Baadhi
ya wasanii wa Bongo Fleva, Rich Mavoko (wa kwanza kutoka kushoto),
Linah,Barnaba, Joh Makini wakiwa kwenye pozi na mmoja wa mashabiki wao
ndani ya Ukumbi wa Escape One katika shoo ya Usiku wa Ishi Kistaa
iliyofanyika usiku wa kuamkia leo.
Msanii wa Hip Hop, Izzo Business akisaini kwenye moja ya bango la shoo hiyo muda mfupi baada ya kuwasili mahali hapo.
Mtangazaji
wa Clouds FM, Millard Ayo (kulia), akiitangaza shoo hiyo wakati wa
kuanza burudani hizo, pembeni yake alikuwa na muongozaji mwenzake wa
shoo hiyo, Penny.
Mbongo Fleva, Shilole (kulia), akipata kilaji na mmoja wa wasanii wachanga kwenye muziki huo, Rubby.
Mkurugenzi wa Masako wa Vodacom, Kelvin Twissa (kushoto), akipiga stori na msanii wa Hip Hop, Nick wa Pili.
Shilole (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika pozi na baadhi ya mashabiki waliojitokeza kwenye shoo hiyo ndani ya Ukumbi wa Escape One.
Mwigizaji wa Tamthilia ya Mahusiano, Mwinjaku (kushoto) akiwa katika pozi na msanii wa Bongo Fleva, Rubby.
USIKU wa kuamkia leo
kulikuwa na bata mbalimbali zikiendelea katika kumbi za burudani jijini
Dar es Salaam, lakini kati ya kumbi zote bata la nguvu lilikuwa ndani ya
Ukumbi wa Escape One Mikocheni, jijini Dar es Salaam kwenye shoo ya
Usiku wa Ishi Kistaa ambayo iliwakutanisha baadhi ya mashabiki wa
burudani na mastaa mbalimbali wa Bongo Fleva na Bongo Movies ambao
waliinjoi kwa kucheza muziki mzuri sambamba na mashindano ya hapa na
pale.
Miongoni mwa mashindano madogomadogo
yaliyoendeshwa na waandaaji wa shoo hiyo ni pamoja na mashabiki kuimba
akapela ya wimbo wa msanii yoyote kisha kupatikana mshindi ambaye
alitangazwa na burudani ikaendelea.
No comments:
Post a Comment