Musa mateja
MUIGIZAJI
nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’, amedaiwa kumsaliti mpenzi
wake wa siku nyingi, Chuchu Hans baada ya kukutwa akiwa amepozi kimahaba
na mshiriki wa Miss Tanzania mwaka 2011, Husna Maulid katika Ukumbi wa
Escape One, Mikocheni jijini Dar, hivi karibuni.Muigizaji nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ akipozi kimahaba na Husna Maulid.
Wawili hao waliokuwa wamepakatana, walikutwa katika ukumbi huo wakati
bendi mbili kubwa za muziki wa dansi nchini, FM Academia na The African
Stars ‘Twanga Pepeta’ zilipokuwa zikiangusha burudani kabambe ya
kushindana.
Uwepo wa Ray na Husna ulitafsiriwa kuwa ni usaliti kwani muda wote
waliokuwa ndani ya ukumbi huo wawili hao walikuwa wamegandana kimahaba
huku wataalamu wa ubuyu wakikazia madai kwa kusema wawili hao ni
wapenzi.
“Sasa wewe kusoma hujui hata picha huoni? Hawa watakuwa ni wapenzi
tu, haiwezekani mtu mpakatane, mpeane kampani kiasi hiki na mtu ambaye
siyo mtu wako,” alisikika shuhuda mmoja.
Ray ambaye kabla ya kuwa na Chuchu aliwahi kutoka kimapenzi na
mwigizaji Blandina Changula ‘Johari’ na Ruth Suka ‘Mainda’, alionekana
kufurahia kumpakata Husna huku wakipeana kampani ya kuzungumza, lakini
alipatwa na mshtuko mkubwa baada ya kugundua kuwa alikuwa akifuatiliwa
na kamera ya paparazi wetu.
Kutokana na mazingira ya wawili hao ukumbini hapo, paparazi wetu
alishindwa kuzungumza nao juu ya ishu hiyo na hata alipowatafuta kwa
simu siku iliyofuata, simu zao ziliita bila kupokelewa (huenda walijua
wataulizwa nini).Lakini Chuchu, ambaye ndiye ‘mmiliki’ wa Ray hivi sasa,
alipoulizwa kama anajua lolote juu ya ukaribu wa watu hao, alishtuka na
kudai haamini kama Ray anaweza kumsaliti au amewahi kupiga picha na
Husna za kimahaba.
“Khaa! Unasemaje? Mimi siamini labda kama kuna picha zao za pamoja
naomba unitumie Whatsapp nizione maana nashindwa niongee nini, sikujua
kama walienda popote Ray na Husna.”
Mwanahabari wetu alimtumia picha hizo Chuchu lakini hadi tunakwenda mitamboni, mrembo huyo hakuwa amejibu kitu chochote.
No comments:
Post a Comment