Wednesday, April 15, 2015

MASOGANGE ATIMULIWA SAUZ!

HABARI ikufikie kuwa muuza nyago wa video za wasanii wa Bongo Fleva (video queen), Agness Gerald ‘Masogange’ anadaiwa kutimuliwa nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ na sasa amekuwa akionekana Bongo akirandaranda mitaani.
Muuza nyago wa video za wasanii wa Bongo Fleva (video queen), Agness Gerald ‘Masogange’.
TUJIUNGE JOHANNESBURG
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho Masogange ni rafiki yake aliyeko maeneo ya Midland jijini Johannesburg, Sauzi, staa huyo alitimuliwa na mwenye nyumba baada ya kodi ya pango kwisha na kutakiwa kulipa jambo ambalo lilimshinda.
Ilisemekana kwamba mwanaume aliyekuwa akimpa jeuri aliyetajwa kwa jina maarufu la Said 2010 ambaye ni mfanyabiashara, Mbongo aishie jijini humo alimtosa hivyo bidada akarejea Bongo kinyemela.
KUMBE CHANZO NI TUNDA
Habari nzito zilidai kwamba chanzo cha jamaa huyo ‘kumfungia vioo’ Masogange ni baada ya kunasa kwenye penzi la muuza nyago mwingine wa video za wasanii wa Kibongo aliyetajwa kwa jina maarufu la Tunda.
Ilidaiwa kwamba zile mbwembwe za Masogange za kujitundika mitandaoni zilifika mwisho baada ya Said kuhamia kwa Tunda, mtoto mweupe mwenye sura ya mvuto ambaye anaonekana kwenye video za nyimbo za akina Matonya, TID ‘Mnyama’, Christian Bella na wengine wengi.Ilizidi kunyetishwa kwamba, awali, Tunda alikuwa Bongo lakini jamaa huyo alimtumia tiketi ya ndege na sasa anatanua naye Bondeni kwa Madiba.
Masogange akipozi.
UGOMVI
Ubuyu uliendelea kumwagwa kwamba, hivi karibuni Masogange na Tunda waliingia kwenye ugomvi mkubwa huku wakitukanana mitandaoni bila kuanika sababu ya bifu lao.
“Kama ulikuwa unamfuatilia Masogange wiki mbili hivi zilizopita, utagundua kuna mtu alikuwa anagombana naye. Si mwingine ni huyo Tunda ambaye amemdatisha jamaa hadi akasahau kama kuna Masogange.
“Wewe fikiria, Masogange siyo mtu wa kutua Bongo kimyakimya bila kutupia picha kwenye Instagram ili kuwarusha roho wenzake. Siyo kwamba hawezi, sasa hivi yupo juu ya mawe ndiyo maana anajificha,” kilisema chanzo hicho.
SUALA LA URAIA
Chanzo hicho kilipotonywa kuwa mwaka jana Masogange alitamba kuukwaa uraia wa Sauzi na kuukana wa Bongo kilisema:“Mimi nimeishi hapa South Africa (Sauzi) zaidi ya miaka mitano. Nilishaomba uraia miaka kibao sijapata hadi leo, huyo Masogange ni nani wampe uraia kwa siku mbili? Hizo fiksi tu. Kama aliomba sawa lakini hawezi kupewa uraia kirahisirahisi. Kuna process (taratibu) ndefu hadi mtu apate uraia.”
Pasport ya Agness Masogange.
MASOGANGE ATAKWENDA TENA SAUZI?
Chanzo hicho kilizidi kudadavua kuwa siyo kwamba Masogange hatakwenda tena Sauzi kwa sababu ana watu na marafiki kibao nchini humo lakini kwa sasa hana maskani ya kufikia baada ya kutimuliwa.“Anaweza kwenda any time (muda wowote) lakini mpaka awe na uhakika na pa kufikia,” kiliongeza chanzo hicho.
Baada ya kujazwa habari hizo, gazeti hili lilimtafuta Masogange, alipopatikana alisomewa kila kitu ‘eituzedi’ ambapo aliomba chondechonde isiandikwe kwamba ametimuliwa bali yupo Bongo kwa ajili ya mapumziko.
“Jamani si kweli, waambie wahariri nipo huku (Bongo) kwa ajili ya mapumziko tu,” alisema Masogange kwa kifupi.
TUJIKUMBUSHE
Mwaka juzi Masogange alikamatwa Sauzi kwa msala wa madawa ya kulevya ambapo alihukumiwa kisha akalipa faini na kurejea Bongo kabla ya baadaye kutangaza kupata uraia nchini humo.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...