Tuesday, May 12, 2015
WASANII BONGO MOVIES NI NANI ALIYEWAROGA?
KWENU wasanii wa Bongo Movies. Bila shaka mko poa na mnaendelea na mishemishe zenu za mjini kama kawaida. Kutokana na ubize wa kazi zenu na zangu, leo nimeona bora niwakumbuke kwa barua.
Mkitaka kujua hali yangu, mimi ni mzima wa afya namshukuru Mungu naendelea na majukumu yangu kama kawaida ambapo moja ya majukumu hayo, ni hili la kuwaandikia barua kuwakumbusha pale ninapoona hamuendi sawa au kuwapongeza mnapofanya vizuri.
Dhumuni la barua hii ni kutaka kuwauliza ni nani amewaroga? Imefika hatua nimeona niwaulize swali hilo kutokana na mustakabali mzima wa mvuto wa sanaa yenu uliopo kwa sasa.Kutokana na kazi yangu, mbali ya kufanya kwa ukaribu na makundi mengine ya kijamii, nimefanya na nyinyi kwa muda mrefu kidogo, najua baadhi yenu mtakuwa ni mashahidi wa hili.
Pointi yangu hapa ni hii. Kuna wakati nyinyi wasanii wa filamu mlikuwa juu sana kimauzo, umaarufu na hata mafanikio kwa jumla. Mlikuwa ndiyo mnaozungumzwa mitaani na kila rika. Si watoto, mama na hata baba zao. Sinema zilikuwa !٪zinakamata!& watu kwelikweli.
Si mnakumbuka kipindi kile mlivyokuwa mnaonekana nyinyi tu hata katika muziki wa bendi, watakuwepo mastaa wengi ukumbini lakini utasikia majina ya wasanii wa Bongo Movies !٪yakirushwa!& ukumbini. Mitaani kwenye !٪vibanda-umiza!& ilikuwa kila mmoja anazungumzia mastaa wa sinema pengine kuliko mastaa wa muziki, wanasiasa na hata wanamichezo. Lakini kwa takriban miaka mitatu iliyopita ufalme wenu umepokwa na Bongo Fleva.
Sasa hivi watoto wanamjua Diamond, Ali Kiba na wengineo lakini si nyinyi tena. Wanafuatilia kazi zao, wanafuatilia habari zao. Wanataka kujua wanafanya nini katika maisha yao ya sanaa kila siku. Mafanikio ya wasanii wa muziki yanaonekana dhahiri. Mashabiki wanaona wanavyovuka mipaka, wanaona wanafanya shoo na kutengeneza mamilioni katika nchi za watu.
Upande wenu kimya kimetawala. Si kwamba hamtoi muvi, la hasha. Mnatoa lakini mvuto umepungua. Watu hawazifuatilii sababu mvuto wenu umeshuka. Sinema mnazitoa, Wabongo hawaoni zile mishemishe za nyinyi kutangaza kazi mpya, kufanya matamasha makubwa ya sinema, kuvuka mipaka ya Tanzania hata kwa kufanya ziara katika nchi za jirani kama ilivyokuwa kipindi kile cha kina Vincent Kigosi !٪Ray!&, Steven Kanumba (marehemu) na wengineo.
Ndugu zangu mbona mliweza kipindi kile halafu sasa mshindwe? Hata kama mnashindwa kwenda kwa pamoja jitihada binafsi zinahitajika. Pigeni kazi za !٪individual,!& vukeni mipaka kwa nguvu zenu tuone mnatoboa.
Msikae mbali na vyombo vya habari, mnajiharibia wenyewe bila kujijua. Fanyeni kazi, zifikisheni kwenye media kazi zenu zitangazwe na si kuweka chuki na waandishi halafu baadaye mnakuja kulaumu kwamba mnatengwa.
Najua mnaweza, naamini mnaweza kuamka na kufanya mambo makubwa ya kushangaza. Fanyeni kweli na sisi tutawapa sapoti! Kutakapokucha
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment