DONGO! Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi
wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa
huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula
makombo.
Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu
alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema
Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba.
Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba
na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu
kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye
Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha
ufalme wa Diamond kimuziki.
Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama
moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje
ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya.
“Hamna jipya waache waendelee kumpigia kampeni (Kiba) lakini mimi
nafanya muziki wangu, mashabiki wanafahamu. Kwa hao watoto wa kike,
hakuna kipya kwangu si kimuziki hata maisha yao binafsi.
“Wema namjua vizuri, Jokate ndiyo usiseme. Mwache huyo Kiba aendelee
kula makombo kwa Jokate kama ameamua kipita njia nilizopita si mbaya,
inaruhusiwa,” alisema Diamond.
Jitihada za kumpata Jokate ili aweze kufunguka kuwa anajisikiaje
kuitwa makombo na Diamond hazikuzaa matuda kufuatia simu yake kuita bila
kupokewa, jitihada zinaendelea.
No comments:
Post a Comment