KISA cha Padri Anatoly Salawa (pichani) ambaye pia
ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la
Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference,
Tec), kunaswa hivi karibuni kichakani akiwa na mrembo, kimechukua sura
mpya, Gazeti la Kufichua Maovu, Uwazi linakokotoa.
TUJIKUMBUSHE
Tukio hilo la kushangaza lilijiri hivi karibuni
majira ya saa 8: 02 usiku ambapo padri huyo na mrembo walinaswa ndani ya
gari aina ya Toyota RAV 4 lenye namba ya usajili T 674 ADA kwenye
kichaka kilichopo maeneo ya viwanda na gereji za magari makubwa,
Kurasini jijini Dar.
Gazeti ndugu na hili, Ijumaa la Mei 15, mwaka huu liliandika kwa kina
habari hiyo ikiwa na kichwa kisemacho; PADRI WA KATOLIKI ANASWA
KICHAKANI!
YALIYOJIRI SASA
Kabla ya tukio hilo halijapachikwa kwenye Gazeti
la Ijumaa, Padri Salawa alipigiwa simu mara kadhaa ili kupewa nafasi ya
kujitetea lakini hakupokea na hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa
maneno (SMS) kwa simu ya mkononi, hakujibu.
GAZETI LATOKA, AWEKWA KITI MOTO
Kwa mujibu wa mtu wa karibu
kutoka ofisi za Tec, Kurasini jijini Dar (jina tunalo) aliliambia gazeti
hili juzi kuwa, baada ya Gazeti la Ijumaa kuingia mtaani, Ijumaa
iliyopita, wakuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki walimuweka
kikao padri huyo kwenye Ofisi za Tec na kumtaka aweke wazi kisa chote.
“Jamani mmeua bendi huku Tec. Mnajua kama Padri Salawa amewekwa
kitimoto kikali sana? Yaani ni tatizo kubwa,” kilisema chanzo
hicho.Kikaendelea: “Baada ya Gazeti la Ijumaa kutoka, maaskofu, mapadri
nchini kote walishtuka! Kumbe magazeti yenu yanafika nchi nzima! Mimi
nilikuwa sijui.
“Ilibidi awekwe kikao na kuulizwa nini kilitokea mpaka ametoka kwenye
gazeti tena kichakani na mrembo halafu mbaya zaidi usiku mnene, ndipo
akaanika kisa chote.”
PADRI ASIMULIA
Kwa mujibu wa chanzo hicho, padri huyo alisimulia
kilichompata ambapo alisema kuwa usiku wa siku ya tukio, yeye alikuwa
kwenye baa moja iliyopo maeneo ya Kurasini ambapo huwa kunakuwa na
muziki.“Alisema akiwa kwenye baa hiyo, alitokea msichana huyo na
kumwomba ampeleke nyumbani kwake maeneo yaleyale kwa vile yeye ana gari
na ni usiku.
“Akasema alimkubalia lakini alimwambia anamchukua mtu mwingine
waongozane wote, yule msichana akakataa, akasema waende wawili tu.”
PADRI AINGIA LAINI, WAONDOKA
“Padri akazidi kusimulia kwamba,
waliingia kwenye gari na msichana huyo, waliondoka kuelekea alikoomba
kupelekwa ambako si mbali sana na baa hiyo.”
ENEO LA TUKIO
“Maaskofu waliendelea kumsikiliza. Huku akidondosha
machozi, akasema kuwa walipofika eneo lililotokea tukio, alisimamisha
gari kwa lengo la kumshusha msichana huyo, ndipo ghafla akavamiwa na
watu na kuanza kupigwa picha, wengine kutaka kumshika.”
ALITUMIA KARETI KUJIOKOA!
“Padri alisema kabla ya kudhibitiwa
alicheza kareti kwa vile anazijua ili awasambaratishe lakini kwa vile
watu hao walikuwa zaidi ya wanne walimzidi nguvu.”
TURUDI KWA OFM
Uwazi liliwageukia wapiga picha wa Oparesheni
Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global Publishers na kufanya nao mahojiano kwa
kupitia utetezi wa padri huyo.OFM: “Siyo kweli, baada ya walinzi Wamasai
kutupigia simu na sisi kwenda pale ulipita muda. Kwa hiyo kama ni
msichana kushuka angeshashuka. Pia, wakati wanakurupushwa ndani ya gari,
padri alitaka kujua sisi ni nani, tukatoa vitambulisho vya kazi
kuonesha ni waandishi wa habari wa OFM.
Kumbe walinzi wale wa Kimasai, waliwapigia simu polisi ambao
tulikutana eneo la tukio. Kingine ni kwamba, walinzi walisema gari hilo
limekuwa likienda mahali pale mara kwa mara na walikuwa wakilitilia
shaka kwamba huenda ni la wahalifu.“Baada ya kuwafumania kichakani na
kuwapiga picha, polisi walichukua namba zetu na kutuambia kwamba
watakapotuhitaji watatuita, hivyo padri na mrembo huyo tuliwaacha na
polisi.”
MASWALI KWA PADRI
Utetezi wa Padri Salawa unapingana na akili za
kawaida. Kwamba, aliombwa lifti na mrembo huyo na alikubali! Je, kama
angekuwa adui angetambuaje hilo hususan kwa kitendo cha kumwambia
aondoke na mtu mwingine wawe watatu lakini msichana akamkatalia!
Pili, kama kweli alivamiwa, kwa nini yeye alikutwa suruali iko nusu
mwilini na msichana hana nguo kabisa? (picha zipo) na kwa nini walikutwa
kichakani?Tatu, ni jambo la kawaida kwa mapadri kuwa baa, lakini je, ni
sawa kila anayetokea na kuomba kupelekwa mahali inakuwa hivyo kweli?
CHANZO: UWAZI
No comments:
Post a Comment