Friday, May 1, 2015

MAHABA NIGARAGAZE, ADUI AWE ‘BABY’ WANGU




Na Musa Mateja
ILIANZA kama utani lakini siku zilivyosonga ndivyo uhusiano wao ulivyowekwa wazi, hao ni watu wawili waliowahi kuwa maadui wakubwa miaka kadhaa nyuma.

Hapo nawazungumzia staa wa filamu Shamsa Ford na msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ambao kwa sasa wamezama kwenye mahaba niue.

Awali, wahusika wote walitumia nguvu kubwa kukanusha juu ya uhusiano wao lakini inatajwa kuwa mahaba yao ndiyo gumzo kuliko ya wengine wote katika Bongo Muvi na yanashika nafasi ya pili katika Bongo Fleva nyuma ya Diamond na Zari kwa sasa.

Awali, uadui wao ulitokana na Nay kuwaponda wasanii wa kike wa Bongo Muvi na kudai wengi wao hawana lolote na kazi yao ni kujiuza, Shamsa alikuwa mmoja wa waliopokea kwa hasira kali na kumbwatukia Nay lakini ule usemi kuwa ‘wagombano ndiyo wapatanao’, ulikuwa unawahusu.

Walipoulizwa juu ya mahabati yao baada ya picha kuvunja mitandaoni wakipeana ‘mabusu’ motomoto hivi karibuni, walisema wana ‘project’ maalum ya filamu.

Sasa inavyoonekana filamu yao imekuwa ya ukweli badala ya zile za kuigiza. Pichani ni jinsi mahaba nigaragaze yalivyotawala katika maisha ya wawili hao.

ambacho kitamtengenezea zaidi kipato.







No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...