguo kabisa? (picha zipo) na kwa nini walikutwa kichakani?Tatu, ni jambo la kawaida kwa mapadri kuwa baa, lakini je, ni sawa kila anayetokea na kuomba kupelekwa mahali inakuwa hivyo kweli?
CHANZO: UWAZI

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...