Monday, March 9, 2015

MAMA WEMA AMZABA VIBAO ASKARI!

Haya ni madai mazito! Mama mzaa chema wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu anadaiwa kumzaba vibao askari wa kampuni binafsi.
Mama mzaa chema wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu.
UJIUNGE NA SHUHUDA
Kwa mujibu wa shuhuda huyo, tukio hilo lililovuta hisia za watu wengi lilijiri kwenye Bandari ya Dar es Salaam, majira ya mchana Ijumaa iliyopita.Kabla ya kushusha stori kamili, Ijumaa Wikienda lilimhoji shuhuda huyo kama anamjua vizuri mama Wema ambapo alithibitisha kuwa ni yeye huku akisapotiwa na wenzake waliokuwa wakisikika kwenye simu.


KUMBE ALIFUATANA NA WEMA
“Nani asiyemjua mama wa staa mkubwa kama Wema? Tena kafuatana na Wema mwenyewe. Kila mtu hapa anamjua ngoja tujaribu kupata picha zake nzuri,” alisema shuhuda huyo kwa kujiamini.
Shuhuda huyo alidai kwamba chanzo cha yote, mama Wema alidaiwa kutumia mlango usio sahihi na alipofuatwa kuelekezwa ndipo likaibuka timbwili zito.

ALIKUWA ANATOKEA WAPI?
“Kinachoonekana alikuwa ameshuka kwenye boti akitokea Zanzibar kwenye shughuli binafsi. Wakati anatoka kuchukua hamsini zake akiwa na Wema, wakapita mlango ambao siyo sahihi.
“Sasa askari wa kampuni binafsi akawafuata na kuwazuia ili kuwapa maelekezo lakini mama Wema alikasirika, akaanza kumpiga vibao.

“Hapo ndipo lilipoibuka timbwili zito kwani askari naye hakutaka kukubali kirahisi.
“Naye mama Wema kuonesha si mtu wa mchezo aligeuka mbogo na kusababisha watu kushindwa kuamini.

MAMA WEMA KAPITIA JESHINI?
“Yaani swali kubwa kila mtu alikuwa anahoji kama mama Wema amepitia jeshini kwa jinsi alivyoonekana ngangari.“Kiukweli yule mama siyo wa kumchezea anaonekana yupo vizuri kimazoezi.

Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
WAMALIZANA POLISI
“Baadaye walipelekana kwenye kituo cha polisi cha pale bandarini wakamalizana lakini tayari ishu hiyo ilishageuka gumzo maeneo hayo.“Hatujui walikubaliana nini zaidi ya kuwaona wakitimua zao kwani hawakutaka kukusanya tena watu,” alidai shuhuda wetu huyo.

MAMA WEMA AOMBA APUMZIKE
Baada ya kumwagiwa tukio hilo la moto, gazeti hili lilimtafuta mama Wema ambaye hakukanusha kutokea kwa tukio hilo badala yake aliomba aachwe kwanza apumzike nyumbani kwake, Sinza-Mori jijini Dar.
“Niache nipumzike kwanza nitakusimulia tukio,” alisema mama Wema.Alipotafutwa kwa mara nyingine hakuwa tayari kutoa ushirikiano hivyo jitihada za kusikia upande wake zinaendelea.

WEMA VIPI?
Kwa upande wake Wema, simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa ikielezwa kwamba alikuwa amebanwa na majukumu.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...